Uchaguzi 2020 Kauli Mbiu ya CHADEMA: Uhuru, Haki na Maendeleo ya watu

Uchaguzi 2020 Kauli Mbiu ya CHADEMA: Uhuru, Haki na Maendeleo ya watu

MOSintel Inc

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2016
Posts
817
Reaction score
593
Wasalaam wakuu,

Poleni sana na shughuli mbalimbali za kujenga taifa.

Sote katika jukwaa la siasa tumekwisha shuhudia la mgambo likilia kwa vyama mbalimbali kuanza kampeni za uchaguzi wa tarehe 28, oktoba 2020.

Tayari vyama vimekwisha anza kunadi sera zao kupitia wagombea wao. Binafsi nimefurahishwa sana na ilani ya chama cha demokrasia na maendeleo, CHADEMA. Kufurahishwa kwangu huko kumetoka na sera zao ambazo kiukweli zinagusa uchumi wa taifa letu(MACROECONOMICS) na pamoja na uchumi wetu sisi wananchi mmoja mmoja (MICROECONOMICS).

Sera za CHADEMA zenye fungamanisho la sekta ya umma na sekta binafsi (PPP or public-private partnership) ni nguzo katika kukuza uchumi wa nchi na uchumi wa watu wake.

Katika sera hizi mgombea wa CHADEMA nafasi ya Urais Mhe. Tundu Antipas Lissu ameanza kuelezea vyema utekelezaji wa sera hizi atakazozisimamia katika kipindi chake cha utawala wa miaka mitano( 2020-2025).

Sera hizi zimekwisha anza kupokelewa na watu wengi maana zinagusa kila kundi ikiwa ni pamoja na Wafanyakazi, Wakulima, Wajasiriamali, Wawekezaji, Wasomi na Wanafunzi wa elimu kuanzia msingi mpaka vyuo vikuu.

Summary ya Sera za CHADEMA katika ilani yake ya 2020:


1. Katiba Mpya (ikiyasimamia maoni ya kamati ya Warioba)

2. Uhuru wa vyombo vya habari.

3. FAO LA KUJITOA LINARUDI
-ukiwa na utayari wa kusitisha mkataba wa kazi, utapokea mafao yako kulingana na mfuko wako mafao.

4. Maduka yasiyotozwa Kodi jeshini yanarudi.

5. Riba za mikopo ya elimu ya juu itashuka kutoka 13% mpaka 3%.

6. Sheria kandamizi zote zenye upendeleo kwa makundi fulani zitafutwa.

7. Maendeleo yatalenga watu na si vitu, kwamba ili nchi ipate maendeleo lazima kwanza watu wake waendelezwe kielimu(maarifa na ujuzi), kiafya na malazi(makazi Bora).


8. Kodi ya ongezeko la thamani VAT itakua 10% kutoka 18% ya Sasa hivi, ili kuchochea na kurudisha matumaini ya watu kurudi katika biashara na kuongeza uzalishaji mali na hivyo kuinua pato la Taifa.


9. Kodi ya ardhi itapunguzwa ili kuifufua sekta ya makazi ambayo katika kipindi hiki cha miaka mitano imefifia.

10. Kupandisha madaraja na mishahara ya wafanyakazi; swala ambalo lipo kisheria na litafanywa na serikali ya CHADEMA chini ya Rais wake Mh. Tundu Antipas Lissu.

11. Mazingira Bora ya uwekezaji. CHADEMA imepanga kuboresha mazingira mazuri ya uwekezaji ikitumia mbinu ya ubia wa sekta ya umma na binafsi katika kuwavutia wawekezaji kupitia punguzo la kodi na uendelezwaji, ufufuaji na uanzishwaji wa maeneo maalum ya kimkakati ya kiuchumi yaani SEZ(Special Economic Zones).

12. Matibabu kwanza malipo baadae; Kupitia bima ya Afya kwa wananchi wote serikali ya CHADEMA imejiandaa kutoa bima kwa wananchi wote ili kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma ya Afya bora katika muda wote. Hii itapunguza vifo ambavyo mara kadhaa vimesababishwa na wagonjwa kukosa fedha za matibabu kwa wakati.


