Kero ya usafiri wa umma kwa wakazi wa Buza

Kero ya usafiri wa umma kwa wakazi wa Buza

oko majimaji

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2016
Posts
790
Reaction score
2,079
Habari Mabibi na Mabwana.

Naomba nisiwachoshe niende moja kwa moja kwenye kero, Kero hii inihusiana na usafiri wa umma kwa wakazi wa Buza ( kwa Lulenge hadi Kanisani). Hapo awali usafiri wa daladala kutokea maeneo tofauti kwenda Buza gari zilikuwa zinaenda hadi Buza Kanisani ( mwisho wa gari) lakini kuanzia jana tarehe 03 June 2024 daladala zote zimesitishwa kufika Buza Kanisani na zinatikiwa ziishie na kugeuzia Buza kwa Mama Kibonge.

Hili ni tatizo kwa wakazi wa maeneo ya kwa Lulenge hadi Kanisani kwa sababu ukitaka kwenda Kariakoo, Makumbusho, Mnazi Mmoja na kadharika itakubidi ukodi bodaboda au bajaji ili ufike stendi kwa Mama Kibonge ndio upate usafiri wa kwenda hayo maeneo niliyotaja.

Kutokana na kipato kidogo cha wakazi wa maeneo hayo ya Buza kwa Lulenge hadi Kanisani wamejikuta wakitembea umbali mrefu kufuata huduma ya usafiri, tatizo hili litakwenda kuwaathiri moja kwa moja wadogo zetu wanafunzi wa sekondari wanaosoma maeneo tofauti zaidi hawa wakike maana kwa vipato vyetu huku ni ngumu mzazi kumpa nauli ya pikipiki kila siku.

Pia kinachotusikiisha zaidi Buza Kanisani kuna kituo cha kugeuzia daladala kilijengwa na hakijatumiwa, kwanini wasiruhusu daladala zifike hadi Buza kanisani ndio zirudi zipitie hapo kituoni kwa Mama Kibonge kuliko kuwachosha watu watembee zaidi ya kilomita mbili kufata usafiri wa daladala.

Kupitia andiko hili nina imani mkuu wa mkoa Albert Chalamila litamfikia na ataona namna gani ya kutatua kero hii kwa maslahi mapana ya wananchi wa Buza.

Ahsanteni na niwatakie kazi njema.
 
Mtoa mada utanisamehe ila mnaokaa huko🙌 niishie hapa🤐
 
Ushamba mzigo mdogo wangu sasa JF wewe ndio umeona ujanja sio? Hii ni forum kwa ajili ya jamii
Hiyo ni tafsiri yako wewe. Uza simu kapange kwengine au ulitaka niulize unakaa buza na unaingia online. Huko mnaishije

Anyways just jokes
 
Habari Mabibi na Mabwana.

Naomba nisiwachoshe niende moja kwa moja kwenye kero, Kero hii inihusiana na usafiri wa umma kwa wakazi wa Buza ( kwa Lulenge hadi Kanisani). Hapo awali usafiri wa daladala kutokea maeneo tofauti kwenda Buza gari zilikuwa zinaenda hadi Buza Kanisani ( mwisho wa gari) lakini kuanzia jana tarehe 03 June 2024 daladala zote zimesitishwa kufika Buza Kanisani na zinatikiwa ziishie na kugeuzia Buza kwa Mama Kibonge.

Hili ni tatizo kwa wakazi wa maeneo ya kwa Lulenge hadi Kanisani kwa sababu ukitaka kwenda Kariakoo, Makumbusho, Mnazi Mmoja na kadharika itakubidi ukodi bodaboda au bajaji ili ufike stendi kwa Mama Kibonge ndio upate usafiri wa kwenda hayo maeneo niliyotaja.

Kutokana na kipato kidogo cha wakazi wa maeneo hayo ya Buza kwa Lulenge hadi Kanisani wamejikuta wakitembea umbali mrefu kufuata huduma ya usafiri, tatizo hili litakwenda kuwaathiri moja kwa moja wadogo zetu wanafunzi wa sekondari wanaosoma maeneo tofauti zaidi hawa wakike maana kwa vipato vyetu huku ni ngumu mzazi kumpa nauli ya pikipiki kila siku.

Pia kinachotusikiisha zaidi Buza Kanisani kuna kituo cha kugeuzia daladala kilijengwa na hakijatumiwa, kwanini wasiruhusu daladala zifike hadi Buza kanisani ndio zirudi zipitie hapo kituoni kwa Mama Kibonge kuliko kuwachosha watu watembee zaidi ya kilomita mbili kufata usafiri wa daladala.

Kupitia andiko hili nina imani mkuu wa mkoa Albert Chalamila litamfikia na ataona namna gani ya kutatua kero hii kwa maslahi mapana ya wananchi wa Buza.

Ahsanteni na niwatakie kazi njema.
poleni sana na mama yenu yuko Korea anatunukiwa mapiihechidii ya heshima akiwa ameambatana na wasanii.
 
Pole sana mkuu.
Pale Buza pana stendi ilijengwa tena ile ni ya serikali na ilianza kutumika na watu walikuwa wanakusanya mapato pale.

Toka jana ile pale kwa mama Kibonge imeanza kutumika ila ile ni ya mtu binafsi. Kila gari likitoka elfu 2 kitu ambacho nacho kinawaumiza watu wa magari.

Nakuhakikishia hiyo stendi miezi 6 haitofika itakufa kifo cha mende.

Sababu. Haijaja kutatua changamoto za jamii ila kuongeza changamoto na taabu nyingi.


POLENI SANA WAKUU WA KWA LULENGE,HOSPITAL,KANISANI,KWA MAKINDA HADI TANESCO
 
Pole sana mkuu.
Pale Buza pana stendi ilijengwa tena ile ni ya serikali na ilianza kutumika na watu walikuwa wanakusanya mapato pale.

Toka jana ile pale kwa mama Kibonge imeanza kutumika ila ile ni ya mtu binafsi. Kila gari likitoka elfu 2 kitu ambacho nacho kinawaumiza watu wa magari.

Nakuhakikishia hiyo stendi miezi 6 haitofika itakufa kifo cha mende.

Sababu. Haijaja kutatua changamoto za jamii ila kuongeza changamoto na taabu nyingi.


POLENI SANA WAKUU WA KWA LULENGE,HOSPITAL,KANISANI,KWA MAKINDA HADI TANESCO
Hata mimi nimewaza kitu kama hicho wanaforce stendi iwe kule kwa mama kibonge wana maslahi napo binafsi wamejenga maflemu kibao ili tu wapige hela serikali walichunguze kwa makini hili japo wao watakuja na hoja zoa uchwara.
 
Hata mimi nimewaza kitu kama hicho wanaforce stendi iwe kule kwa mama kibonge wana maslahi napo binafsi wamejenga maflemu kibao ili tu wapige hela serikali walichunguze kwa makini hili japo wao watakuja na hoja zoa uchwara.
Ile stend ni ya muda hadi imeota majan na wamefekaa weee sasa wanaona zle frem znakuwa mapagaleee.
Pale hamna kituuuu.
Yan kama stend ya temeke imeshindikana kuwa stend sembuse ile kulee ambayo imeleta kero kwa watuuu.

Stendi ya mabasi(kijichi) ya kwenda kusini nayo ilikufa hivi japo wao walijipanga ila ilikuwa na mapungufu ambayo ilibidi warud mbagala

Soon inakufa kifo kibaya.
 
Tuwapatie wakorea sehemu ya Bahari ili walete daladala Buza.
 
wameona mnaomba mno punguzo la nauli.
 
Back
Top Bottom