Kenya washituka, wapinga vikali mkataba wa DP World

Kenya washituka, wapinga vikali mkataba wa DP World

Etwege

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2018
Posts
7,207
Reaction score
17,674
Baada ya kuchukua bandari zote za Tanganyika kwa mkataba wa kimangungo kwa ahadi kemukemu ambazo hazijaandikwa popote kwamba watazifanya bandari kuwa bora kwa kuvutia mizigo Afrika nzima, wameenda Kenya wakawasainisha mkataba uleule wa kimangungo kwamba watazifanya bandari zao kuwa bora Afrika nzima!

Yani ni sawa na mchezaji anasaini Yanga na kuwaahidi atawafungia magoli mengi balaa msimu huu, baada ya hapo anaenda kusaini tena Simba na kuwaahidi atawafungia magoli mengi balaa msimu huu! Inawezekanaje?

Ina maana hakuna kipengele chochote cha kumbana huyu DP world? Yani kazi ya DPW ni kurundika mashariti tu kwa nchi inazowekeza ila yenyewe hamna kuwekewa shariti hata moja?

Ndiyo maana Prof Shivji akasema kwenye mkataba huu haki zote ni za DP world na wajibu wote ni wa serikali ya Tanzania. Tanzania haina haki yoyote ya kuwawekea hata kipengele kwamba mkishawekeza kwenye bandari za Tanzania basi musiwekeze tena kwenye bandari za washindani wetu kwa terms zilezile na zetu.!

Serikali imepeleka mswada bungeni wa kuifanya sheria ya kulinda rasilimali za taifa iliyotungwa mwaka 2017 na kusainiwa na aliyekuwa rais Hayati Magufuli kuwa isitumike tena ili kuwapa nafasi kampuni la DP world kuchukua bandari zote za Tanganyika na kuziwekeza kadiri watakavyoona inafaa.

Ikumbukwe wakati sheria ya kulinda rasilimali za taifa inatungwa waziri mkuu alikuwa ni huyu Kassim Majaliwa , naibu spika alikuwa ni Dk Tulia, makamu wa rais alikuwa ni Samia Suluhu, waziri wa sheria alikuwa ni Mwigulu Nchemba, na wabunge waliopitisha bungeni ni hao hao wa CCM!

Watu ni walele na chama ni kilele waliotaka na kuona kuna umuhimu wa kutunga sheria ya kulinda rasilimali za taifa ,lakini sasa ni haohao hawaitaki tena hiyo sheria, wanaona hamna haja ya kuwa na sheria ya kulinda rasilimali za taifa.!

Je, wakati wanaitunga na kuipitisha hii sheria waliipitisha kwa kuwa walikuwa na uchungu wa rasilimali za taifa kutoka moyoni? Au walipitisha tu kwa sababu tu rais alikuwa ni Magufuli?

Tunaposema Magufuli alizungukwa na wanafiki kutoka kichwani hadi miguuni mtuelewe jamani.

 
Mwanasiasa sio mtu wa kumuamini hata kidogo tena hasa wanasiasa wa Tanzania, wao wanachojali ni maslahi yao binafsi tu. Popote upepo unapovuma wao wanaegemea hukohuko
 
Baada ya kuchukua bandari zote za Tanganyika kwa mkataba wa kimangungo kwa ahadi kemukemu ambazo hazijaandikwa popote kwamba watazifanya bandari kuwa bora kwa kuvutia mizigo Afrika nzima, wameenda Kenya wakawasainisha mkataba uleule wa kimangungo kwamba watazifanya bandari zao kuwa bora Afrika nzima!

Yani ni sawa na mchezaji anasaini Yanga na kuwaahidi atawafungia magoli mengi balaa msimu huu, baada ya hapo anaenda kusaini tena Simba na kuwaahidi atawafungia magoli mengi balaa msimu huu! Inawezekanaje?

Ina maana hakuna kipengele chochote cha kumbana huyu DP world? Yani kazi ya DPW ni kurundika mashariti tu kwa nchi inazowekeza ila yenyewe hamna kuwekewa shariti hata moja?

Ndiyo maana Prof Shivji akasema kwenye mkataba huu haki zote ni za DP world na wajibu wote ni wa serikali ya Tanzania.

Tanzania haina haki yoyote ya kuwawekea hata kipengele kwamba mkishawekeza kwenye bandari za Tanzania basi musiwekeze tena kwenye bandari za washindani wetu kwa terms zilezile na zetu.!

