Kauli yenye akili ya Simbachawene: Mh Rais mimi sina nyota hata moja hivyo jukumu la kuvisimamia vyombo vya dola ni lako Amiri Jeshi mkuu

Kauli yenye akili ya Simbachawene: Mh Rais mimi sina nyota hata moja hivyo jukumu la kuvisimamia vyombo vya dola ni lako Amiri Jeshi mkuu

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Naomba niweke wazi hapa nahitaji kueleweshwa juu ya hili suala. Katika hotuba yake Waziri wa mambo ya ndani alidokeza juu ya utawala ndani ya wizara ya Mambo ya ndani, akadai hana nyota na wala yeye si Amiri jeshi mkuu. (Hili nakubali asilimia mia). Hivyo ameonyesha wazi kuwa hatakuwa anamuingilia kiutendaji Mkuu wa Jeshi la Polisi. (Mimi ndio nimeelewa hivyo). Jambo ambalo linaonyesha mtangulizi wake alikuwa akimuingilia kiutendaji maana nimesikia kuwa alikuwa anaambiwa toa huyu weka huyu.

Lakini sheria inayosimamia shughuli za Polisi hapa nchini ( Police Force and Auxilliary Services Act) kifungu cha 7 (1)(2) kinaweka bayana kuwa IGP atafanya kazi kwa mujibu wa amri za Waziri . Kwa ufupi anaripoti kwa Waziri wa Mambo ya Ndani.

Sasa basi nauliza tu je huyu jamaa aliyeondolewa alikuwa anafanya makosa kumpa IGP orders?

Nahitaji msaada ili nieleweshwe.
 
Baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Simbachawene kutoa kauli hii ndipo Mh Rais Magufuli akampongeza kwa kulitambua hilo na kumuambia kuwa hata Waziri Mwinyi amedumu Wizara ya Ulinzi kwa sababu analielewa vizuri jambo hilo.

Rais Magufuli akasisitiza kuwa Wakuu wa vyombo vya ulinzi wanaripoti moja kwa moja kwa Rais ambaye ndiye Amiri Jeshi Mkuu.

Mh Simbachawene amesema yeye atajikita kwenye shughuli za kiutawala na kwa upande wa vyombo vya dola atakuwa anatoa ushauri kwa Mh Rais Magufuli pale inapobidi.

Maendeleo hayana vyama!
 
Aiseh hili sikuwahi kulifikiria kichwani mwangu ingawa several times huwa nawaza mbona Dr. Mwinyi anasurvive pale Ulinzi na usalama bila shida ingawa ndio pagumu?
Kwa maneno rahisi hawa waliotangulia walikosa hekima 'acknowledging the authority' walipokuwa wizarani.
Hapo ndio unapokuja kujua ukikaa kwenye kiti fulani waulize waliokutangulia na wakapita successively ndio usalama wako.
Kwa kauli hiyo ya simbachawene ameshatoboa na nadhani hatowafokea tena wale makamishna.
 
Aiseh hili sikuwahi kulifikiria kichwani mwangu ingawa several times huwa nawaza mbona Dr. Mwinyi anasurvive pale Ulinzi na usalama bila shida ingawa ndio pagumu?
Kwa maneno rahisi hawa waliotangulia walikosa hekima 'acknowledging the authority' walipokuwa wizarani.
Hapo ndio unapokuja kujua ukikaa kwenye kiti fulani waulize waliokutangulia na wakapita successively ndio usalama wako.
Kwa kauli hiyo ya simbachawene ameshatoboa na nadhani hatowafokea tena wale makamishna.
Haha! Mwenzao alikuwa anakula vichwa tu, kumbe kuna mtu anamchora huku anamlia timing.
 
Baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Simbachawene kutoa kauli hii ndipo Mh Rais Magufuli akampongeza kwa kulitambua hilo na kumuambia kuwa hata Waziri Mwinyi amedumu Wizara ya Ulinzi kwa sababu analielewa vizuri jambo hilo.

Rais Magufuli akasisitiza kuwa Wakuu wa vyombo vya ulinzi wanaripoti moja kwa moja kwa Rais ambaye ndiye Amiri Jeshi Mkuu.

Mh Simbachawene amesema yeye atajikita kwenye shughuli za kiutawala na kwa upande wa vyombo vya dola atakuwa anatoa ushauri kwa Mh Rais Magufuli pale inapobidi.

Maendeleo hayana vyama!

Ongera zake. Kajieleza vizuri. Ila hapo naona wanategana na mkuu wake wa kazi
 
Back
Top Bottom