Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Kampeni za uchaguzi Kenya zimemalizika rasmi jana lakini wataalamu wa siasa wanahofia juu ya hatari kutokana na taarifa potofu zinazochapishwa mitandaoni na wafuasi wa wagombea wakuu.
Benedict Manzin mchambuzi wa siasa za Afrika, kusini mwa Jangwa la Sahara amesema wafuasi wa Naibu Rais, William Ruto na wale wa Raila Odinga wanasambaza taarifa mitandaoni zinazodai kuwa wapinzani wao wanajihusisha na "njama za wizi wa kura".
Mashirika ya kiraia nchini Kenya na shirika la uangalizi yameonya kwamba taarifa hizo potofu zinahatarisha demokrasia na yameyataka majukwaa ya mitandao ya kijamii kuchukua hatua.
Serikali ya Kenya pia imeanzisha kitengo maalum cha kushughulikia makosa ya uchaguzi na matamshi ya chuki.
Benedict Manzin mchambuzi wa siasa za Afrika, kusini mwa Jangwa la Sahara amesema wafuasi wa Naibu Rais, William Ruto na wale wa Raila Odinga wanasambaza taarifa mitandaoni zinazodai kuwa wapinzani wao wanajihusisha na "njama za wizi wa kura".
Mashirika ya kiraia nchini Kenya na shirika la uangalizi yameonya kwamba taarifa hizo potofu zinahatarisha demokrasia na yameyataka majukwaa ya mitandao ya kijamii kuchukua hatua.
Serikali ya Kenya pia imeanzisha kitengo maalum cha kushughulikia makosa ya uchaguzi na matamshi ya chuki.