Kazi nzuri ITV, Said Mwema

Kazi nzuri ITV, Said Mwema

Invisible

JF Admin
Joined
Feb 26, 2006
Posts
16,286
Reaction score
8,380
Napenda kuwapongeza ITV kwa kazi nzuri ya kufichua rushwa inayoliwa na Polisi wa Trafiki. Aidha napenda kumpongeza Jerry Muro kwa kuwa imara na kwa namna ya kipekee alivyofanikisha kuchukua vema picha za polisi hawa wala rushwa na kuliaibisha jeshi letu na polisi wa usalama barabarani.

Pia nalipongeza Jeshi letu la Polisi kwa kuchukua hatua madhubuti baada ya kugundua kuwa kilichooneshwa na ITV ni kitu sahihi na kuwasimamisha kazi mara moja wafanyakazi 11.

Congrats, keep this good job!
 
Napenda kuwapongeza ITV kwa kazi nzuri ya kufichua rushwa inayoliwa na Polisi wa Trafiki. Aidha napenda kumpongeza Jerry Muro kwa kuwa imara na kwa namna ya kipekee alivyofanikisha kuchukua vema picha za polisi hawa wala rushwa na kuliaibisha jeshi letu na polisi wa usalama barabarani.

Pia nalipongeza Jeshi letu la Polisi kwa kuchukua hatua madhubuti baada ya kugundua kuwa kilichooneshwa na ITV ni kitu sahihi na kuwasimamisha kazi mara moja wafanyakazi 11.

Congrats, keep this good job!

weenaye bwana!

sijui ndio starehe zimekujaa au sijuinini

mimi nilifikiri ITV wametoa info jinsi JF ilivyothabiti

yaani rushwa za traf9ki zimekuwa big deal

hebu tupishe sie
 
Napenda kuwapongeza ITV kwa kazi nzuri ya kufichua rushwa inayoliwa na Polisi wa Trafiki. Aidha napenda kumpongeza Jerry Muro kwa kuwa imara na kwa namna ya kipekee alivyofanikisha kuchukua vema picha za polisi hawa wala rushwa na kuliaibisha jeshi letu na polisi wa usalama barabarani.

Pia nalipongeza Jeshi letu la Polisi kwa kuchukua hatua madhubuti baada ya kugundua kuwa kilichooneshwa na ITV ni kitu sahihi na kuwasimamisha kazi mara moja wafanyakazi 11.

Congrats, keep this good job!

Mzee tupe kwa upana zaidi kulikoni mbona habari inakosa vionjo fulani fulani hivi...
 
Mzee tupe kwa upana zaidi kulikoni mbona habari inakosa vionjo fulani fulani hivi...
Masatu,

Iko hivi, kuna kipindi kilirushwa na Jerry Muro wa ITV, wengi walidai ni risk kwake kwakuwa amewagusa polisi.

Aliitwa leo (nikapata taarifa toka kwa member mmoja wa JF) na kuwapelekea mkanda wa kipindi kilichorushwa na kituo chao, wakawatambua askari hao na kuwachukulia hatua haraka iwezekanavyo, mkanda huo umetolewa nakala na kusambazwa nchini kote.

GT,

you-are-too-funny-ag1.gif
 
weenaye bwana!

sijui ndio starehe zimekujaa au sijuinini

mimi nilifikiri ITV wametoa info jinsi JF ilivyothabiti

yaani rushwa za traf9ki zimekuwa big deal

hebu tupishe sie

Babangu,

hee-hee-hee-ag1.gif


Hawa jamaa wamekuwa kero sana, najua kama umefika Bongo siku si nyingi basi kama ulikuwa na safari ya kwenda mikoani tokea Dar yatakuwa yamekukuta ya kusimamishwa kila sehemu na kuliwa walau 20,000 kwa makosa usiyoelewa elewa na ukiwanyima basi utacheleweshwa hadi ukasirike kabisa!

