Kenya yapiga marufuku uvuvi kwenye mpaka wake na Somalia

Kenya yapiga marufuku uvuvi kwenye mpaka wake na Somalia

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
media

Bahari Hindi
Kenya imepiga marufuku shughuli za uvuvi katika Bahari ya Hindi karibu na nchi ya Somalia, kwa sababu za kiusalama.

Afisa wa serikali katika Kaunti ya Lamu, Joseph Kanyori, amesema wavuvi wote wamezuiwa kwenda kuvua katika maeneo ya Ras Kamboni na karibu na mji wa Kiunga unaopakana na nchi hizo mbili.

Kanyori ameliambia Gazeti la kila siku nchini humo la Daily Nation kuwa, hatua hiyo imechukuliwa kwa sababu za kiusalama.

Aidha, ameeleza kuwa eneo hilo la bahari limeshuhudia utekaji wa wa binadamu, dawa za kulevya pamoja na bidhaa zingine wakati huu usalama ukiimarishwa.

Marufuku haya yanakuja wakati huu Kenya na Somalia zikiwa kwenye mvutano wa kidiplomasia kuhusu mmiliki wa eneo la Bahari Hindi, linaloamiwa kuwa na utajiri wa gesi na mafuta.

Somalia imekwenda kuishtaki Kenya katika Mahakama ya Kimataifa, kulalamikia tatizo hilo la mpaka wa majini huku, ripoti zikieleza kuwa, Somalia inaungwa mkono na mataifa ya nje.

Mogadishu imetishia kumwondoa Balozi wake jijini Nairobi.
 
Israel vs Hamas
India vs Pakistan

Hawa ndio huwa nawakubali hawanaga utani wakiamua ni mtanange kweli kweli lkn Kenya maneno mengi
 
media

Bahari Hindi
Kenya imepiga marufuku shughuli za uvuvi katika Bahari ya Hindi karibu na nchi ya Somalia, kwa sababu za kiusalama.

Afisa wa serikali katika Kaunti ya Lamu, Joseph Kanyori, amesema wavuvi wote wamezuiwa kwenda kuvua katika maeneo ya Ras Kamboni na karibu na mji wa Kiunga unaopakana na nchi hizo mbili.

Kanyori ameliambia Gazeti la kila siku nchini humo la Daily Nation kuwa, hatua hiyo imechukuliwa kwa sababu za kiusalama.

Aidha, ameeleza kuwa eneo hilo la bahari limeshuhudia utekaji wa wa binadamu, dawa za kulevya pamoja na bidhaa zingine wakati huu usalama ukiimarishwa.

Marufuku haya yanakuja wakati huu Kenya na Somalia zikiwa kwenye mvutano wa kidiplomasia kuhusu mmiliki wa eneo la Bahari Hindi, linaloamiwa kuwa na utajiri wa gesi na mafuta.

Somalia imekwenda kuishtaki Kenya katika Mahakama ya Kimataifa, kulalamikia tatizo hilo la mpaka wa majini huku, ripoti zikieleza kuwa, Somalia inaungwa mkono na mataifa ya nje.

Mogadishu imetishia kumwondoa Balozi wake jijini Nairobi.
Huwezi kuchagua aina ya jirani wa kuishi naye !!!.
 
Back
Top Bottom