Kenya: Wahadhiri, madaktari bingwa na wafanyakazi wagoma

Kenya: Wahadhiri, madaktari bingwa na wafanyakazi wagoma

Donatila

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,772
Reaction score
22,598
Masomo katika vyuo vikuu vya serikali na vyuo vya udaktari yalisimama Alhamisi baada ya wahadhiri na wafanyakazi wa vyuo hivyo na madaktari bingwa kugoma wakidai marekebisho ya muundo wa mishahara.

Vyanzo vya habari nchini Kenya vimeripoti kuwa wanachama wa umoja wa wahadhiri vyuo vikuu (Uasu), Umoja wa wafanyakazi wa vyuo vikuu Kenya (Kusu), Kudheiha na Umoja wa Wataalamu wa Afya na madaktari wa meno (KMPDU) wameapa kutorejea kazini mpaka pale serikali itakapokubaliana kuonyesha pendekezo lake kujibu pendekezo lao la muundo wa mishahara walilolitoa 2017-2021.

Kwa mujibu wa gazeti la The Nation waandamanaji hao vinginevyo, wanataka muajiri wao aheshimu na kutekeleza pendekezo lao kama lilivyotolewa.

Katibu mkuu wa Uasu Constantine Wasonga amesema walikuwa hawajapinga agizo la Waziri wa Fedha Ukur Yattani la kutoa fursa ya kuwepo mazungumzo kufikia suluhu.

“Sisi hatujawahi kukataa kukutana na msuluhishi, badala yake anatakiwa kuyafahamisha mabaraza ya vyuo na serikali kupeleka mapendekezo yao, lakini sisi mgomo wetu unaanza rasmi leo ,” aliwaambia waandishi wa habari


Chanzo: voaswahili
 
Back
Top Bottom