Kenya: Serikali yamfukuza Raia wa Ufaransa kwa kuficha mafuta

Kenya: Serikali yamfukuza Raia wa Ufaransa kwa kuficha mafuta

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
6da97b06-50de-4a08-beb5-23e0c43a17b6.jpg
Mmalaka Nchini Kenya imesitisha kibali cha kuendelea kuishi Nchini humo mmoja wa wauzaji wakubwa wa mafuta raia wa Ufaransa kutokana na sakata la uhaba wa mafuta linaloendelea.

Mfaransa huyo ni Christian Bergeron ambaye ni Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Rubis Energy Kenya ambayo ni kampuni tanzu ya Rubis Group yenye makao makuu Ufaransa.

Mdhibiti wa Nishati, Jumanne ya Aprili 12 aliwashutumu baadhi ya wauzaji wa mafuta kwa kuficha nishati hiyo katika soko la ndani kisha kuuza kwenye masoko ya nchi za nje.

Alisema kampuni hizo zitaadhibiwa kwa kuzuia ujazo wa mafuta wanayoruhusiwa kuingiza Kenya kwa miezi mitatu ijayo.

Makampuni ya Kenya yanauza 65% ya mafuta wanayoingiza kwenye soko la ndani kisha mengine wanasambaza katika Nchi Jirani zikiwemo Uganda, Rwanda na Democratic Republic of Congo.

Kumekuwa na tatizo la uhaba wa mafuta katika wiki za hivi karibuni hali ambayo imesababisha kuwe na foleni nyingi kwenye vituo vya mafuta.

Source: BBC
 
Back
Top Bottom