Kenya na India Zaipiku Tanzania Kwa Mauzo ya Tanzanite

jnuswe

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2010
Posts
1,270
Reaction score
549
Hii habari ni mbaya sana kwetu Watanzania, lakini pia ni fundisho kwetu tujisahihishe kujua ni wapi tunapokosea katika mikakati ya kukuza uchumi wetu. India imeweza kuuza Tanzanite yenye thamani ya Dola million 300 Kenya million 100 na Tanzania million 38.

Inakuwaje madini ambayo yanapatikana Tanzania pekee duniani hizo nchi zinatupiku ? Inaumiza sana kusikia mambo kama haya.
Chanzo:Mwananchi
 
hua mabroker wanapeleka nairobi kuuza kwa bei nzuri na wakenya wanapeleka india
 

nimeona hii taarifa roho ikaniuma sana inasemekana kenya kuna stock kubwa sana ya tanzanite na ndio moja ya thamani inayoipandisha kiuchumi kila kukicha kenya
 
Hivi Serikali ipo wapi? ndiyo maana Kagame anamdharau jamaa? ushauri aliyowahi kuutoa mama kilango hadi leo haujawahi kutekelezwa, sijui jamani,
 
Ccm oyeeeh!Waache waongoze tu kama le profeseli hajui kwa nini nchi yake ni masikini ulitegemea nini???Mbona hata mlima kilimanjaro wazungu wana jua upo kenya!
 
hawa ndio wafanya biashara wakubwa wa tanzanite mleta mada ni mkweli
 
Hivi Serikali ipo wapi? ndiyo maana Kagame anamdharau jamaa? ushauri aliyowahi kuutoa mama kilango hadi leo haujawahi kutekelezwa, sijui jamani,

Usianze kulaumu bila ktafakari.tatizo la tanzania kuwa na wanasiasa wababaishaji.nasema hili watoroshaji wakubwa wa madini yetu sio tanzanite pekee hata dhahabu ruby nk ni wachimbaji wadogowadogo ambao kwa bahati mbaya wanatetewa sana na wanasiasa.ili hali inajulikana udhibiti wao ni mgumu sana.katika kujua mapatao yao na control ya mauzo ikiwa pamoja na ulipaji kodi.
 
Misingi ya nchi ni mibovu saa yoyote goma linadondoka
 
Asilimia 80 ya madini aina ya Tanzanite yanayozalishwa nchini Tanzania, yanatoroshwa nje ya nchi na wafanyabiashara wasio waaminifu, huku nchi ikiambulia asilimia 20 tu ya madini hayo yanayozalishwa eneo la Mererani mkoani Manyara.

Kamishna wa Madini kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Paul Masanja, amesema hayo wakati wa maonyesho ya kimataifa ya Vito, yanayofanyika jijini Arusha na kukutanisha washiriki zaidi ya 500, huku kampuni 69 zikishiriki maonyesho hayo.

Masanja ametoa mfano wa mwaka 2013 ambapo Tanzania ilipata mapato yanayofikia dola za Marekani milioni 38 kutokana na Tanzanite, wakati Kenya walipokea Tanzanite yenye thamani ya dola milioni 100, huku India ikipata dola milioni 300 za madini hayo.

Amesema kuwa kutokana na hali hiyo, serikali imeamua kujenga jengo la kuuzia madini hayo na litakapokamilika hakuna mfanyabiashara atakayeruhusiwa kuuza madini hayo nje ya jengo hilo kama ilivyo sasa.
 
Dah kiukweli wafanya haraka na wadhibiti
 
Viongozi wetu kwa kufungua vinywa vyao hawajambo lakini utekelezaji 0.000
 
Naona kitu muhimu kwa Tanzania ni kuweka sheria zitakazotumika...commissions zitakazo chunguza na kutoa mwelekeo mzuri wa kufwatwa..kenya iko na commission ya minerals iliyotoa jinsi ya kupata mapato kutokana na madini na jinsi ya kugawana baina ya serikali, makampuni na wananchi
 
Hii ndo Tanzania katika muendelezo wake wa maajabu yake duniani Kenya, India zaipiku Tanzania mauzo ya tanzanite.


Chanzo:Mwananchi
 

Hiyo biashara haifanywi na serikali inafanywa na watu binafsi.Bei nzuri ziko kenya na India.Wanunuzi wa Tanzania na nyie si mtoe bei nzuri kwa wachimbaji wadogo kama wenzenu wakenya na wahindi wa india?
Wakenya na wahindi wananunua kwa bei kubwa kuliko watanzania na kuuza india na marekani.

Namsifu Muhongo aliposema watanzania wana mitaji ya kuuza juice na maji tu gesi na madini hawawezi.Hivi wafanyabiashara watanzania hawajui soko bora liko marekani na india? Nunueni kwa bei kubwa watanzania watawauzia halafu kauzeni huko ulaya na marekani na india mtajirike
Kila kitu mnalaumu siasa na Chama hivi hao wakenya hizo Tanzanite huwa wananunuliwa na chama cha KANU,CORD AU ODM?
 
Kama ningekua mmoja Wa viongozi swala la madini ya Tanzanite lingenifanya nione aibu ninapokutana na viongozi Wa nchi jirani. Mambo haya japo viongozi ni Wa kuyafuatilia na kuhakikisha faida kwa nchi ,inafedhehesha kila mtanzania ukiyasikia. Wakenya wazalendo sana kwa nchi yao ,yaani ata tanzanite za kuiba zinaipatia Kenya dola milioni 100 ,na India dola milioni 300,wakati Tanzania dola milioni 38; na tanzanite ndio yenye thamani kuliko dhahabu na almasi,na kupatikana Tanzania tu,dah! Tanzanite yenye uzito wa chini ya kilo ina thamani ya dola milioni moja. Ukweli viongozi wajivishe uzalendo,aibu ikifichwa ndani itaanza kuja tokea nje. Tumekataa kuhusika meno ya Tembo kwa ndege ya raisi Wa China,bado linatupiwa hili la kuachilia tanzanite,yaani watu wanakula huku wanatucheka ,lol ,kweli mungu atusaidie.
Serikali kudhibiti utoroshwaji wa madini nje ya nchi

http://issamichuzi.blogspot.com/2014/11/serikali-kudhibiti-utoroshwaji-wa.html
 

Hata kama ni wachimbaji wadogo, mbona hao wakubwa wanasomba udongo ,wanasamehewa kodi, na wanachangia 3% , bado si jawabu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…