Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 12,699
- 22,598
Sipatani sana na wanasiasa kwa sababu moja kuu; wengi wao wamekithiri kwa uongo na ahadi za udanganyifu, kuanzia wenyeviti wa mitaa, wabunge, mawaziri au hata maraisi. Nionyeshe mwanasiasa asiye mdanganyifu nitakuonyesha mtu asiyestahili kuwa mwanasiasa.
Chukulia Kenyatta kwa mfano, raisi wa sasa wa Kenya.
Wakati wa kampeni za uraisi alitoa ahadi kwamba kuwa na kesi ICC si hoja, kwani akifanikiwa kuwa raisi atashirikiana na ICC kikamilifu ili kumaliza suala la tuhuma za ICC dhidi yake - tuhuma nzito kabisa zinazohusu mauaji ya watu wasio na hatia.
Baada ya kuwa raisi Kenyatta ameanza kuimba nyimbo tofauti kabisa; kwanza alianza kampeni ili nchi za Afrika kwa ujumla zijitoe ICC. Hakufanikwa katika hili. Na sasa maraisi wa Afrika katika mkutano wao huko Ethiopia wameamua kuliandikia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wakiomba/wakidai kwamba mtu anapokuwa madarakani kama raisi asishitakiwe katika ICC!
Natumaini busara ya wale wanaokaa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa la sasa ni ya kiwango cha juu kuliko wale walioliandikia ombi/dai la kutaka maraisi waliopo madarakani wasishitakiwe ICC.
Ukitafakari ombi la maraisi wa Afrika, utaona kwamba wanachomaanisha hawa viongozi wa bara langu la Afrika ni kwamba, kukiwa na kiongozi dikteta na muuaji, aruhusiwe kuendelea kuua tu asishitakiwe hadi atakapoacha madaraka ya uraisi.
Pia, hadi sasa nashindwa ni mtu gani mwenye busara kamili anaweza kujitetea kwamba eti ni Waafrika pekee wanaoshitakiwa ICC, sio wazungu. Mtoto wa shule ya msingi? Hivi ni kwa jinsi gani maraisi wa nchi wanaweza kujitetea kwamba mbona wazungu wanaua kama sisi Waafrika lakini hawapelekwi ICC? Khaaa!!! Kwa hiyo, kwa busara zenu enyi waheshimiwa maraisi, mnaona kwamba ili kusawazisha hili kinachohitajika ni kuwaruhusu maraisi wa Kiafrika waue bila kushitakiwa kama wanavyofanyiwa maraisi wa kizungu?
Mtu hadi unachaguliwa kuwa raisi wa nchi yako bado unakosa busara juu ya basic principle kwamba "two wrongs will never make a right?" Just unbelievable.
Kama kweli maraisi wangu wa Afrika wangekuwa na nia na busara ya kutaka kujadili kutoshitakiwa na ICC maraisi waliopo madarakani, wangejadili na maswali yafuatayo;
Haya ndio mambo ya msingi ambayo kama kweli maraisi wetu wangepaswa kuyajadili. La sivyo wanaongea vitu ambavyo vinapoteza muda si wetu tu bali hata wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na binafsi nawasikitikia hao waliowachagua kuwa maraisi. Wanatutia aibu sisi Waafrika wengine kudai mambo yanayolinda usalama wa wana Afrika yaondolewe kwa sababu za ki Abunuwasi kama wanazozitoa.
Chukulia Kenyatta kwa mfano, raisi wa sasa wa Kenya.
Wakati wa kampeni za uraisi alitoa ahadi kwamba kuwa na kesi ICC si hoja, kwani akifanikiwa kuwa raisi atashirikiana na ICC kikamilifu ili kumaliza suala la tuhuma za ICC dhidi yake - tuhuma nzito kabisa zinazohusu mauaji ya watu wasio na hatia.
Baada ya kuwa raisi Kenyatta ameanza kuimba nyimbo tofauti kabisa; kwanza alianza kampeni ili nchi za Afrika kwa ujumla zijitoe ICC. Hakufanikwa katika hili. Na sasa maraisi wa Afrika katika mkutano wao huko Ethiopia wameamua kuliandikia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wakiomba/wakidai kwamba mtu anapokuwa madarakani kama raisi asishitakiwe katika ICC!
Natumaini busara ya wale wanaokaa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa la sasa ni ya kiwango cha juu kuliko wale walioliandikia ombi/dai la kutaka maraisi waliopo madarakani wasishitakiwe ICC.
Ukitafakari ombi la maraisi wa Afrika, utaona kwamba wanachomaanisha hawa viongozi wa bara langu la Afrika ni kwamba, kukiwa na kiongozi dikteta na muuaji, aruhusiwe kuendelea kuua tu asishitakiwe hadi atakapoacha madaraka ya uraisi.
Pia, hadi sasa nashindwa ni mtu gani mwenye busara kamili anaweza kujitetea kwamba eti ni Waafrika pekee wanaoshitakiwa ICC, sio wazungu. Mtoto wa shule ya msingi? Hivi ni kwa jinsi gani maraisi wa nchi wanaweza kujitetea kwamba mbona wazungu wanaua kama sisi Waafrika lakini hawapelekwi ICC? Khaaa!!! Kwa hiyo, kwa busara zenu enyi waheshimiwa maraisi, mnaona kwamba ili kusawazisha hili kinachohitajika ni kuwaruhusu maraisi wa Kiafrika waue bila kushitakiwa kama wanavyofanyiwa maraisi wa kizungu?
Mtu hadi unachaguliwa kuwa raisi wa nchi yako bado unakosa busara juu ya basic principle kwamba "two wrongs will never make a right?" Just unbelievable.
Kama kweli maraisi wangu wa Afrika wangekuwa na nia na busara ya kutaka kujadili kutoshitakiwa na ICC maraisi waliopo madarakani, wangejadili na maswali yafuatayo;
- ICC ifanyeje basi, pale raisi dikteta na muuaji yuko katika nchi ambayo katiba yake haina ukomo wa kugombea uraisi (kama Zimbabwe, Uganda nk)? Je, ICC isubiri hadi huyo raisi atakapokufa ndio imfungulie mashitaka?
- Je, kwa kutaka maraisi waliopo madarakani wasifunguliwe mashitaka ICC, maraisi wa Afrika watakuwa tayari pia kuhakikisha katiba za nchi zote Afrika zina ukomo wa vipindi vya uraisi, viwili visivyozidi miaka mitano kila kimoja?
- Je, ikiwa maraisi wa Afrika wanataka raisi aliyepo madarakani asifunguliwe mashitaka ICC, watakubali kwamba mtu yeyote mwenye tuhuma za mauaji asiruhusiwe kugombea uraisi katika nchi yeyote, eidha kabla hajawa raisi au kutogombea muhula mwingine ikiwa yeye ni raisi tayari? (kwa mantiki hii Kenyatta asingegombea uraisi Kenya kwa kuwa alikuwa na tuhuma tayari, au asiruhusiwe kugombea uraisi awamu ya pili)
Haya ndio mambo ya msingi ambayo kama kweli maraisi wetu wangepaswa kuyajadili. La sivyo wanaongea vitu ambavyo vinapoteza muda si wetu tu bali hata wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na binafsi nawasikitikia hao waliowachagua kuwa maraisi. Wanatutia aibu sisi Waafrika wengine kudai mambo yanayolinda usalama wa wana Afrika yaondolewe kwa sababu za ki Abunuwasi kama wanazozitoa.