13. Kodi ya wafanyakazi kwenye mshahara (PAYE) haitazidi 8%. Serikali ya CHADEMA chini ya Mh. Tundu Antipas Lissu imepanga kutoza kuchukua kodi ya PAYE isiyozidi 8% ili kupunguza kodi kubwa ambayo ni mzigo kwa Wafanyakazi.


14. Masharti ya mikopo kwa Vijana itakua nafuu. Wanafunzi wa elimu ya juu hawata daiwa madeni yao waliyokopeshwa na HESLB mpaka pale watakapoajiriwa either katika sekta ya umma ama binafsi.

15. Upatikanaji wa Maji Safi na salama kwa gharama nafuu. Serikali ya CHADEMA ikishirikiana na sekta binafsi imejipanga kusambaza na kutengeneza miundombinu ya maji Safi na salama kwa ustawi wa Watanzania.



16. kuboresha miundombinu vijijini. Vijijini ikiwa ndiyo sehemu inayokaliwa na watu wengi ambao ni wazalishaji wa Chakula na malighafi kwa ajili ya viwanda, serikali ya CHADEMA chini ya Mh. Tundu Antipas Lissu imepanga kuimarisha miundombinu vijijini ili kuunganishwa maeneo ya kimkakati ya uzalishaji malighafi shambani na bidhaa viwandani.

Nawasilisha haya machache.

#Mpiga-kura_huru
#Uchaguzi2020
#TUKAPIGE_KURA
#TANZANIA-AFRICA
#VISION2025
#AGENDA2063


images%20(75).jpg
tapatalk_1596959097188.jpg
tapatalk_1596922153722.jpg
tapatalk_1596959220782.jpg
tapatalk_1596922220474.jpg
tapatalk_1596959302139.jpg
 
Day aisee yaani Watanzania wasipomchagua huyu jamaa na wabunge wake na madiwani wake watakua wamechagua kubaki masikini.

Hizi Ni Sera nzuri Sana na of course zinatekelezeka.

Mimi binafsi kura yangu, ya mke wangu na nitahakikisha nawaelimisha majirani zangu, ndugu zangu marfiki zangu hata wale wa CCM wafanyakazi wenzangu na kila nitakapopata nafasi ya kuongea na mpiga kura wamchague Tundu Lissu.
Na wewe Mtanzania mwenzangu fanya hivyo sambaza Sera hizo nzuri kwa kila Mtanzania hata kwa Watoto wa Shule ya msingi ili wakue na ufahamuzuri wa Sera hizo.
 
Wako watu ambao kwa kutojua kwao watabeza wakidai eti pesa za kutekeleza sera hizo zitatoka wapi. Kwa kuanzia nawakumbusha Watanzania wenzangu kuwa taifa letu hili ni tajiri, ni taifa lililobarikiwa, ni taifa lenye vyanzo vingi sana vya mapato. Kwa bahati mbaya taifa hili limehatamiwa na walafi na wezi chini ya genge linalojulikana kama Chama cha Mapinduzi, CCM.

CCM ni chama cha walaji, chama cha wanyang'anyi na chama cha wanafiki na tusipoliondoa hili genge madarakani hatutafaidi hazina ya nchi hii hata tukitambika. Watu wote wazalendo wa kweli waliokuwa na nia ya kulinusuru taifa hili mikononi mwa hawa wakoloni weusi, wamekumbana na mateso makubwa hadi wengine kupoteza roho zao mradi CCM inabaki madarakani.

Nitaendelea...
 
Wako watu ambao kwa kutojua kwao watabeza wakidai eti pesa za kutekeleza sera hizo zitatoka wapi. Kwa kuanzia nawakumbusha Watanzania wenzangu kuwa taifa letu hili ni tajiri, ni taifa lililobarikiwa, ni taifa lenye vyanzo vingi sana vya mapato. Kwa bahati mbaya taifa hili limehatamiwa na walafi na wezi chini ya genge linalojulikana kama Chama cha Mapinduzi, CCM.

CCM ni chama cha walaji, chama cha wanyang'anyi na chama cha wanafiki na tusipoliondoa hili genge madarakani hatutafaidi hazina ya nchi hii hata tukitambika. Watu wote wazalendo wa kweli waliokuwa na nia ya kulinusuru taifa hili mikononi mwa hawa wakoloni weusi, wamekumbana na mateso makubwa hadi wengine kupoteza roho zao mradi CCM inabaki madarakani.

