Kenya: Runinga za NTV na KTN News zarudi hewani huku Citizen ikiendelea kuzimwa

Kenya: Runinga za NTV na KTN News zarudi hewani huku Citizen ikiendelea kuzimwa

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
9f803b580d587037f610368ae88878bf.jpg
Vituo viwili vya televisheni vilivyokuwa vimefungiwa kwa siku saba na Serikali ya Kenya kuhusiana na kurusha matangazo ya kujiapisha kwa kiongozi wa upinzani Raila Odinga, vimeanza kurusha tena matangazo.

Lakini kituo cha tatu cha Citizen kimeendelea kufungiwa.

Kituo cha NTV kimetangaza kupitia ukurasa wake wa Twitter kuwa kimerejesha matangazo kwenye channel zake za kulipiwa, huku KTN News nayo ikirejesha chaneli zake za bure.

Kituo cha Citizen kimeendelea kutokuwa hewani. Vituo hivyo vitatu vilifungiwa baada ya kujaribu kurusha mubashara, hafla ya kujiapisha kwa kiongozi wa Muungano wa Upinzani NASA, Raila Odinga siku ya Jumanne, kama Rais wa wananchi.
 
Cha mkufu mwanafu ha, na akila? ......., na washike adabu zao! Wakirudia huo 'usangwenya' wao tena, hiyo siku nyingine ndo watazimiwa kabisa.
 
Safi. Ikiwezekana walipwe fidia juu ya hasara ya kutopeperusha matangazo yao
 
Back
Top Bottom