Serikali imepeleka mswada bungeni wa kuifanya sheria ya kulinda rasilimali za taifa iliyotungwa mwaka 2017 na kusainiwa na aliyekuwa Rais Hayati Magufuli kuwa isitumike tena ili kuwapa nafasi kampuni la DP world kuchukua bandari zote za Tanganyika na kuziwekeza kadiri watakavyoona inafaa.

Ikumbukwe wakati sheria ya kulinda rasilimali za taifa inatungwa waziri mkuu alikuwa ni huyu Kassim Majaliwa , naibu spika alikuwa ni Dk Tulia, makamu wa rais alikuwa ni Samia Suluhu, waziri wa sheria alikuwa ni Mwigulu Nchemba, na wabunge waliopitisha bungeni ni hao hao wa CCM!

Watu ni walele na chama ni kilele waliotaka na kuona kuna umuhimu wa kutunga sheria ya kulinda rasilimali za taifa ,lakini sasa ni haohao hawaitaki tena hiyo sheria, wanaona hamna haja ya kuwa na sheria ya kulinda rasilimali za taifa.!

Je, wakati wanaitunga na kuipitisha hii sheria waliipitisha kwa kuwa walikuwa na uchungu wa rasilimali za taifa kutoka moyoni? Au walipitisha tu kwa sababu tu rais alikuwa ni Magufuli?

Tunaposema Magufuli alizungukwa na wanafiki kutoka kichwani hadi miguuni mtuelewe jamani.
 
Ama kweli masikini Hana kauli kwa mwenye fedha, upo sahihi kabisa kwa Sababu kama wao wametupa mashariti ya kutoruhusu mwekezaji mwingine kwenye bandari na wao lazima tuwekeane nao makibaliano ya kutokuwekeza kwa mshindani wetu tena ili tuweze kunufaika zaidi.

Lakini kama atawekeza the same way na alivyowekeza kwetu inamaana Yuko huru sana kufanya atakavyo na wakati huo sisi hatuna la kumfanya
 
Watu wenye maoni tofauti wavumiliwe kuna ukweli fulani wanauona wasipuuzwe. Mkataba DP World ni mkataba wa kipuuzi kuwahi kutokea ulimwenguni.

Sasa kama wakipata kenya, tanzania, msumbiji, afrika kusuni, somalia, djibout, eritrea hamuoni kuwa huu utakuwa ukoloni kwa taifa moja la ng'ambo kutawala pwani yote ya mashariki ya afrika?

DP itatawala biashara zote zitakozafanyika katika bahari za nchi hizo kwa mawanda yote. Ni ukoloni kiuchumi kutakapopelekea wajiingize kwenye siasa ili kulinda maslahi yao kwa gharama yoyote ikibidi kupenyeza vibaraka wao. Straggle for existance/fittest dubai si mjinga kutaka kenya na tanzania awekeze
 
Watu wenye maoni tofauti wavumiliwe kuna ukweli fulani wanauona wasipuuzwe. Mkataba DP World ni mkataba wa kipuuzi kuwahi kutokea ulimwenguni. Sasa kama wakipata kenya, tanzania...
Upo sahihi, waarabu wameamua kurudisha ile milki yao ya pwani ya bahari ya Hindi iliyoanzia lamu hadi Mikindani enzi hizo kabla ya kupokonywa na German East Afrika.

Huu uwekezaji wa hawa waarabu siyo wa bahati mbaya, ni calculations za muda mrefu. Sasa Kwa Tanzania wamepata bwerere kupitia mswahiba wao wa kizanzibari ambao sasa ni viongozi katika Serikali ya JMT. Watanzania tusikubali ukoloni huu wa waarabu kupitia viongozi wetu wa kiafrika/Tanzania
 
mind kuwa wana historia hiyo katika makabrasha yao. Watajitanua sana na kujiingiza kwenye siasa ama wao au kwa kutumia vibaraka wao hawa wanaowapigia debe kuwa mkataba wao ni mzuri. Mikataba ni kitu kibaya sana lazima mwenye mali apoteze na aliyeingia apate. Lile ni taifa linalotaka kutawala taifa jingine kiuchumi na baadaye kisiasa na kitamaduni. Hata hii zanzibar ikiendelea kuwatukuza hao masultan ipo siku watarudi zanzibar na kutawala tena. Historia wanayo kuwa mababu zao walitawala ukanda huo
 
Back
Top Bottom