Jeshi letu likiwa safi basi linaweza kupambana na wachafu wengine!
 
weenaye bwana!

sijui ndio starehe zimekujaa au sijuinini

mimi nilifikiri ITV wametoa info jinsi JF ilivyothabiti

yaani rushwa za traf9ki zimekuwa big deal

hebu tupishe sie

Hahahaha, Kwa jinsi nilivyofuatilia post za GT,kwa kweli ninaingiwa na wasi wasi kama huyu ndiye yule yule GT mwenye hoja nzito zinazojenga na kuamsha waliolala, sitaki kuamini kama ndiye huyu ameamua kuwa mpinga watu hapa JF, sitaki kuamini pia kama anaweza akawa amenunuliwa na mafisadi kama alivyonunuliwa MTIKILA, Ninachotaka kukiamini ni kuwa GT ameamua kufurahisha baraza kwa muda mfupi then atarudi kwenye mstari wa comments zinazojenga na kutetea maslahi ya taifa hili la WATANZANIA.
 
Its about time somebody did something, arusha - moshi wanatutesa kama nini. Fire extinguisher, licence, kadi ya gari. Kama unavyo, oh nina njaa sijanywa soda, so? Na sio kwamba i drive a bonite truck, its a starlet, tena two door jamani. The other day someone was simamishwad eti, wewe mbona mdogo hivyo? eeh? na they had a legal licence, eeeh! eh!
 
Its about time somebody did something, arusha - moshi wanatutesa kama nini. Fire extinguisher, licence, kadi ya gari. Kama unavyo, oh nina njaa sijanywa soda, so? Na sio kwamba i drive a bonite truck, its a starlet, tena two door jamani. The other day someone was simamishwad eti, wewe mbona mdogo hivyo? eeh? na they had a legal licence, eeeh! eh!
waga,

GT hajatumwa, na kama katumwa basi katumwa na wananchi. Kutofautiana mitizamo ni jambo zuri sana katika mijadala kama hii.

Nkamangi,

Hapa umeniua kabisa!
 
Waanandugu hakika kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho...
Waheshimiwa sana wale wakina trafiki naona sasa wameanza kuwa makini hata kwenye kupokea na jinsi ya kupokea rushwa....
Hivi majuzi itv imeanza kuwaonyesha wahuni na wahujumu uchumi live .......nafiikiri hii inabidi iende maofisini pia tuonyeshwe na risiti zao jamani.......na jinsi wanavyopekea pesa za rushwa .........
Hata kama kila mtu anakula kwa ofisin kwake ila watakuwa wanakula na kwa adabu!!!!!
 
Kombe asema watashugulikiwa vilivyo na hakuna atakaebaki!!!!!mwema asema apongeza itv na kusema safari imeanza.....nimecheka sana wakati
safari imeanza toka siku nyingi.....kuanzia ubungo pale mpaka mwenge..urudi posta........,
 
Trafiki 11 wasimamishwa kwa rushwa
Halima Mlacha
Daily News; Saturday,October 04, 2008 @00:02

Askari 11 wa Usalama Barabarani wa mikoa ya Iringa, Morogoro na Pwani wameondolewa kwenye vitengo vyao vya kazi baada ya kuonyeshwa kwenye televisheni wakipokea rushwa, imeelezwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Mkuu wa Polisi, Inspekta Jenerali Said Mwema, alisema kufuatia tukio hilo, amewaagiza makamanda wa Polisi wa mikoa kuwachukulia pia hatua za nidhamu zinazostahili.

Alisema askari hao 11 walioonekana kwenye mkanda wa uchunguzi uliofanywa na kituo cha televisheni cha ITV, watahojiwa na kuchunguzwa na ikithibitika kuhusika watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria na kanuni za Polisi.

"Kipindi kile nilikiona na kimenifurahisha sana, nachukua fursa hii kuvipongeza vyombo vya habari kwa kutuunga mkono katika vita dhidi ya rushwa hasa kipindi maalumu kilichorushwa na ITV kwa kweli kimetufundisha," alisema Mwema.

Alisema lengo la Polisi ni kujidhihirisha katika jamii ya Watanzania kwa kuwa na utumishi ulio bora, hivyo imejipanga kutafuta miundombinu ya kisasa katika kuongeza ufanisi katika utendaji wake badala ya kutumia askari zaidi ya 1,000 barabarani.

"Tutashirikiana na Wizara za Miundombinu na Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kuhakikisha kuwa tunakuwa na mfumo na miundombinu ya kisasa, ili makosa ya barabarani, ajali na uvunjifu wowote wa sheria uonekane kwa urahisi kupitia kamera za CCTV," alisema.

