Kero hii inakuwaje?

JICHO LA 3

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2011
Posts
356
Reaction score
62
Jamani wale wenzangu na mie wadadakwa wakaka tunaopanda daladala..
utakuta mtu kwenye daladala anasikiliza mziki kwenye simu yake
simu yenyewe ya kichina, nasema ya kichina cz ni simu zinazoongoza kwa kelele
badala ya kuweka headphone ili iwe kwa faida yake yeye anaweka sauti ya nje tena kali sana kiasi kwamba inakuwa kero kwa abiria mwenzake
wengine kuongea hatuwezi sababu huwezi jua unaemwambia atachukulia vipi suala hilo lkn kiukweli inaudhi.
ombi langu kama wengine mnatabia kama hizi bs jirekebisheni.
 
unamwambia tu....
hata dereva akifungulia mziki kwa kelele mnamwambia tu....
 
The boss...nnachoogopa hapa ni jinsi gani atakavochukulia
maana kuna wengine unaweza jikuta ukazua ugomvi
si unajua kila binadamu na uelewa wake.
 
The boss...nnachoogopa hapa ni jinsi gani atakavochukulia
maana kuna wengine unaweza jikuta ukazua ugomvi
si unajua kila binadamu na uelewa wake.

ongea nae kistaarabu
mwambie dada/kaka punguza sauti ya mziki wako....
tumechoka sana wenzio.ataelewa tu kama mstaarabu...
asipoelewa basi unamuacha...

msichukulie kero ndogondogo kama za kupita....
zinaathiri sana.....ndo maana kila mtu akipata pesa
anakimbilia kununua gari,mwisho kero ya foleni inazidi...
 



daaah...itabidi nizichange kwa kweli maana.
ndomana foleni bongo zinazidi kwa sababu ya kukwepa kero kama hizi
 
Kama konda atamkaukia nakataa kulipa nauli ushenzi sitaki! Mtu umetulia zako unapanga mikakati halafu mtu anipigie kelele na konda anakaa kimya!
 
Huo ni ulimbukeni na kukosa ustaarabu, washenzi kabisa! Kwa nini starehe yao wanaifanya kuwa kero kwa wengine? Sipendi, nasema sipendi kabisa!
 

Hii thread km si mahala pake hv?!!
 
na washenzi wengine kwenye dala dala wana tabia za kujisogeza na kuwabana kina mama bila sababu,washenzi tu.
 
na washenzi wengine kwenye dala dala wana tabia za kujisogeza na kuwabana kina mama bila sababu,washenzi tu.
Mkuu kweli umechukia_maake hiyo lugha uliyotumia ni kali sana
 
wavumilie tu ukiwagusa zogo utakalolifumua hapo utajuta hata kwanini umo humo ndani......
 
mi ndo maana nowdayz sipandi daladala nakula za boda tu had kwa ofc
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…