Kauli ya Albert Chalamila akigusia Maandamano ya CHADEMA kwa mafumbo, adai yanaweza kuahirishwa

Kauli ya Albert Chalamila akigusia Maandamano ya CHADEMA kwa mafumbo, adai yanaweza kuahirishwa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Albert Chalamila amesema ameamini Ekaristi takarifu inaponya na inaleta undungu, kufuatia kitendo cha Padri Dkt. Charles Kitima kuwakutanisha pamoja Katibu Mkuu wa CCM, Emmanuel Nchimbi, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA-Bara, Tundu Lissu na Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika ambapo Chalamila amesema inawezekana hata yale mengine yaliyopangwa yakaahirishwa kwenye madhabahu.

Chalamila amesema hayo leo September 15, 2024 katika Kongamano la Tano la Ekaristi Takatifu Kitaifa lililofanyika katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es salaaam.

“Ndugu yangu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Ndugu yangu, Baba yangu Emmanuel Nchimbi, kwakweli nimeamini Ekarisiti Takatifu inaponya na inaleta undugu, na inawezekana hata yale mengine yaliyopangwa yakaahirishiwa hapahapa kwenye madhabahu hii” —— RC Chalamila

Ingawa RC Chalamila hajaweka wazi kuwa ni mambo gani anayosema yanaweza kuahirishiwa kwenye madhabahu lakini Watu wanaofuatilia siasa za Tanzania wameitafsiri kauli yake kuwa huenda anazungumzia maandamano yaliyoitishwa na CHADEMA September 23,2024 na kwamba huenda Chalamila anamaanisha kukutanishwa kwa Viongozi hao kunaweza kupelekea maamuzi ya maandamano hayo kuahirishwa.

Pia soma: Tutaandamana kwa sababu ni halali, Polisi wawachukulie hatua hao wanaosema watavunja amani
 
Gen Z wabongo wamelala sana
Hehe yani kelele hizi zote halafu mnakaa kuwategemea gen z bongo,,,,hao wanajulikana ni kizazi cha UTI sugu kwahio kwabongo kama unaweka plan zozote ukiwaweka akilini Gen Z imekula kwako bora kidogo muende kwa millenials panaweza eleweka ila kwa Gen Z mambo yao ndo kama hayo mnayoyaona huko sinza na tabata halafu mtegemee kupata matokeo chanya toka kwao
 
Chalamila hakusoma Newton's laws of motion?

Pasi na kuweka external force mambo hubaki vilevile, CDM wataendelea kutekwa na kuuawawa kama kuku bandani.

Lazima jambo lifanyike, cheche huzaa moto na moto huzaa moto mkubwa. Before you know it the old republic has perished and give way for the new one.
 
Nyerere mwenyewe alikuwa anafaya maandamano.

Alikuwa ndio "dean " of activists .

Sijui hawa walevi huwa wanaokotwa wapi na hawajui historia
images - 2024-09-15T203620.418.jpeg
 
Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama DSM mh Albert Chalamila
Hiyo kamati ya ulinzi ivunjwe.

Watu wanakula kodi na kupata vitambi hawajui wanachotakiwa kufanya.

Matukio hayo yanaogopesha hata kwa wasiokuwepo Tanzania.
 
Unaijua hiyo kamati ya ulinzi inapatikana je? Nimecheka eti ivunjwe, ha ha ha ha
Umemaliza kucheka??

Hakuna kitu kisichovunjwa, kama kungekuwepo na katiba imara ndio maana hata Kenya wamewaonyesha mfano kwa ex- IGP wao vile inafaa .

Ni basi tu banana republic impunity prevails.

Hakuna anayejali.

Kwani Polisi wanafuata PGO yao?

Asilimia 98% hawaifuati wala hawaijui.

Mwisho endelea kucheka tu mpaka siku atakapotekwa mumeo ndio utajua kuna vya kuchekesha na vipo vya kusikitisha.
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Albert Chalamila amesema ameamini Ekaristi takarifu inaponya na inaleta undungu, kufuatia kitendo cha Padri Dkt. Charles Kitima kuwakutanisha pamoja Katibu Mkuu wa CCM, Emmanuel Nchimbi, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA-Bara, Tundu Lissu na Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika ambapo Chalamila amesema inawezekana hata yale mengine yaliyopangwa yakaahirishwa kwenye madhabahu.

Chalamila amesema hayo leo September 15, 2024 katika Kongamano la Tano la Ekaristi Takatifu Kitaifa lililofanyika katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es salaaam.

“Ndugu yangu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Ndugu yangu, Baba yangu Emmanuel Nchimbi, kwakweli nimeamini Ekarisiti Takatifu inaponya na inaleta undugu, na inawezekana hata yale mengine yaliyopangwa yakaahirishiwa hapahapa kwenye madhabahu hii” —— RC Chalamila

Ingawa RC Chalamila hajaweka wazi kuwa ni mambo gani anayosema yanaweza kuahirishiwa kwenye madhabahu lakini Watu wanaofuatilia siasa za Tanzania wameitafsiri kauli yake kuwa huenda anazungumzia maandamano yaliyoitishwa na CHADEMA September 23,2024 na kwamba huenda Chalamila anamaanisha kukutanishwa kwa Viongozi hao kunaweza kupelekea maamuzi ya maandamano hayo kuahirishwa.

Pia soma: Tutaandamana kwa sababu ni halali, Polisi wawachukulie hatua hao wanaosema watavunja amani
Drawing from my extensive experience as an elderly citizen of this nation, I believe Chalamila would be the worst Regional Commissioner the region has ever had since its founding.
 
Back
Top Bottom