Kauli za kibabe zimekuwa nyingi katika utoaji wa pembejeo za kilimo kuliko uhalisia

Kauli za kibabe zimekuwa nyingi katika utoaji wa pembejeo za kilimo kuliko uhalisia

Chendembe

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2019
Posts
444
Reaction score
488
Tuliamini na kuaminishwa kuwa kilimo ndio UTI wa mgongo wa nchi yetu.

Tafadhali Serikali tusiwatie watu wetu maskini mchanga machoni kwa kuchezea kilimo. Wakulima wengi ni hoehae, ambao ni Serikali pekee inaweza kuwakomboa. Hali ilivyo Sasa ni adaa na dharau kubwa kwa wakulima.

Kauli za kibabe zimekuwa nyingi katika pembejeo za kilimo kuliko uhalisia. Ni mabovu tuu ya watendaji badala ya kutafuta namba Bora ya kuliendea suala la pembejeo. Busara zimeondoka.

Eti mbolea ya ruzuku kwa tiketi!!! Na haionekani, tunakitafuta nini kwa wavuja jasho! Kwanini utaratibu uliotumika katika mafuta wa kuweka ruzuku huko usitumike kwenye mbolea na pembejeo za kilimo? Nani anapanga foleni kupata namba ya ruzuku ili aweze kununuwa mafuta?

Nashauri Serikali kulitazama hili zaidi ya inavyolitizama katika mafuta. Tunawatengenezea wananchi umasikini wa kutupwa na njaa itatamalaki.

Tujifunze kilichotokea kwenye Korosho. Pembejeo kucheleweshwa, kupatikana kwa shida na kutokidhi mahitaji hata ya mkulima mwenye heka moja.

Mhe. Raisi wetu shituka na kinachoendelea katika sekta hii adhimu yenye kundi kubwa la waathilika. Pamoja na mapungufu machache yaliyokuwepo katika awamu ya tatu na nne, lakini ni Bora mara Sabini. Tuboreshe utaratibu wa Dr. Kikwete na Mhe. Mkapa bila Soni.
 
Watanzania tupunguze kulalama. Miaka sita mbolea ya ruzuku haikuwepo na bei ilifika takribani laki na ushee. Leo ruzuku ipo na wakulima wanapata mbolea kwa tshs nadhani 70, 000.

Hili nalo ni kulalama badala ya kuwa na shukrani walau kiasi. Nikuulize wewe mleta mada, serikali ya familia yako unayoiongoza wewe imeyaweza yote?
 
Watanzania tupunguze kulalama. Miaka sita mbolea ya ruzuku haikuwepo na bei ilifika takribani laki na ushee. Leo ruzuku ipo na wakulima wanapata mbolea kwa tshs nadhani 70, 000. Hili nalo ni kulalama badala ya kuwa na shukrani walau kiasi. Nikuulize wewe mleta mada, serikali ya familia yako unayoiongoza wewe imeyaweza yote?
Utaratibu wa upatikanaji ni rafiki kwa mwananchi wa Kazuramimba? Inapatikanaje? Inatosheleza mahitaji halisi ya mkulima?

Tanzania ilifika hatua ya kuuzwa mbolea vijini katika awamu ya nne, leo mbolea lazima inunuliwe makao makuu za wilaya tena kwa wakala, alafu unaenda bila kuwa na uhakika Kama utaikuta na kuipata, Daaah, badala ya kuwapunguzia watu Kero tunaongeza kerooo.

Viongo wa juu wajuwe, ukiritimba uzalisha rushwa. Usikute wanaotetea wanahamisha mbolea hiyo na kuiuza kwa mlango wa pembeni.
 
Watanzania tupunguze kulalama. Miaka sita mbolea ya ruzuku haikuwepo na bei ilifika takribani laki na ushee. Leo ruzuku ipo na wakulima wanapata mbolea kwa tshs nadhani 70, 000. Hili nalo ni kulalama badala ya kuwa na shukrani walau kiasi. Nikuulize wewe mleta mada, serikali ya familia yako unayoiongoza wewe imeyaweza yote?
Wewe upo mjini na huhusiki na kilimo.

Uliza ndugu yako aliyeko kijijini kama anaweza pata hii mbolea kirahisi.
 
