kauli tata ya Nape Nnauye

MKOLA MLIMA

Member
Joined
Dec 9, 2012
Posts
55
Reaction score
15
Jana wakati natazama taarifa ya habari ya saa mbili usiku kupitia kituo cha ITV nimemsikia Nape akiongea na wananchi wa kata ya Kiborloni mjini Moshi, alisema 'wanaounga mkono serikali tatu ni wahuni'. je kauli kama hiyo inapaswa kutamkwa kiongozi kama yeye, ambaye anatambua kuwa maoni yaliyotolewa ni ya wananchi.

kwa maana hiyo wananchi walitoa maoni ya serikali tatu ni wahuni?


Angalizo: kwa hadhi aliyokua nayo Nape anapaswa kuchuja na kupima kauli zake kabla ya kutamka mbele ya hadhara.
 
Nilimsikia, halafu kauli ya serikali mbili ambazo anadai ndo msimamo wa ccm hakuwa anaitamka anafanya kuonyeshea vidole viwili (alama ya cdm) halafu wananchi ndo wanatamka.,
 
Hii katiba huenda isipatikane na tukabakiwa na hii iliyopo, dalili zinaonyesha hivyo.
 
Hilo kopo tupu ndugu, kwa kifupi huyo ni mlopokaji, na hayo ni matusi kwa watanzania, kura haziombwi kwa kuwatukana wapiga kura, sababu hao ndio waliotoa maoni hayo. Pia wanaccm mnadanganywa na Nape, anajifanya kuiponda Chadema ili mjue haipendi, lakini ukweli ni kwamba Nape anaikubali Chadema mwanzo mwisho, angalia mavazi anavyoshona, anashana kama gwanda za Chadema, nawapa pole vijana msiojielewa, mnapoteza muda bure
 
Umefika muda sasa kwa Watanzani kusema BASI INATOSHA!
 

Huku kijana sasa anajichimbia kaburi. Hii ni tabia ya viongozi waliovimbiwa na madaraka, yeye ni nani hasa kujiona ana haki zaidi katika mustakabali wa taifa?

Kiongozi asiyeheshimu mawazo ya wengine na kuwa mvumilivu wa tofauti ya maoni hafai kuongoza hata familia yake. Hii ni caliber ya binadamu ambao siku wakipata madaraka makubwa zaidi ya kuamua hatima ya maisha ya watu huishia kuwa type ya Iddi Amin na Jean Bokassa. Shame on him!!!
 
Huu uzi unaweza futwa au kufungiwa kama ule wa Jana.. kuhusu hayo maneno...

Kikwete alishasema anayoema nape ndio naye pia anasema so wanayapanga kabla ya kuongewa.... Nape kageuza Katiba ya Chama na si ya Wananchi...
 
nahisi kuna uwezekano mkubwa wa kutengua hata maoni ya wengi na kuletewa ya viongozi wachache; Nape ana uhakika gani kama ccm watataka serikali mbili! hadhi ya wajumbe wa tume ya katiba anaiona kuna wanaofanana na uhuni ama anataka kujiona yeye zaidi ya yeyote ndani ya hiyo tume? kwenye mambo ya kitaifa ingefaa sana watu waache kuonyesha uchumia tumbo; kuna wana ccm na watanzania wengi tu ambao hawataki serikali mbili; kama moja imeshindikana wameshaona tatu ni mwafaka. si muda wa kulishana maneno tena!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…