Kenyan & Tanzanian Surburbs

kuna point moja muhimu sana ndugu zangu, msisahau pirates katika bahari ya hindi ambao pia ni wasomalia wanaishi kenya na mamilion ya dollars wanayo yapata kwakazi hio yanakwenda kenya kununua na kujenga majumba ya kifahari kama hayo.

hilo nalo neno mkuu, waziri wa ulinzi wa kenya bw yusuf haji, ambaye ni msomali wa kenya, alisema kichwa cha al shabaab kiko kenya eastleigh na mkia ndio uko somalia. Jamaa mihela yote wanawekeza kenya, kwao hakukaliki. Ikumbukwe kuna wasomali asilimia kubwa sana wenyeji wazawa wa kenya wakichanganyika na wa kutoka somalia huwezi kuwatofautisha.
 

Tatizo la TZ siasa nyingi na maneno mengi wakati vitendo hakuna..hata RWANDWA wanatuacha tunabaki tunashangaa.
 
kuna point moja muhimu sana ndugu zangu, msisahau pirates katika bahari ya Hindi ambao pia ni wasomalia wanaishi Kenya na mamilion ya dollars wanayo yapata kwakazi hio yanakwenda Kenya kununua na kujenga majumba ya kifahari kama hayo.
mipango miji iliyopo Kenya kumbuka ni ya tangia hata hizo pirating activities zilikuwa hazijaanza.

Jamani watz, tukubali ukweli kuwa 'uswahili' umetuzidi na umetuponza then tuanzia hapa kurekebisha makosa. Kuendelea kubisha juu ya haya ni kuendelea 'kuwaacha wakazi wa jangwani' kujenga "vijiji ndani ya Jiji"

 
The area around Naivasha is also developing quite fast;


😛oa
 
Last edited by a moderator:
Huu uzi umenifurahisha sana waTz tumeishiwa maneno! Ukweli kenya wanatuacha mbali kny swala la makazi,wenzetu mtu binafsi anainvest estates za apartments na ni well planned with low rent! Ingawa serikali ya kenya imetumia nguvu nyingi kuijenga Nairobi zaidi kiasi kila mkenya ukimuuliza anasema natoka Nrb hata kama ni wa central KE!
 
Kinachonifanya niupende uzi huu ni kuwa umetupa ushahidi ikiwa watu wakiwa serious mambo hufanyika, siku zote watu wamekuwa wakisifiana kuwa wamefanya kazi kubwa na kutufanya tunaolalamikia utendaji kuwa si wazalendo. Kama nchi inaweza kufanya kama hivi au hata nusu ya hivi kwa nini isipongezwe, kila siku wawekezaji ooh wafadhili. Hawa kuna kipindi hawakupata msaada wa mtu yeyote na wemekuwa na mipango thabiti na wemeweza kuitekeleza, najua si yote waliyotamani lakini wamefanya kitu. Waswahili wanasema penye nia pana njia, hawa kweli wanayonia lakini sio sisi.
Hiki ndio kinachotufanya wengine kuingia kwenye mitandao ya kijamii kupaza kilio chetu kuwa mambo si sawa, ingawa tunaambia mitandao ya kijamii haiendeshi serekali. Tunatamani tuone kama haya, tuone viongozi wetu wapanga na kuongoza kuelekea mwelekeo huu wala hamtatuona kulalamika kwenye mitandao hii.
Asante wewe uliyeanzisha huu uzi ingawa uliuanzisha kwa mashindano, umetusaidia kupata kielelezo ya kile tunachopigia kelele humu wakati wote.
Tunaweza kufanya haya yote kama viongozi wetu mtakuwa na vision, msione aibu kutafuta kujifunza toka kwa wenzetu.
 
Hakuna kutukuza ujinga we are not prepared at all... our neighbors are forging ahead...
 
Arusha Gallery. Ngoma, mkuki na ngao. Ukinunua hapa kitu, wanakutumia hadi nyumbani kwenu popote pale duniani kwa kupitia DHL, hapo vipi wandugu ?!


One of the many works by kenyan architects.....i hate this one though.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…