DP Ruto wanted to kick me out before end of my term - Uhuru
Rais UK alikuwa anazungumza na wazee na viongozi wengine kutoka eneo la ML. KENYA. Eneo la mlima Kenya linajumuisha gatuzi kadhaa kutoka mikoa ya zamani ya Central na Eastern, ambazo zina watu wa aina tofauti. Hakuwa anazungumza na wakikuyu tu kama mleta mada anavodai. Kunao wameru, waembu, watharaka pia.
Alidai kwamba DP Ruto alitaka kuwashawishi wabunge wapitishe mswada wa kukosa imani naye, almaarufu kama 'impeachment', ili wamng'atue. Hio ni njia ya kumuondoa rais aliye madarakani, ambayo inakubalika kisheria. Hili ni jukwaa la great thinkers mleta mada, huku huwa tunajadili facts sio umbea. Mada yako ilifaa iambatane na taarifa kutoka 'source' rasmi kama hiyo hapo, ili wadau(na hawa mabendera fuata upepo wengine) waweze kujisomea wenyewe.