Hivi punde
JF-Expert Member
- Apr 1, 2017
- 2,554
- 8,587
Wataalamu na wawezeshaji wa kituo cha kimataifa cha utawala bora cha Basel cha Uswisi wapo nchini kutoa mafunzo kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Kupitia kituo cha kimataifa cha kusaidia urejeshaji wa mali zilizopatikana kwa njia ya rushwa (ICAR), kituo hicho kinatoa mafunzo ya siku tano kwa Takukuru.
Programu ya mafunzo hayo iliyofunguliwa jana Mei 21, 2018 na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, John Mbungo itahitimishwa Mei 25, 2018.
Mafunzo hayo yanalenga masuala ya uchunguzi na uendeshaji wa kesi za makosa makubwa ya rushwa kwenye mikataba ya ujenzi wa miundombinu na ununuzi wa umma; na mbinu za rushwa na udanganyifu katika mikataba na ununuzi.
Taarifa ya Takukuru inasema mafunzo hayo yanawashirikisha maofisa wa idara zingine ikiwamo Mamlaka ya Kupambana na Rushwa Zanzibar (Zaeca); Mamlaka ya Ununuzi wa Umma (PPRA); Kitengo cha Udhibiti wa Fedha Haramu Tanzania (Fiu); Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP); na Jeshi la Polisi.
Mbungo akifungua mafunzo hayo aliwaeleza washiriki kuwa sehemu kubwa ya bajeti ya nchi huelekezwa kwenye miradi ya maendeleo ambayo utekelezaji wake katika ununuzi umegubikwa na vitendo vya rushwa na unawanufaisha wachache.
Kupitia kituo cha kimataifa cha kusaidia urejeshaji wa mali zilizopatikana kwa njia ya rushwa (ICAR), kituo hicho kinatoa mafunzo ya siku tano kwa Takukuru.
Programu ya mafunzo hayo iliyofunguliwa jana Mei 21, 2018 na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, John Mbungo itahitimishwa Mei 25, 2018.
Mafunzo hayo yanalenga masuala ya uchunguzi na uendeshaji wa kesi za makosa makubwa ya rushwa kwenye mikataba ya ujenzi wa miundombinu na ununuzi wa umma; na mbinu za rushwa na udanganyifu katika mikataba na ununuzi.
Taarifa ya Takukuru inasema mafunzo hayo yanawashirikisha maofisa wa idara zingine ikiwamo Mamlaka ya Kupambana na Rushwa Zanzibar (Zaeca); Mamlaka ya Ununuzi wa Umma (PPRA); Kitengo cha Udhibiti wa Fedha Haramu Tanzania (Fiu); Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP); na Jeshi la Polisi.
Mbungo akifungua mafunzo hayo aliwaeleza washiriki kuwa sehemu kubwa ya bajeti ya nchi huelekezwa kwenye miradi ya maendeleo ambayo utekelezaji wake katika ununuzi umegubikwa na vitendo vya rushwa na unawanufaisha wachache.