Kiherehere
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 1,806
- 622
cHADEMA WAMERUKIA MKUKI KWA MBELE
CHAMA CHA KUIBA AGENDA ZA WENGINE NA KUZIGEUZA KUWA ZAO
SASA WANAADHIRIKA
Kichwa cha dagaa, au cha nguruwe. Come on.Mtikila kichwa sana
big up mtikila
Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila amesema Chadema ilikurupuka na kudandia hoja ya Katiba mpya ya nchi bila kuzingatia maslahi ya Watanzania na kuonya kuwa mchakato wa kuunda Katiba unaweza kushindwa kama utafanywa kwa lengo la kukidhi matakwa ya watu wachache wanaoshinikizwa na wageni.
Akizungumza kwa simu jana, Mtikila alisema si viongozi wa Chadema wenye dhamira ya dhati ya uundaji wa Katiba mpya kwa maslahi ya Watanzania, kwa kuwa wanataka Katiba iundwe, kwa maslahi binafsi kwa lengo la kuendeleza zama za ukoloni.
Mimi nilipojaribu kuzungumzia Katiba mpya na haja ya kuwa na Serikali tatu, watu waliniona kichaa, jambo ambalo lilisababisha kampeni ya kutaka Katiba kuwa ngumu na isiyo na mafanikio sasa watu hao hao wanataka Katiba mpya kwa maslahi yao, alisema.
Hata hivyo Mtikila alimwomba Rais Kikwete, asisahau kumjumuisha kwenye Tume atakayoiunda kwa kuzingatia kuwa ametumia muda mwingi kudai Katiba mpya ya nchi akiwa na dhamira ya dhati.
mtikila ni fisadi hastahili kabisa kuwepo katika Tume ya Katiba. Kama mtakumbuka alishawahi kuumbuliwa na Rostom Aziz kuwa naye Mtikila huenda kuchukua hela ya ufisadi toka kwa RA, na hadi leo hajapinga! Mchungaji haaminiki bora apotezewe tu
Vongozi wengine bwana sasa kama alianzisha yeye kwanini asiungane na wanaodai katiba mpya leo? Kama anataka nae ajumuhishwe kwenye tume hiyo kwanini aseme katiba hiyo ni kwa manufaa ya Chadema? Sasa akiwemo humo itakuwa manufaa ya nani?
Huyu Mzee sijui huwa anawaza nini kweli akili zikizidi huwa zinapitiliza
Mchungaji mtikila ni mtu asiyetabirika na mara zote anaangalia namna ya kupata maslahi kutokana na hoja mbalimbali. Ameanzisha hoja nyingi sana nchini kuanzia Magabachori hadi wazawa lakini hazina nguvu wala mishiko sahihi kwa wachambuzi wa mambo. Huwa anaanza vizuri lakini anakorofisha mahali fulani huko njiani kabla ya kufika. Akiwa kama mtanzania anayo haki ya kuchangia uundaji wa katiba mpya lakini si mtu wa kumwamini kuwa ana nia ya dhati ya kusaidia watanzania. Tarime walimpiga mawe kwa usaliti wake!!!
Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila amesema Chadema ilikurupuka na kudandia hoja ya Katiba mpya ya nchi bila kuzingatia maslahi ya Watanzania na kuonya kuwa mchakato wa kuunda Katiba unaweza kushindwa kama utafanywa kwa lengo la kukidhi matakwa ya watu wachache wanaoshinikizwa na wageni.
Akizungumza kwa simu jana, Mtikila alisema si viongozi wa Chadema wenye dhamira ya dhati ya uundaji wa Katiba mpya kwa maslahi ya Watanzania, kwa kuwa wanataka Katiba iundwe, kwa maslahi binafsi kwa lengo la kuendeleza zama za ukoloni.
Mimi nilipojaribu kuzungumzia Katiba mpya na haja ya kuwa na Serikali tatu, watu waliniona kichaa, jambo ambalo lilisababisha kampeni ya kutaka Katiba kuwa ngumu na isiyo na mafanikio sasa watu hao hao wanataka Katiba mpya kwa maslahi yao, alisema.
Hata hivyo Mtikila alimwomba Rais Kikwete, asisahau kumjumuisha kwenye Tume atakayoiunda kwa kuzingatia kuwa ametumia muda mwingi kudai Katiba mpya ya nchi akiwa na dhamira ya dhati.