Kenya na Tanzania sasa zimefika pabaya. Nani anatia ngumu? Leo madereva 51 kati ya 53 waliokutwa na Corona mpakani na Kenya ni watanzania!

Kenya na Tanzania sasa zimefika pabaya. Nani anatia ngumu? Leo madereva 51 kati ya 53 waliokutwa na Corona mpakani na Kenya ni watanzania!

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Hizi nchi kwa huu utawala hazitakuwa na mwisho mzuri. Ukiona hadi Raila analalamika basi shida ni lazima ipo kwa Rais wetu. Tumwambie ukweli.

Kwa takwimu hizi za madereva 51 kati 53 waliokutwa na Corona kwenye mpaka kati ya Kenya na Tanzania kuwa watanzania basi ni lazima jambo lifanyike. Na pia haiwezekani mipaka yote tuwe ni sisi tu! Lazima sisi ndiyo chanzo cha matatizo! Tukiendelea hivi tuna mwisho mbaya. Tusiendelee kamwe kujidanganya aslani.

Ma RC wanafunga mipaka bila kutoa muda, kila RC anajitamkia lake. Wakati Shigela akisema anafunga mpaka kwa kuwa Kenya wanaleta Corona Tanzania, yeye mama Anna Munghwira kule Kilimanjaro anasema ni kutokana na Kenya kutokuwa fair kibiashara kwa Tanzania. Tuchukue kipi?

Tuache siasa mfu. Wakuambiwa ukweli aelezwe ukweli. Haiwezekani nchi zote za mpakani zione tatizo kwa Tanzania. Tuache kujikomba kwa Rais tumueleze ukweli kuwa aina yake ya siasa ni ya hatari kwa ustawi wa nchi.

Na tangia lina ma RC wakatangaza kufunga mipaka?

Eti Corona imeisha Tanzania. Ni upuuzi kuamini hivyo!
 
Jana kasema anashangaa madereva wanaambiwa wana corona wakat wamesafiri km kibao hawajaanguka!
Hahahaha ndio Rais wetu huyu Tuliopewa na Mungu!aisee 2015 tulibugi sanaa.Yani kimeo haswaa
Ungemuuliza wanaposema madereva wanasafirisha UKIMWI kutoka Mbambabei hadi Kashozi au Kishansa hadi Dar es Salaam wanabebwa kwenye machela, huwa wanaendesha magari na nguvu zao!
 
Katika uendeshaji wa biashara za kimataifa, vitu muhimu viwili vya kuzingatia ndani ya kila taifa husika ni "comparative & competitive advantages". Hizi ni "economic phenomena" ambazo zinapaswa kuangaliwa ktk jicho la kiuchumi zaidi na wala si kisiasa.

Kwa hiyo basi kila nchi inaihitaji nyingine kind biashara. Hata kama kuna hili janga jipya la kidunia, mataifa yanapaswa kudumisha mahusiano mazuri ya kibiashara. Ndiyo maana lipo shirika la afya la Umoja wa Mataifa, yaani WHO ambalo lina "harmonized procedures" za kukabiliana nalo.

Ni vyema mataifa yote yenye kufanya biashara pamoja, yakazingatia kwa pamoja usalama na afya za wadau wote waliopo ktk ""value chain"" pindi waingiapo kutoka taifa moja kwenda ktk taifa lingine. Ni lazima tuthamini hatua zinazochukuliwa na mataifa, hasa kwa kuzingatia kuwa wanafanya hivyo kwa ajili ya kuzui maambukizi mapya kutokana na vigezo vyote muhimu vinavyozingatiwa kimataifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Moja ya faida kubwa ya hili balaa la Corona ni kuwatambua Wasaliti wa Taifa letu

Wapumbavu wapo against Taifa lao kwenye kila kitu ili tu kumkomoa Rais na Serikali

Kenyata alidhani JPM ni kama JK!

JPM ukiweka Ugoko anakuwekea gongo, ukimwaga Ugali yeye sio tu anamwaga Mboga bali hata Jiko analiloweka kwenye Pipa la Maji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Punde si punde madereva wa malori wataadimika aisee na mishahara yao itakua juu
 
Moja ya faida kubwa ya hili balaa la Corona ni kuwatambua Wasaliti wa Taifa letu

Wapumbavu wapo against Taifa lao kwenye kila kitu ili tu kumkomoa Rais na Serikali

Kenyata alidhani JPM ni kama JK!

JPM ukiweka Ugoko anakuwekea gongo, ukimwaga Ugali yeye sio tu anamwaga Mboga bali hata Jiko analiloweka kwenye Pipa la Maji

Sent using Jamii Forums mobile app
Pamoja na changamoto zetu kwenye Corona ,Rais Kenyata na serikali yake wameonyesha ni jinsi gani walivyo na roho ya kishetani...
Kwa kinachoendelea ni wazi kuwa ni vita ya kibiashara na si Corona tena...
Katika hili afe kipa afe beki hawa mafala bora uhusiano uvunjike tu ni wabinafsi sana...ninasema hivi kwa kuwa tabia zao zinajulikana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom