Kauvimbe kadogo juu kidogo kutoka kitovuni. Ukibonyeza kananywea!

Kauvimbe kadogo juu kidogo kutoka kitovuni. Ukibonyeza kananywea!

Dimma

Member
Joined
Aug 15, 2017
Posts
99
Reaction score
135
Habari wana JF.

Naombeni msaada wa mawazo ama tiba. Jinsia yangu ni ME, umri 30.

Sentimita moja au mbili hivi kutoka kitovuni (upande wa kuelekea juu) kuna kauvimbe kanakuwa kanatokeza na kunywea/kupotea. Nikila chakula na kushiba, kauvimbe kanatokeza. Nikikabonyeza kwa kidole kanarudi ndani (kanapotea), ila baada ya muda mfupi kanatokeza tena.

Napoenda haja kubwa, ndipo kanapotea mazima. Mpaka napokula/naposhiba tena ndipo kanachomoza tena. Hakana maumivu yoyote. Nakaribia mwaka sasa tangu nigundue.

Nimejaribu kufanya some searches google, nahisi itakuwa ni HERNIA ambayo hutokea karibu na kitovu kwa upande wa juu.

Wakuu, kweli hiyo ni hernia? Mbali na operesheni, je kuna TIBA MBADALA za ASILI kuponya tatizo hilo?

Ahsanteni.
 
wataalamu na madaktari pitieni hapa tafadhari.
 
Back
Top Bottom