Nitaendelea...
Sio watabeza, ni takataka, alisema atafuta kodi, kwamba Leo kuna kodi 15 kwa wafanyabiashara na hazitaji, kwamba akifuta kodi bidhaa kutoka nje zitamwagika nchini, nani alimwambia tunahitaji kurudi kwenye ukoloni wa kuifanya nchi yetu dampo la bidhaa za mabeberu? UPUUZI.
 
Sio watabeza, ni takataka, alisema atafuta kodi, kwamba Leo kuna kodi 15 kwa wafanyabiashara na hazitaji, kwamba akifuta kodi bidhaa kutoka nje zitamwagika nchini, nani alimwambia tunahitaji kurudi kwenye ukoloni wa kuifanya nchi yetu dampo la bidhaa za mabeberu? UPUUZI.
Hiki ulichoandika ndio UPUUZI wenyewe sasa
 
Hiki ulichoandika ndio UPUUZI wenyewe sasa
Hatuhitaji kuwa dampo la bidhaa, hatuhitaji kuwa koloni tena, hatutauzwa tukijiona, huwezi fanya hayo bila kodi kama hujauzwa..bora tufunge mkanda tukiwa huru.
 
Sio watabeza, ni takataka, alisema atafuta kodi, kwamba Leo kuna kodi 15 kwa wafanyabiashara na hazitaji, kwamba akifuta kodi bidhaa kutoka nje zitamwagika nchini, nani alimwambia tunahitaji kurudi kwenye ukoloni wa kuifanya nchi yetu dampo la bidhaa za mabeberu? UPUUZI.
Unazungumza hayo yote, ukiwa umevaa suruali, shati, saa na viatu kutoka China. Sasa bidhaa gani ambazo hazipo zitamwagika nchini. Wacha kuwa na mawazo finyu.
 
Tatizo sio uzuri wa sera, tatizo ni nani kwa mujibu wa katiba yetu atamuangusha bosi wake ktk mchakato huu wa uchaguzi, naamini kwa katiba tuliyonayo, hata usipopiga kura taarifa itatoka kuwa umeipigia kura ccm!
 
Hatuhitaji kuwa dampo la bidhaa, hatuhitaji kuwa koloni tena, hatutauzwa tukijiona, huwezi fanya hayo bila kodi kama hujauzwa..bora tufunge mkanda tukiwa huru.
Umeona mkuu, hawa jamaa chenga kweli, eti wanajivunia kuifanya nchi dampo la bidhaa kutoka nje, Magufuli anahamasisha viwanda wao wanakuja na mbadala wa kufuta kodi 15 kwa wafanyabiashara na kufanya bidhaa kutoka nje zimwagike nchini, hawajui moja ya sababu ya colonialism hata watoto wa Sekondari wanasoma ilikuwa ni kutafuta sehemu ya kumwaga bidhaa zao za viwandani, hatutarudi kuwa koloni tena.
 
Hatuhitaji kuwa dampo la bidhaa, hatuhitaji kuwa koloni tena, hatutauzwa tukijiona, huwezi fanya hayo bila kodi kama hujauzwa..bora tufunge mkanda tukiwa huru.
Hapo ulipo ushauzwa, ulihaidiwa Noah kutoka kwenye fungu la madini ya Acacia umeishia kula ugali kwa harufu ya samaki.
 
Umeona mkuu, hawa jamaa chenga kweli, eti wanajivunia kuifanya nchi dampo la bidhaa kutoka nje, Magufuli anahamasisha viwanda wao wanakuja na mbadala wa kufuta kodi 15 kwa wafanyabiashara na kufanya bidhaa kutoka nje zimwagike nchini, hawajui moja ya sababu ya colonialism hata watoto wa Sekondari wanasoma ilikuwa ni kutafuta sehemu ya kumwaga bidhaa zao za viwandani, hatutarudi kuwa koloni tena.
Uwe dampo mara ngapi? Dampo la mchina lisilo na viwango, Sanlg, simu feki , nguo za viwango vya chini, na mengineyo mengi.
 
