Kenya: Kesi ya uchaguzi wa urais Mahakama ya Juu kutoa uamuzi leo

Kenya: Kesi ya uchaguzi wa urais Mahakama ya Juu kutoa uamuzi leo

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
4cf2dcf70c4de16ccc57981dffe0a8a5.jpg
Wakenya leo Novemba 20 wanasubiri mwelekeo ambao nchi itachukua ambapo Mahakama ya Juu itatoa uamuzi katika kesi za kupinga uchaguzi wa marudio wa Oktoba 26 ambao Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi na kususiwa na upinzani.

Kiongozi wa upinzani Raila Odinga ambaye alirejea nchini Ijumaa kutoka ziara ya siku kumi Amerika, amesema atatangazia wafuasi wake hatua atakazochukua Juma hili.

Japo Bw Odinga alikataa kutaja mwelekeo atauchukua hadi majaji wa Mahakama ya Juu watoe uamuzi wao Jumatatu, aliashiria kwamba upinzani utaendelea kukabiliana na serikali.

"Safari ya ukombozi wa tatu imeanza rasmi leo", Bw Odinga aliwaambia wafuasi wake Ijumaa ambapo watu zaidi ya watano waliuawa na mali kuharibiwa wakati Polisi walipokabiliana na wafuasi waliofurika katika barabara za Nairobi kumkaribisha Odinga.

Ikiwa mahakama itatupilia mbali kesi zilizowasilishwa na aliyekuwa mbunge wa Kikome John Harun Mwau na Wanaharakati Njonjo Mue na Khelef Khalifa, Rais Mteule Uhuru Kenyatta na Naibu wake William Ruto wataapishwa kwa kipindi cha pili baadaye mwezi huu.

Updates;

Mahakama ya Juu ya Kenya yatupilia mbali kesi zilizowasilishwa kupinga uchaguzi wa marudio, imeidhinishwa ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta

Jaji Mkuu David Maraga amesema majaji kwa kauli moja wameamua kwamba kesi zote mbili hazina msingi.
 
Ni kweli mkuu
Mkuu tusubiri yatakayojiri. Wanaweza kuamua sasa basi masuala ya uchaguzi, wakenya wengi wao wamechoka hivyo wanahitaji kusonge mbele.
 
Jubilee wameshashinda sasa
Wanasubir tu kumuapisha uhuru
 
kufutafuta wameona wanaweza kuingiza nchi matatani hivyo wataamua kwa kusema bora liende tu
Hapo ndipo hatari zaidi ukipindisha sheria kwa kusema bora liende unaweza kulipasua taifa
 
Tayar mahakama impa ushindi
Uhuru Sasa n kuapishwa kumebak
 
Hapo ndipo hatari zaidi ukipindisha sheria kwa kusema bora liende unaweza kulipasua taifa
Bora liende imekuwa, mahakama imetupilia mbali wamesema kesi zote hazina msingi wowote ule
 
Wakenya wakitoa maoni yao baada ya mahakama kutupilia mbali kesi zilizofunguliwa kupinga ushindi wa Rais Kenyatta.
 
Back
Top Bottom