Kenya miongoni mwa nchi 20 zenye watu wakarimu zaidi duniani

Kenya miongoni mwa nchi 20 zenye watu wakarimu zaidi duniani

Tunzo

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2013
Posts
4,082
Reaction score
2,402
Kenya imeorodheshwa miongoni mwa nchi 20 zenye watu wakarimu zaidi duniani. Kenya inashikilia nafasi ya 12 kwenye orodha ya takwimu za mwaka 2015 ambayo inaongozwa na Myanmar ambayo zamani ilifahamika kama Burma.

Myanmar ilishikilia nafasi hiyo pia mwaka 2015 na kwa pamoja na Marekani mwaka 2014. Tanzania imeorodheshwa ya 57 na Uganda ya 26.

Orodha hiyo ilizingatia uwezekano wa watu kuwasaidia wageni, watu kutoa pesa za kusaidia wengine na watu kujitolea muda wao kuwasaidia wengine.
Kwenye orodha hiyo, ambayo hutayarishwa na shirika la Charities Aid Foundation, nchi ambazo raia wake waliwasaidia wageni kwa urahisi ni nchi ambazo zinakabiliwa na mizozo ya kivita.

Somalia ni ya nne kwenye orodha ya watu wanaojitolea kushiriki katika wasaidia wengine sana duniani. Orodha hiyo inaongozwa na Iraq, ikifuatwa
na Libya, na nambari tatu Kuwait. Malawi ni ya sita kwenye orodha hiyo na Botswana ya saba. Shirika hilo liliwahoji watu takriban 1,000 kutoka kila moja ya nchi 140 zilizoangaziwa.


Chanzo: BBC Swahili.
 
Wangesema nchi inayoongoza kwa vichaa hapo angalao na sisi tungeongoza
 
Orodha ya jumla ya nchi kwa
ukarimu mwaka 2015
Taifa Nambari
Myanmar 1
Marekani 2
Australia 3
New Zealand 4
Sri Lanka 5
Canada 6
Indonesia 7
Uingereza 8
Ireland 9
Umoja wa Milki za Kiarabu 10
Uzbekistan 11
Kenya 12
Uholanzi 13
Norway 14
Turkmenistan 15
Malta 16
Iceland 17
Bhutan 18
Kuwait 19
Denmark 20
Ujerumani 21
Malaysia 22
Switzerland 23
Finland 24
Sweden 25
Uganda 26
Mongolia 27
Singapore 28
Guatemala 29
Austria 30
Iraq 31
Ubelgiji 32
Panama 33
Kyrgyzstan 34
Cyprus 35
Jamhuri ya Dominika 36
Thailand 37
Malawi 38
Nepal 39
Slovenia 40
Saudi Arabia 41
Cyprus Kaskazini 42
Israel 43
Libya 44
Iran 45
Sierra Leone 46
Ufilipino 47
Sudan Kusini 48
Luxembourg 49
Taiwan 50
Cameroon 51
Liberia 52
Haiti 53
Botswana 54
Chile 55
Nigeria 56
Tanzania 57
Somalia 58
Uruguay 58
Kosovo 60
Afrika Kusini 61
Costa Rica 62
Zambia 63
Vietnam 64
Peru 65
Syria 66
Msumbiji 67
Brazil 68
Guinea 69
Bolivia 70
Jordan 71
Burkina Faso 72
Colombia 73
Honduras 74
Korea Kusini 75
Nicaragua 76
Ghana 77
Afghanistan 78
Spain 79
Lebanon 80
France 81
Italy 82
Argentina 83
Ethiopia 84
Congo 85
El Salvador 85
Tajikistan 87
Mauritania 88
Gabon 89
Portugal 90
India 91
Pakistan 92
Romania 93
Senegal 95
Kazakhstan 96
Ecuador 97
Cambodia 98
Mali 99
Belarus 100
Paraguay 101
Benin 102
Togo 103
Cote d'Ivoire 104
Albania 105
Ukraine 106
Mexico 107
Zimbabwe 108
Poland 109
Moldova 110
Chad 111
Misri 112
Latvia 113
Japan 114
Niger 115
Rwanda 116
Venezuela 117
Estonia 118
Macedonia 119
Georgia 120
Jamhuri ya Czech 121
Tunisia 122
Morocco 123
Lithuania 124
Slovakia 124
Urusi 126
Croatia 127
Bosnia na Herzegovina 128
Bulgaria 129
Armenia 130
Azerbaijan 131
Madagascar 132
Montenegro 133
Hungary 134
Serbia 135
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 136
Ugiriki 137
Yemen 138
Maeneo ya Palestina 139
China 140
 
Hizi takwimu za Kibangi bangi kweli.
Wewe owa Mke wa kikenya ndio utajua,kama hujachimbiwa kaburi kabla hujafa.

Ukarimu gani walionao Wamarekani hapo Wakati wanabagua wenzao weusi na kuuwana kila siku.
Kuna ukarimu wa kutoka Moyoni na kuna Unafiki wa Ukarimu kama Mmarekani
 
wonders shall never end!
wana ukarimu kwa wazungu ila kupendana wenyewe kwa wenyewe wameshindwa..ukabila unawatafuna.
 
Marekani nafasi ya 2 huku wenye rangi nyeusi kwao sio wenzao!!! Kenya nafasi 12 !!!!! Ukarimu ni nini!? ...India 91 China 140 mara mia bora China kuliko India....
 
mnajuionyesha wenyewe vile hamna ukarimu kwa haya majibu yenu... haya ona vile mnachuki kwa watu ambao hamjakutana nao uso kwa uso.... haya endeleeni tuwaone
 
Marekani nafasi ya 2 mmh labda mimi siishi dunia hii..!
 
mnajuionyesha wenyewe vile hamna ukarimu kwa haya majibu yenu... haya ona vile mnachuki kwa watu ambao hamjakutana nao uso kwa uso.... haya endeleeni tuwaone
hawapendi hii habari, wanapitia kwa hasira. wanafiki watapatikana tu.
 
Kenyaa ???

Kwani Twaweza wameruhusiwa kufanya utafiti huu ?

MO11 Watanzania wa hapo awali enzi za ustaarabu mngekua na namba nzuri, lakini sio hawa wa leo full majungu na chuki na visasi. Mumekua na chuki sijui kisa nini, halafu hata ubaguzi umewaingia.

Juzi kwenu tetemeko la ardhi Kagera linaibua mijadala ya kila aina, imebidi hadi jeshi letu la KDF lije kutoa misaada, nyie humo ndani ni kuvurugana tu. Mnawakamata wapinzani kisa wamekwenda kutoa misaada. Sasa mbona msiorodheshwe kwenye nchi zisizo na ukarimu.

Kenya ya leo tuna wageni wanaoishi huku, tumewapokea kwa ukarimu sana. Hata Watanzania wanaosihi huku wanahisi wapo nyumbani, wengine hata wamewekeza na kujenga nyumba za kupangisha. Kwenu hapo mtu akifahamika mgeni, mnaanza chuki na majungu kimya kimya.

Watanzania wapo hata omba omba hapa Kenya ambao tunawasaidia barabarani kila siku.
 
Sisi Tanzania tutaongoza kwa lipi mungu Wangu
 
Back
Top Bottom