Tundu Lissu hutapata kura yangu tu bali hata harakati zako za urais nitachangia. Hatutapata mtu mwingine mwenye uwezo wa kuitoa CCM madarakani miaka ya karibuni. Chama kilichotawala miaka 60 na kushindwa hata kuwapatia wananchi hatamahitaji muhimu.
 
Unazungumza hayo yote ,ukiwa umevaa suruali ,shati ,saa na viatu kutoka china. Sasa bidhaa gani ambazo hazipo zitamwagika nchini. Wacha kuwa na mawazo finyu.
Zinalipiwa kodi, kupitia kodi hiyo nchi inajengwa na itajengeka to the extent kwamba hatutategemea tena bidhaa zao, bila kodi hakuna kitakachojengwa, hawatakuwa na haja ya kuja kuwekeza as soko la uhakika la bidhaa za viwanda vyao wanalo, hakutakuwa na pato la nje, nguvu ya kimaamuzi ya nchi itatoweka na hivyo tutakuwa koloni, hatutarudi huko.
 
Zinalipiwa kodi, kupitia kodi hiyo nchi inajengwa na itajengeka to the extent kwamba hatutategemea tena bidhaa zao, bila kodi hakuna kitakachojengwa, hawatakuwa na haja ya kuja kuwekeza as soko la uhakika la bidhaa za viwanda vyao wanalo, hakutakuwa na pato la nje, nguvu ya kimaamuzi ya nchi itatoweka na hivyo tutakuwa koloni, hatutarudi huko.
Ni katika vile viwanda 600 mlivovifungua ahera?
 
Zinalipiwa kodi, kupitia kodi hiyo nchi inajengwa na itajengeka to the extent kwamba hatutategemea tena bidhaa zao, bila kodi hakuna kitakachojengwa, hawatakuwa na haja ya kuja kuwekeza as soko la uhakika la bidhaa za viwanda vyao wanalo, hakutakuwa na pato la nje, nguvu ya kimaamuzi ya nchi itatoweka na hivyo tutakuwa koloni, hatutarudi huko.
Yani uwezo mdogo wa kufikili ni shida, Mara hutaki kuwa na bidhaa nyingi nchini utegemee viwanda vya ndani, umebadilika tena eti mnakusanya kodi.
Kweli mtaji wa ccm ni elimu na wametuweza sana kwenye hilo la elimu. Ila tunashukuru Mungu vilaza wanazidi kupungua nchini kwahiyo ccm itaondoka tu ili tupate maendeleo ya kweli.
Zinduka wewe mdanganyika.
 
Tundu Lissu hutapata kura yangu tu bali hata harakati zako za urais nitachangia. Hatutapata mtu mwingine mwenye uwezo wa kuitoa CCM madarakani miaka ya karibuni. Chama kilichotawala miaka 60 na kushindwa hata kuwapatia wananchi mahitaji muhimu.
Mahitaji muhumu yapi atayoyaleta Lissu bila kodi? anataka akatudangishe kwa mabwana zake? anahubiri kufuta kodi na kufanya makubwa, private sector kukamata uchumi wa nchi, atatoa wapi pesa kuyafanya hayo anayoasema ni makubwa kwa wafanyakazi? ni uchumi upi alosomea kwamba akifuta kodi za bidhaa za nje ni tija kwa Taifa? Hopeless kabisa.
 
Hapo ulipo ushauzwa, ulihaidiwa Noah kutoka kwenye fungu la madini ya Acacia umeishia kula ugali kwa harufu ya samaki.
Ni mpumbavu tu ndo aliwaza funguo ya Noah, mie ni mkulima, SGR inajengwa itasaidia kusafirisha kwa gharama nafuu bidhaa zangu za kilimo, Mwl Nyerere HEP linajengwa, litapunguza gharama za umeme na hivyo kupunguza gharama za uzalishaji kwenye hatchery zetu wafugaji, pesa hizi ni pamoja na hizo za Acacia ambazo nyie mlisema tutashitakiwa, nchi hii ni yetu sote si ya wafanyakazi tu, wakati wafanyakazi wakiongezwa mishahara miaka nenda rudi mkulima aliongezwa nini? wafanyakazi wanaelewa hilo na wamefunga mikanda ili kidogo hiki tufaidi sote.
 
Back
Top Bottom