Pamoja na hayo, Mwema alisema katika tathmini ya hali ya uhalifu ya kipindi cha robo ya pili ya mwaka huu, imeonyesha upungufu wa matukio ya uhalifu kutokana na sababu mbalimbali lakini kubwa zaidi ni kuimarika kwa ushirikiano kati ya wananchi na Polisi, (Polisi Jamii).

Hata hivyo alisema chombo hicho bado kinakabiliwa na wakati mgumu hasa katika miezi ya Oktoba, Novemba na Desemba ambako matukio ya uhalifu hujitokeza kwa kiwango cha juu kama vile mauaji na unyang'anyi wa kutumia silaha hali ambayo hata hivyo Polisi imejipanga kukabiliana nayo
 
Gerry nipigie no hii tuma kwanza msg
ndio napokea,....ntkupa list ya hao vifisadi hapa dar
then ntakupa mcongomwingine wa kutoka nao live kaka!!!!ila siku ziendavyo kumbuka kuwamaliza na wa maofisini hasa halmashauri za kinondoni na ilala na temeke rushwa njenje....tender wanapewa wenye hela zao tu rushwa kwanza ..ukitaka hiki pesa kwanza
 
tatizo, ni pale AGP alipoamua kuwahamisha vituo, badala ya kuwasimamisha kwa uchunguzi kamili.
 
haaaaaaa,hhaaaa

Duh imetulia Hiyio yan hao mabibiarusi wa Moshi hawako serious wanafananisha starlet na truck la coke mmmbut may be starlet yako ilikuwa red in colour.......

LOL
 
Ingetokea kwa wenzetu weupe tungesikia yafuatayo;-
IGP kajiuzuru-kwa kutosimamia maadili.
Waziri mhusika na maswala ya Polisi kajiuzuru.
Na wengine wengi wangejiuzuru...maana ni aibu sana kwa jeshi la polisi tena mno rushwa LIVE kama wanaigiza vile kumbe ni true story dah...!
 
Good lookin out fidel. If I knew you in person…I would take you to the strip and lap dances would be on me brotha…lol…
 
Kipindi cha ITV kuhusu ripoti barabaran kilichorushwa kwa ustadi mkubwa kimeweka mambo wazi na SAIDI Mwema amakubali kwamba matrafiki wanakula rushwa kwa kwenda mbele utafikiri kiama imefika. Serikali sasa inaweza kuchukua mbinu hiyo kuwanasa maaskari wengine wala rushwa. Maaskari walionyeshwa wakipokea rushwa wanaweza kufukuzwa kazi, je wale waliotoa rushwa watachukuliwa hatua gani? Na Je Jerry Muro aliyerekodi maovu hayo kwa ugunduzi huo na kazi nzuri atapewa zawadi gani?
 
Waanandugu hakika kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho...
Waheshimiwa sana wale wakina trafiki naona sasa wameanza kuwa makini hata kwenye kupokea na jinsi ya kupokea rushwa....
Hivi majuzi itv imeanza kuwaonyesha wahuni na wahujumu uchumi live .......nafiikiri hii inabidi iende maofisini pia tuonyeshwe na risiti zao jamani.......na jinsi wanavyopekea pesa za rushwa .........
Hata kama kila mtu anakula kwa ofisin kwake ila watakuwa wanakula na kwa adabu!!!!
!

Mama hundred,
wajua mara nyingi sana tumepiga kelele kwenye forum na mitaani kuhusu traffic.Mie mara mbili niliwahi kueleza kuhusu rushwa ya traffic polisi ubungo.

Taarifa iliyotolewa na ITV ukweli kwa uwazi zaidi.Tatizo halianzii kwa Traffic bali kwa mwajiri wao has kitengo cha traffic.Kuna maeneo sugu kwa rushwa barabarani na wananchi wamekuwa wanatoa taarifa hata kupitia tovuti ya jeshi la polisi/Tatizo hatua hazichukuliwi hata kidogo.Imekuwa mazoea na zaisi sana baadhi ya wakubwa wanakula na traffic haohao.Traffic anapandwa eneo moja mwaka mzima kwa kuwa mkubwa wake anakatiwa % kila siku kutokana na rushwa.

Hakuna cha risiti wala nini hiyo ni rushwa kavu kavu.Ndiyo Tanzania tuliyoahidiwa 2005.Kila mtu anakula kwa urefu wa kamba yake ati
 
Back
Top Bottom