Utaratibu wa upatikanaji ni rafiki kwa mwananchi wa Kazuramimba? Inapatikanaje? Inatosheleza mahitaji halisi ya mkulima?
Tanzania ilifika hatua ya kuuzwa mbolea vijini katika awamu ya nne...
Achana na huyo mropokaji hajui lolote, nyinyi ndo mnaojua adha mnazozipata.......huku kwenye majukwaa wanajinasibu kutoa maelfu ya tani ya mbolea ya ruzuku kumbe chenga tu, na nyingine ndo hiyo ilikamatwa ikivushwa kwa magendo kwenda malawi.
 
Watanzania tupunguze kulalama. Miaka sita mbolea ya ruzuku haikuwepo na bei ilifika takribani laki na ushee. Leo ruzuku ipo na wakulima wanapata mbolea kwa tshs nadhani 70, 000.

Hili nalo ni kulalama badala ya kuwa na shukrani walau kiasi. Nikuulize wewe mleta mada, serikali ya familia yako unayoiongoza wewe imeyaweza yote?
Hiyo mbolea ya ruzuku ya 70K ipo wapi!!??
 
Watanzania tupunguze kulalama. Miaka sita mbolea ya ruzuku haikuwepo na bei ilifika takribani laki na ushee. Leo ruzuku ipo na wakulima wanapata mbolea kwa tshs nadhani 70, 000.

Hili nalo ni kulalama badala ya kuwa na shukrani walau kiasi. Nikuulize wewe mleta mada, serikali ya familia yako unayoiongoza wewe imeyaweza yote?
Hivi wewe unajielewa kweli!?? acha tunaolima ndo tuongee wapumbavu na wajinga kama nynyi muwe ndugu watazamaji,kwa hiyo miaka sita unayosema mbolea bei juu sana ilikuwa 50000-55000 maeneo yangu ilikuwa ni 45000 acha kutuletea chai kwenye mambo ya msingi.
 
Bashe mzeee wa that extent ha ha msomali huyu anamvisha samia kiremba cha ukoka.

Mbole ni shida kubwa tena janga kubwa sana morogoro Kampuni ya Yara wamempa mtu mmoja tu asambaze mkoa wote huùuu haha hatari sana
 
Thread yako ingeleta maana endapo tungekuwa enzi za ujamaa, now tupo soko huria.... kwahiyo huwezi tu uka assume kwamba ni obligation ya serikali kusaidia wakulima.

Hata hizi ruzuku wanatoa serikali ni kama tu welfare na hisani.... wakulima wanatakiwa wajisaidie wenyewe.

Kwanza huyu mkulima mwenyewe mdogo akilima sana ni hekari moja, ambayo chakula anachovuna kina msaada mdogo kwenye uchumi. Kwasababu anachovuna yeye mwenyewe ndo anakitumia kama chakula, hakiwasaidii wengine
 
Hivi wewe unajielewa kweli!?? acha tunaolima ndo tuongee wapumbavu na wajinga kama nynyi muwe ndugu watazamaji,kwa hiyo miaka sita unayosema mbolea bei juu sana ilikuwa 50000-55000 maeneo yangu ilikuwa ni 45000 acha kutuletea chai kwenye mambo ya msingi.
Wewe ni mpumbavu squared. Unajiita mkulima halafu unakosa mbolea ya ruzuku wakati bibi yangu kule kijijini ndani kabisa kaipata. Umejaa negativity za kipumbavu tu. Unakurupuka leo kudai mbolea wakati imegawiwa tangu Sept huko, tena kwa kubembeleza baadhi ya sehemu. Halafu jitu kama wewe linakurupuka toka usingizini ati hakuna mbolea za ruzuku. Pumbavu mkubwa wewe. Endelea kulalama, utashiba huko kulalama kwako.
 
Watanzania tupunguze kulalama. Miaka sita mbolea ya ruzuku haikuwepo na bei ilifika takribani laki na ushee. Leo ruzuku ipo na wakulima wanapata mbolea kwa tshs nadhani 70, 000.

Hili nalo ni kulalama badala ya kuwa na shukrani walau kiasi. Nikuulize wewe mleta mada, serikali ya familia yako unayoiongoza wewe imeyaweza yote?
Sasa wewe hapo umesaidia mchango gani katika kutafuta ufumbuzi wa tatizo aliloliona mleta mada?

Badala yake unakuja na mipasho tu.

Eleza, hiyo mbolea ya ruzuku inapatikana, au ni ubabaishaji tu!
 
