Kenyatta ana kwa ana na ICC

Kenyatta ana kwa ana na ICC

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
Kenyatta ana kwa ana na ICC

10703746_862177320467601_5670308694828991977_n.jpg





141008075142_uhuru_kenyatta_640x360_bbc_nocredit.jpg

Rais Uhuru Kenyatta ICC

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, amefika mbele ya mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC huko Hague, ambako anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu dhidi ya binaadamu.

Yeye ni kiongozi wa kwanza wa taifa kuwasili mbele ya mahakama hiyo.

Kenyatta amefika mbele ya mahakama hiyo baada ya waendesha mashtaka kuishutumu serikali ya Kenya kukata kuwasilisha ushahidi muhimu.


Kenyatta amekanusha madai ya kupanga na kufadhili ghasia za kikabila nchini Kenya baada ya uchaguzi uliokumbwa na utata mwaka 2007/2008.


Kikao cha leo kitatathmini ombi la upande wa mashitaka la kutaka kuahirishwa kwa kesi hiyo hadi pale serikali ya Kenya itakapoikabidhi mahakama hiyo ushahidi unaohitajika kuhusiana na mali ya Rais Kenyatta.


Upande wa utetezi nao unataka kesi hiyo ifutiliwe mbali ukisema kuwa upande wa mashitaka hauna ushahidi wa kutosha kwa kesi hiyo kuendelea.


Kiongozi wa mashitaka Fatou Bensouda, amewasili mahakamani akisema kesi hiyo iko katika awamu muhimu sana.

Kenyatta ameamua kukaa kimya akimtaka wakili wake kuongea kwa niaba yake.chanzo.
http://www.bbc.co.uk/swahili/habari/…/10/141008_kenyatta_icc
 
Back
Top Bottom