Kauli tata mtaani kwenu

BONNIE GOLD

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2021
Posts
414
Reaction score
805
Upo zako mgahawani, utasikia kauli hizi zenye utata mtupu:

Mhudumu: Vipi umeshawashughulikia wateja?"

Wateja: Aah! Sema kuhudumiwa, siyo kushughulikiwa.

Mhudumu: Karibu Masta, za mzunguko?

Mteja 1 wa kiume: Mzunguko gani, acha ufala wewe.

Mteje 2: Oya shika hela yako (anatoa 10,000).

Mhudumu 2: Mzee hauna ndogo? Tupe ndogo bhana, hii hatuna chenji.

Mteja 3: Oyyyyyyy naomba kitumbua na maziwa. Jana kitumbua chako kilikuwa kitamu kweli kweli.

Mhudumu: Weka kauli sawa, sio kitumbua changu, mi siyo mpishi.

Mteja 4: Ahaaaaaa, shee mkuuu ndugu yangu! Za siku zako, unaendeleaje na hali?

Mhudumu: Wewe, kauli gani hizo, za siku zipi yani, dadavua?

Mteja: Oyy acha leo sina hela, nitakupitishia.

Mhudumu: Weka kauli sawa, sema ntakupitia hela yako baadae, sio ntakuptishia!!Utanipitishia nini sasa, mti au? Acha ujinga.


KWENYE DALADALA

Konda: Makumbusho makumbusho, vipi unaenda?

Abiria: Hamna siendi, ila ukitaka nikupeleke nakupeleka chaap moja.

Konda: Naomba nauli mzee.

Abiria: Ngoja ikisimama nakupa.

Konda: Acha ujinga weweeee!

Huku mtaani ukiambiwa kauli yeyote na vijana hawa, itafakari mara mbili kwanza!

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…