Kauli tata za RC Chalamila kwenye matamko mbalimbali nchini

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Albert Chalamila, akiwa Mkuu wa Mkoa katika mikoa tofauti, alijipatia umaarufu kutokana na kauli zake tata na zingine ambazo mara nyingi ziliwaacha watu hoi. Akiwa katika Mkoa wa Mbeya, aliwahi kusikika akitoa agizo la kuchapa viboko wanafunzi walioteketeza mabweni, jambo lililozua mjadala mkubwa kitaifa kuhusu mbinu za adhabu shuleni. Aidha, alipokuwa Iringa alifunguka alivyokabiliana na kijana aliyevamia nyumabni kwake, huku Dar akidai kudhibiti Wizi wa Transfoma kwa kuwanywesha Wezi Mafuta ya Transfoma.

1. Tulidhibiti Wizi wa Transfoma kwa kuwanywesha Wezi Mafuta ya Transfoma

Chalamila hapa anasema vitendo vya wizi wa mafuta ya transfoma katika mkoa wa Dar es salaam vilikirthiri, hivyo ili kukomesha vitendo hivyo waliamua kuwa yeyote atakayekamatwa anafanya vitendo hivyo atanyweshwa mafuta ya transfoma na mpaka sasa hakuna wizi wa transfoma Dar es Salaam
Your browser is not able to display this video.
2. Akiwa RC MBEYA, Chalamila alisema Bar na Makanisa Shindaneni, Bia inaongeza Kinga
Your browser is not able to display this video.
3. Wakati akiwa Mkuu wa mkoa wa Mwanza wakati akizungumzia ujio wa Rais Samia kwa ziara ya kikazi aligusia suala la Wananchi kujitokeza na mabango mbele ya Rais na kuzua mjadala mitandaoni
Your browser is not able to display this video.
4. Chalamila alivyozungumzia kauli ya kuambiwa mpenda mapenzi
Your browser is not able to display this video.
5. Chalamila alivyodhani Rais akiwa madarakani kwamba hawezi kufariki, "Nilishika moyo wangu na kumuuliza mke wangu au nimekufa na hutaki kuniambia"
Your browser is not able to display this video.
6. Kauli ya Pombe na Kazi
Your browser is not able to display this video.
7. Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila alivyowacharaza fimbo wanafunzi
Your browser is not able to display this video.

Soma, pia Kauli tata za RC Chalamila kwenye matamko mbalimbali nchini
 
Viongozi wa Serikali wa namna hii eti Tiss ndio inajinasibu kwamba iliwafanyia kwanza Vetting ya kina kabla ya kuteuliwa kwao na kuwaona kwamba eti wanafaa kuteuliwa kushika madaraka katika Ofisi za Umma!!

Ridiculous!
 
Zile kauli zake kipindi cha mgomo wa kariakoo na simu2000 ndo niliona jamaa ni fcken. Mtampaje mwalimu wa histori ukuu wa mkoa
 
As a country Hawa watu wanaweza kuonekana wajinga ila wanaumuhimu sanaaa... Hujaelewa kalale
 
As a country Hawa watu wanaweza kuonekana wajinga ila wanaumuhimu sanaaa... Hujaelewa kalale
Ni kweli kabisa, umma unahabarika kwa Habari ambazo kamwe isingewezekana zipatikane kwa njia za kawaida ambazo zimezoeleka, Participant-Observer Whistle blower
 
Toka awe mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, mh. Albert Chalamila amekuwa akitoa kauli tata sana sana sana...
Ebu tuziorodheshe...

Mnikome kama mlivyokoma maziwa ya mama zenu!
.....
Tuongezee...
 
Kichwa MAJI KABISA huyu!
Wakuu wa mkoa wa Dar wanalevywa na hiko cheo aisee!
 
Viongozi wa Serikali wa namna hii eti Tiss ndio inajinasibu kwamba iliwafanyia kwanza Vetting ya kina kabla ya kuteuliwa kwao na kuwaona kwamba eti wanafaa kuteuliwa kushika madaraka katika Ofisi za Umma!!

Ridiculous!
Wewe una uelewa mkubwa sana!
 
Hizo kauli zinawafuraisha sana wana ccm wale wale wanaokwaza na kauli za Tundu Lissu Antipas.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…