Kenyatta si Mwanademokrasia ila Katiba ya Kenya ni ya Kidemokrasia

Kenyatta si Mwanademokrasia ila Katiba ya Kenya ni ya Kidemokrasia

Ufipa-Kinondoni

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2012
Posts
4,582
Reaction score
2,783
pic+kenya.jpg


Nimejaribu kufuatilia sana purukushani za uchaguzi wa Kenya mpaka sasa. Nimesoma haya:

1. Katiba ya Kenya ni zuri sana na haijatoa mwanya wa mtu kujiinua;

2. Kenyatta anaroho ya kutokubali demokrasia ila anafungwa na Katiba. Natolea mfano wa matamushi aliyotoa juu ya wale walioamua kesi ya uchaguzi. Amewaita kwa maneno mengi sana. Ila kubwa ni lile alilosema ni "wakora". Sina maana kamili kwa kiswahili cha kwetu, ila naamini anamaanisha wanyang'anyi. Ameendelea kusema kuwa majaji wote waliompigia kura za kuopinga uchanguzi wamefanya maamuzi hayo kisiasa. Hili ni kweli? Ni jambo la kujiuliza.

Kwa sababu hiyo, leo Chama cha Mawakili nchini Kenya (LSK) kimemkosoa Rais Uhuru Kenyatta baada ya kuwashambulia majaji wa mahakama ya juu kufuatia uamuzi wa kubatilisha uchaguzi wake.

Rais wa LSK Isaac Okero alimkosoa Rais Kenyatta kwa kumtaja Jaji Mkuu David Maraga na majaji wengine wa mahakama hiyo kuwa wamekosea.

Okero amesema Matamshi ya rais kwamba majaji hao wasubiri rais achaguliwe katika uchaguzi ujao hayafai kutoka kwa kiongozi wa taifa ambaye chini ya katiba ya Kenya ni nembo ya umoja wa Wakenya.

Wewe unasemaje hapo? Kenyatta ni mwanademokrasia au ni Katiba imemfunga?
 
Wale wapambe wake kutoka bavicha wako kimyaa. Wameumbuka babu kubwa.

Hoja ipo very clear..... Hujaelewa nini?

Tunapongeza katiba nzuri, uhuru wa mahakama

Ndio sababu tunadai katiba bora mpya ya jaji Warioba fulstop.
 
Hoja ipo very clear..... Hujaelewa nini?

Tunapongeza katiba nzuri, uhuru wa mahakama

Ndio sababu tunadai katiba bora mpya ya jaji Warioba fulstop.
Ha ha ha, hoja ipo very clear sio? Kenyatta ni Mandela wa pili. Duh.
 
Pamoja na Uzuri wa katiba ya Kenya ila Kenyatta ameonyesha ukomavu maana hata hao wenye katiba Mbovu watawala wameshindwa kuheshimu viapo vyao na kujikuta wakiishi juu ya katiba na si ndani ya katiba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maneno ya Nyerere yako wazi juu ya Katiba yetu. Inampa nafasi kubwa sana rais.

Ila ukiangalia kwa Kenya na matamshi ya Uhuru utagundua kuwa anaogopa msingi ya katiba tu na si matendo yaliyofanya na Tume ya Uchaguzi.
Pamoja na Uzuri wa katiba ya Kenya ila Kenyatta ameonyesha ukomavu maana hata hao wenye katiba Mbovu watawala wameshindwa kuheshimu viapo vyao na kujikuta wakiishi juu ya katiba na si ndani ya katiba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hoja ipo very clear..... Hujaelewa nini?

Tunapongeza katiba nzuri, uhuru wa mahakama

Ndio sababu tunadai katiba bora mpya ya jaji Warioba fulstop.
Kwa hiyo sasa hivi hamumpongezi tena Uhuru Kenyatta Bali mnapongeza katiba nzuri na Uhuru wa mahakama! Machadema pasua kichwa kwa ukigeugeu! Fanna audhubillah minndhalika!! Wallah!
 
Katiba peke yake bila utashi wa kisiasa si kitu,hapa kwetu katiba inatoa uhuru wa mawazo,mikutano na maandamano,mbona vyote vimezuiwa kwa amri kutoka juu? Rais Kenyatta angekuwa na hulka ya kidikteta hakuna chombo chochote kingeweza kumzuia,yeye ndiye mkuu wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama,angeweza kutoa amri ya kuwaswaga kama kuku wale wote ambao wangeleta fyokofyoko,lakini kwa sababu ya kutanguliza uzalendo wake,hakuona sababu ya kumwaga damu za Wakenya ili abaki madarakani,amekuwa mnyenyekevu na mtii kwa Taifa lake kuliko kujivunia vyeo.

