Kauli ya mh. Wasira juu ya katiba yaongeza utata

Kauli ya mh. Wasira juu ya katiba yaongeza utata

Bonson

Senior Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
183
Reaction score
147
Ndugu wana JF,
Kauli ya Waziri Wasira kama ilivyoandikwa na gazeti la RAI inaniongezea maswali lukuki kuhusu mchakato mzima wa katiba na umakini wa viongozi wetu. Kwa alichokisema ni kwamba hadi sasa rasimu ya Katiba Mpya bado haijafika kwenye meza ya Mheshimiwa Rais.

Cha kushangaza na kusikitisha na kinachonipa maswali ni kwamba Mheshimiwa Rais aliwezaje kulizungumzia swala la Katiba katika hotuba yake ya mwezi bila kuisoma au hata kuiona nakala ya Katiba yenyewe?? Je, muheshimiwa anawezaje kusimama mbele ya mamilioni ya raia wa Tanzania na kutoa msimamo kwa rasimu ya Katiba ambayo hajaiona wala kuisoma??

Utata mkubwa zaidi ni ujasiri alionao Mzee Wasira kwamba Katiba ikitua tu mezani, Mkuu ataweka saini yake na kuipitisha. Yaani Wasira hatoi nafasi kwa Rais kuisoma na kutoa msimamo binafsi. Hii ni kumuweka Mheshimiwa Rais katika pressure isiyo ya lazima. Kauli ya Mzee Wasira inahitaji ufafanuzi; Nanukuu kauli yake ; “Ninachofahamu muswada ukija Rais atasaini kwa sababu taratibu na kanuni zote zimefuatwa, lakini kama wenzetu wanahitaji kumuona Rais ni sawa, na amesikia wito na amekubali. Tusubiri matokeo ya mazungumzo.” (mwisho wa kunukuu).

Mzee Wasira hakuisikia hotuba ya Rais akisema kwamba Zanzibar haijashirikishwa vya kutosha?? Hivyo basi utaratibu wote haukufuatwa!!

MUNGU IBARIKI AFRIKA; MUNGU IBARIKI TANZANIA!





 
Katika mambo ambayo JK alibugi step ni kumteua Wasira kuwa Waziri wa kuratibu mahusiano mazuri na makundi mbalimbali ya kijamii,vikiwemo vyama vya upinzani.

Huyo mzee badala ya kuboresha,yeye siku zote ansongeza uhasama.

Ngoja niwakumbushe baadhi ya matamshi yake ambayo badala ya kubiresha uhusiano,badala yake yanakuza uhasama.

Si mnakumbuka majuzi aliporopoka na kuviambia vyama vya upinzani kuwa wasitegemee kuonana na Rais kuongelea Ayala la Katiba,kwa kuwa milango ya Ikulu imefungwa??!!

Lakini siku chache zilizofuatia JK,akamwumbua Wasira,kwa kutangaza kuwa yuko tayari kuonana na viongozi wa vyama vya upinzani,na sasa ishakuwa confirmed kuwa JK atakutana na viingozi hao Jumanne ijayo tarehe 15.

Vile vile watanzania bado tunakumbuka jinsi siku za nyuma ambavyo aliwahi kutamka kuwa Chadema itakufa kabla ya mwaka 2015, baadaye ikagundulika kuwa kumbe alitoa kauli hiyo kutokana na serkali yake ya CCM kupanga mipango haramu wakishirikiana na TISS, kuwabambikizia kesi za ugaidi viongozi waandamizi wa Chadema, mpango ambao maccm wamepata aibu ya karne!!

Kwa mazingira hayo inashangaza kuona Wasira bado hajatoa barua ya kujiuzulu wadhifa wake na bosi wske JK bado anashikwa na kigugumizi,anashindwa kumfukuza kazi!!!
 
wote lao ni moja tu.....huwezi kupigana vita na mamba wakati na wewe uko majini....
 
sasa hadi aisome? wakati kashasema
amejulishwa
ameambiwa
ameelezwa?
 
Mhe.Rais anapaswa kuwa makini sana na Mhe.wasira kwa sababu huwa mambo mengi ana kurupuka.hivi Rais kwa nini hadi leo haja mfukuza wasira na badala yake ana pokea ushauri wake wa kupotosha na ubabe kama wa magufuli?
 
Watu tunacho sahau ni kwamba JK ni binadamu makini sana, anasikiliza pande zote alafu anajua afanye nini ahache lipi - in short, is always one step ahead ya wenzake ndani ya chama chake na vyama vya upinzani.
 
sasa hadi aisome? wakati kashasemaamejulishwaameambiwaameelezwa?
Mkuu atachanganya na za kwake alafu atoe kifaa chenye mshiko kwa mstakabali wa Taifa letu, jamaa huyu si mkurupukaji yuko makini sana - give him ample TIME, nina hakika atawashangaza wengi.
 
Wamezoea Kuropoka, Umimi Umezidi Sana Hapa Tz.Waziri Wasira kama ilivyoandikwa na gazeti la RAI inaniongezea maswali lukuki kuhusu mchakato mzima wa katiba na umakini wa viongozi wetu. Kwa alichokisema ni kwamba hadi sasa rasimu ya Katiba Mpya bado haijafika kwenye meza ya Mheshimiwa Rais.

Cha kushangaza na kusikitisha na kinachonipa maswali ni kwamba Mheshimiwa Rais aliwezaje kulizungumzia swala la Katiba katika hotuba yake ya mwezi bila kuisoma au hata kuiona nakala ya Katiba yenyewe?? Je, muheshimiwa anawezaje kusimama mbele ya mamilioni ya raia wa Tanzania na kutoa msimamo kwa rasimu ya Katiba ambayo hajaiona wala kuisoma??

Utata mkubwa zaidi ni ujasiri alionao Mzee Wasira kwamba Katiba ikitua tu mezani, Mkuu ataweka saini yake na kuipitisha. Yaani Wasira hatoi nafasi kwa Rais kuisoma na kutoa msimamo binafsi. Hii ni kumuweka Mheshimiwa Rais katika pressure isiyo ya lazima. Kauli ya Mzee Wasira inahitaji ufafanuzi; Nanukuu kauli yake ; £¿Ninachofahamu muswada ukija
 
Jamani Waungwana Hebu Nisaidieni Hili: Lile Suala La Vitambulisho Vya Uraia Limefikia Wapi
 
Ni mmoja kati ya wale ambao tangu awali hawakutaka katiba mpya hivyo simshangai akiwa kinyume na kila move ya kupata katiba mpya!
 
Jamani Waungwana Hebu Nisaidieni Hili: Lile Suala La Vitambulisho Vya Uraia Limefikia Wapi

Muungwana...Tanzania si kama uijuavyo...pale kuna zaidi ya billion 200. Walisema by 2014 itakuwa tayari. CHANGA LA MACHO.

Nakuhakikishia hadi 2015, hutaona kitu. na watu wanalipana posho na masurufu.
 
Back
Top Bottom