Thread yako ingeleta maana endapo tungekuwa enzi za ujamaa, now tupo soko huria.... kwahiyo huwezi tu uka assume kwamba ni obligation ya serikali kusaidia wakulima.

Hata hizi ruzuku wanatoa serikali ni kama tu welfare na hisani.... wakulima wanatakiwa wajisaidie wenyewe.

Kwanza huyu mkulima mwenyewe mdogo akilima sana ni hekari moja, ambayo chakula anachovuna kina msaada mdogo kwenye uchumi. Kwasababu anachovuna yeye mwenyewe ndo anakitumia kama chakula, hakiwasaidii wengine
Mawazo potofu yenye kutegemea kukariri kama kasuku mambo unayoambiwa au kusoma vitabuni bila kujua uhalisi wake ni nini; wala bila kuchukulia mazingira ya nchi husika.

Ni wapi pasipotumika ruzuku kwa njia moja au nyingine?

Unakaririshwa "soko huria" hata hujui uhalisia wake ni nini.

Huyo mkulima mdogo, mmoja mmoja hahitaji uzalishaji wa mavuno mengi wa wa mazao akitumia mbegu bora, pembejeo sahihi na kupata ushauri sahihi?

Mkulima mdogo mdogo, kwa ujumla wao kijijini, tarafani, mkoani na kitaifa unatofauti gani na huo wa mashamba makubwa binafsi?
 
Baadhi yao inapotolewa ruzuku za namna hiyo huwa ndio wamepata fursa ya kupiga pesa na kunyanyasa wakulima ! Ruzuku duniani kote hutolewa kwa kupunguzwa bei ya kitu husika kama ilivyofanywa kwenye mafuta sio kuanza kupangishana foleni na kuanza kutoa kibali cha mbolea ya ruzuku!! Ukiona Hivyo ujue hao ni wazee wa fursa wameshaamua kupiga pesa !!

Huo wimbo wa Kilimo ni uti wa mgongo wa Nchi yetu umeimbwa tangu dahari na dahari lakini watu wanafanya masihara !!

Kitu kimoja watu wajue Shibe ndio kila kitu na njaa ni hatari kwa usalama wetu sote !! Hiyo ruzuku iingie moja kwa moja kwenye bidhaa husika kama ilivyokuwa kwenye mafuta !! Wasipewe fursa wapigaji tafadhalini sana !!
 
Baadhi yao inapotolewa ruzuku za namna hiyo huwa ndio wamepata fursa ya kupiga pesa na kunyanyasa wakulima ! Ruzuku duniani kote hutolewa kwa kupunguzwa bei ya kitu husika kama ilivyofanywa kwenye mafuta sio kuanza kupangishana foleni na kuanza kutoa kibali cha mbolea ya ruzuku!! Ukiona Hivyo ujue hao ni wazee wa fursa wameshaamua kupiga pesa !! Huo wimbo wa Kilimo ni uti wa mgongo wa Nchi yetu umeimbwa tangu dahari na dahari lakini watu wanafanya masihara !! Kitu kimoja watu wajue Shibe ndio kila kitu na njaa ni hatari kwa usalama wetu sote !! Hiyo ruzuku iingie moja kwa moja kwenye bidhaa husika kama ilivyokuwa kwenye mafuta !! Wasipewe fursa wapigaji tafadhalini sana !!
Maoni kama haya hayana kazi tena maaana wakulima wameshacheleweshewa mbole hakuna na msimu wa kulima nao umeshafika je hapo nani wa kulaumiwa Bashe na jopo lake wamefeil hata aroma 1 hawajapata mkuu mbolea huku mtaaani ni kisanga sana acha wengine wanaimba mapambia ya kusifu
 
Watanzania tupunguze kulalama. Miaka sita mbolea ya ruzuku haikuwepo na bei ilifika takribani laki na ushee. Leo ruzuku ipo na wakulima wanapata mbolea kwa tshs nadhani 70, 000.

Hili nalo ni kulalama badala ya kuwa na shukrani walau kiasi. Nikuulize wewe mleta mada, serikali ya familia yako unayoiongoza wewe imeyaweza yote?
Acha umbea. Magufuri aliacha mbolea ikiwa elfu hamsini tu kwa kilo 50 yaani mfuko. Leo hii tunauziwa laki na arobaini.

Acha uchochezi
 
Back
Top Bottom