Hapa kwetu mtu kuongea ukweli tu anaitwa mchochezi,sasa hivi kuna makosa mapya kabisa yamedownloadiwa na vyombo vya dola,nayo ni kumsema rais hadharani.Tundu Lissu alikamatwa kwa kosa la kumsema rais hadharani,kwamba hakupaswa kuusema ukweli juu ya kushikiliwa kwa ndege yetu,alipaswa apige kimya! Sasa kama mtu anadiliki kuwakamata wanaomkosoa huku katiba ikiruhusu ukosoaji,kwa nini msiitwe madikteta?

Kumfananisha Rais Kenyatta na miungu watu yenu ni uhayawani wa kiwango cha lami!Kenyatta ni mdemokrasia,mzalendo na mcha Mungu,anastahili pongezi,yeye ndiye alama ya sababu za kusifiwa kwa demokrasia ya Kenya,angekuwa mbinafsi leo hii tungekuwa tumeshawapokea Wakenya kama wakimbizi.
 
Swala la Uhuru kuwa mwana demokrasia halikwepeki iwe kwa kubanwa na katiba au vinginevyo... Huyo mwingine mbona kuna mambo katiba iko wazi kabisa inataka jambo lifanyike hivi yeye anafanya anavyotaka yeye.... Katiba kutaka jambo na Uhuru kuheshimu matakwa ya kikatiba vimeenda sambamba kwa hilo wacha asifiwe tu... Angalia kwenye nchi ya kufikirika Mahakama inaweka zuio, mfalme alietukuka wa nchi ile anawaambia wavunjaji "bomoeni tu" .... Ukiona Uhuru anasifiwa amejipambanua tofauti na wenzie wote... Kuanzia maandamano ya kupinga uchaguzi mpaka sasa... Kwa wengine hata kwenda kutoa pole kwa wahanga wa ajali ni kosa.... Mwache Uhuru aitwe Uhuru matamshi baada ya hukumu ni ghadhabu za kibinadamu tu.

"A voice of one calling in the wildernes"
 
Tuache unafiki, kuna haki za msingi kabisa zimeainishwa kwenye katiba yetu lkn zinageuzwa hisani na nchi sasa inatawaliwa kwa matakwa ya mtu moja.

Ni kweli, Uhuru anajaribu sana kuongoza kwa mujibu wa katiba tofauti na wenzake wengi ktk eneo hili. Ukweli lazima usemwe tu.
 
Kuheshimu Katiba na Sheria za nchi ambazo pia zinatambua separation of power ndio sifa kuu na ya msingi ya kiongozi mdemokrasia na mzalendo. Yaani ww hata sheria mama ya nchi huiheshimu halafu unajipa uzalendo wapi na wapi? Uhuru anastahili heshima ya uanademokrasia na uzalendo kwa taifa lake.
 
Katiba peke yake bila utashi wa kisiasa si kitu,hapa kwetu katiba inatoa uhuru wa mawazo,mikutano na maandamano,mbona vyote vimezuiwa kwa amri kutoka juu? Rais Kenyatta angekuwa na hulka ya kidikteta hakuna chombo chochote kingeweza kumzuia,yeye ndiye mkuu wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama,angeweza kutoa amri ya kuwaswaga kama kuku wale wote ambao wangeleta fyokofyoko,lakini kwa sababu ya kutanguliza uzalendo wake,hakuona sababu ya kumwaga damu za Wakenya ili abaki madarakani,amekuwa mnyenyekevu na mtii kwa Taifa lake kuliko kujivunia vyeo.

Hapa kwetu mtu kuongea ukweli tu anaitwa mchochezi,sasa hivi kuna makosa mapya kabisa yamedownloadiwa na vyombo vya dola,nayo ni kumsema rais hadharani.Tundu Lissu alikamatwa kwa kosa la kumsema rais hadharani,kwamba hakupaswa kuusema ukweli juu ya kushikiliwa kwa ndege yetu,alipaswa apige kimya! Sasa kama mtu anadiliki kuwakamata wanaomkosoa huku katiba ikiruhusu ukosoaji,kwa nini msiitwe madikteta?

Kumfananisha Rais Kenyatta na miungu watu yenu ni uhayawani wa kiwango cha lami!Kenyatta ni mdemokrasia,mzalendo na mcha Mungu,anastahili pongezi,yeye ndiye alama ya sababu za kusifiwa kwa demokrasia ya Kenya,angekuwa mbinafsi leo hii tungekuwa tumeshawapokea Wakenya kama wakimbizi.
You guys, the constitutional gives power the president to do any thing. Kwa hiyo Dogo hayo yote anayoyafanya ni kwa mujibu wa katiba inayompa mamlaka hayo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom