Kero yangu kuhusu "Timetable" kwa mabasi ya mikoani

Kero yangu kuhusu "Timetable" kwa mabasi ya mikoani

EHK

Member
Joined
May 19, 2011
Posts
74
Reaction score
96
Habari wanajamii,

Aisee nimekuja kuweka kero yangu hapa nikitumaini pengine mamlaka husika zitaona na kuangalia namna ya kutatua changamoto hii.

Nianze kwa kupongeza Serikali na mamlaka husika namna zinajitahidi kupunguza madhara yatokanayo na ajali za barabarani hususani kwa mabus. Siku hizi tunaona ajali bado zipo ila madhara ikiwemo idadi ya vifo etc ni kidogo kulinganisha na zamani hii ikimaanisha initiatives mbalimbali zilizowekwa zinafanya kazi. Initiatives hizo ni pamoja na kuweka ving'amuzi kwenye mabus, tochi, askari barabarani n.k.

Binafsi naamini kama initiatives hizo zikisimamiwa vizuri pengine kutakuwa ni suluhisho la kudumu ila pia naona kuna hili suala la timetable ambalo naona ni kero sana kwa abiria na sioni kama lina mantiki katika kuzuia mabus kukimbia. Hii ni kero kubwa hasa kwa mikoa ya nyanda za juu Kusini. Unakuta ratiba inasema kutoka Dsm, inabidi kufika stand ya Iringa, Igumbilo saa 7.30 mchana, sasa najiuliza kama tayari kuna tochi na ving'amuzi kwenye mabus ambavyo vina monitor speed ya chombo ili kitembee mwendo elekezi (80-85kph) kwanini bado unamwambia afike sehemu flan mda flan?.. Kwamba akiwahi inabidi asubiri sehemu hadi mda elekezi ufike! Hii inasababisha usumbufu na uchovu usio na lazima kwa abiria kwa kujikuta mnasimama sehemu karibia saa nzima ili tu kusubiri mda.

Hii naona sio sawa, badala yake mamlaka zingejikita katika kuhakikisha kuna ufanisi wa ving'amuzi, tochi nk. ikiwemo maoperator huko LATRA ili mabus yatembee mwendo elekezi mwanzo mwisho. Kuwepo na adhabu kali kisheria dhidi ya either operator ama askari wataoonekana "kula michongo" ili mabus/ kampuni flan yakimbie zaidi ya speed elekezi. Naomba mamlaka zifanyie kazi hili ama zitafute namna ya kutuondolea kero ya kusimama sehemu bila shughuli yeyote ili kusubiri timetable. Naomba kuwasilisha.
 
Mie nashauri mabasi kituo cha Magufuli ziondoke saa 2 asubuhi badala ya saa 12 alfajiri ili wale wanaotoka mjini kuwahi mabasi waondoke makwao alfajiri kumepambazuka kuepusha vibaka na majambazi.
 
Mie nashauri mabasi kituo cha Magufuli ziondoke saa 2 asubuhi badala ya saa 12 alfajiri ili wale wanaotoka mjini kuwahi mabasi waondoke makwao alfajiri kumepambazuka kuepusha vibaka na majambazi.
Siku hizi Kuna mabus yamejiongeza, yanafuata watu mpaka vitongojini..Si kusubiria abiria Mbezi..
 
Ukiwahi kufika maana yake ulikua unakimbia zaid ya 80kph mwndo ambao unahatarsha maisha ya abiria na watumiaji wengeni wa barabara

Sahiv watu wa mabus wamebuni mbinu ya kuwasha gar direct ile switch ya starter ikizimwa tu king'amuzi hakisomi muda huo gar imewashwa direct Sasa hapo ndo wanakimbia jins wanavyo taka

Unashangaa tu gari kwenye system imetoka dar had Moro inaonekana baada ya kufika Moro inapotea haionekan unakuja kuishtukia ipo iringa kumbe hapa katkat alizima switch kma vle gar imezimwa kumbe bado inamwaga moto

Ving'amuzi sahiv vmechezewa Sana ni kweny magar machache tu ndo vpo vzur
 
Mie nashauri mabasi kituo cha Magufuli ziondoke saa 2 asubuhi badala ya saa 12 alfajiri ili wale wanaotoka mjini kuwahi mabasi waondoke makwao alfajiri kumepambazuka kuepusha vibaka na majambazi.
Ndugu yangu Kuna mabasi ya saa12, saa1, saa2 sasa ni wewe tu uamuzi wako na ratiba yako
 
Ila mimi nina mawazo tofauti juu ya mabasi kumwaga moto, haiwezekani zama zile tuna miundombinu mibovu na mabasi ya teknolojia ya chini, mabasi yalikuwa yanatembea muda mfupi ukilinganisha na sasa.

Kinachotakiwa serikali iboreshe barabara zetu (barabara kuu ziwe njia 4) na pia kuondoa matuta yasiyo na msingi kisha madereva watembee mwendo mkali lakini salama (yaani kama barabara inaruhusu kutembea na 120 au 140) basi dereva afike tu maana wote ni mashahidi wa SU,PT, STL zinachofanya huko road! mbona wao hawafi!! mwendo wa kobe unachosha gari ziruhusiwe kumwaga moto
 
Ukiwahi kufika maana yake ulikua unakimbia zaid ya 80kph mwndo ambao unahatarsha maisha ya abiria na watumiaji wengeni wa barabara
Sahiv watu wa mabus wamebuni mbinu ya kuwasha gar direct ile switch ya starter ikizimwa tu king'amuzi hakisomi muda huo gar imewashwa direct Sasa hapo ndo wanakimbia jins wanavyo taka
Unashangaa tu gari kwenye system imetoka dar had Moro inaonekana baada ya kufika Moro inapotea haionekan unakuja kuishtukia ipo iringa kumbe hapa katkat alizima switch kma vle gar imezimwa kumbe bado inamwaga moto
Ving'amuzi sahiv vmechezewa Sana ni kweny magar machache tu ndo vpo vzur
Sasa katika mazingira haya ndio wayafatilie hayo mabus, likibainika wayachukulie hatua kali badala ya kuweka initiatives za kutesa abiria
 
Ila mimi nina mawazo tofauti juu ya mabasi kumwaga moto, haiwezekani zama zile tuna miundombinu mibovu na mabasi ya teknolojia ya chini, mabasi yalikuwa yanatembea muda mfupi ukilinganisha na sasa.
Kinachotakiwa serikali iboreshe barabara zetu (barabara kuu ziwe njia 4) na pia kuondoa matuta yasiyo na msingi kisha madereva watembee mwendo mkali lakini salama (yaani kama barabara inaruhusu kutembea na 120 au 140) basi dereva afike tu maana wote ni mashahidi wa SU,PT, STL zinachofanya huko road! mbona wao hawafi!! mwendo wa kobe unachosha gari ziruhusiwe kumwaga moto
haya pia ni mawazo mazuri ila kwa uchumi wa nchi yetu, sio mpango wa kesho ama kesho kutwa ni wa miaka mingi mbele ie kuweka double road, kikubwa ni userious katika njia mbalimbali walizoziweka tayari
 
Ukiwahi kufika maana yake ulikua unakimbia zaid ya 80kph mwndo ambao unahatarsha maisha ya abiria na watumiaji wengeni wa barabara
Sahiv watu wa mabus wamebuni mbinu ya kuwasha gar direct ile switch ya starter ikizimwa tu king'amuzi hakisomi muda huo gar imewashwa direct Sasa hapo ndo wanakimbia jins wanavyo taka
Unashangaa tu gari kwenye system imetoka dar had Moro inaonekana baada ya kufika Moro inapotea haionekan unakuja kuishtukia ipo iringa kumbe hapa katkat alizima switch kma vle gar imezimwa kumbe bado inamwaga moto
Ving'amuzi sahiv vmechezewa Sana ni kweny magar machache tu ndo vpo vzur
Huyo ndio m'bongo. Jiji halikosi solution
 
sasa katika mazingira haya ndio wayafatilie hayo mabus, likibainika wayachukulie hatua kali badala ya kuweka initiatives za kutesa abiria
Hatua kali wanazo chukuliwa ni pamoja na kukamatwa na kupelekwa mahakamani
Wanacho fanya madereva wakiona wamewahi sana wanapaki magar nnje kdogo ya mji ili kusubiri muda ndo waingie stand ili wasikamatwe kwahiyo kosa n la madereva kutembea mwendo ambao hauruhisiwi ukiona kapak nnje ya mji toa taarifa
 
Hatua kali wanazo chukuliwa ni pamoja na kukamatwa na kupelekwa mahakamani
Wanacho fanya madereva wakiona wamewahi sana wanapaki magar nnje kdogo ya mji ili kusubiri muda ndo waingie stand ili wasikamatwe kwahiyo kosa n la madereva kutembea mwendo ambao hauruhisiwi ukiona kapak nnje ya mji toa taarifa
kama unawafungia madereva na wengine wanaendelea kumwaga moto manake una deal na channel ambayo sio sahihi. Watu wa kudeal nao ni wanaomanage system, hawa madereva ni wahanga wa mwisho tu.. rules should be simple, gari imeviolate speed piga fines kama zilivyo, tajiri akikasirika yeye atamuwajibisha dereva wake.
 
kama unawafungia madereva na wengine wanaendelea kumwaga moto manake una deal na channel ambayo sio sahihi. Watu wa kudeal nao ni wanaomanage system, hawa madereva ni wahanga wa mwisho tu.. rules should be simple, gari imeviolate speed piga fines kama zilivyo, tajiri akikasirika yeye atamuwajibisha dereva wake.
Ndo dereva ili kukwepa faini anaamua akifika iringa anapaki gari nje ya mji inapita hata dakika 45 nzima mmesimama tu anasubiri muda ufike aende stand sasa ili kukwepa kero ya kusimama nje ya mji abiria watoe taarifa ili waje wapigwe faini ili siku nyingine kusiwepo na kero hiyo
 
Back
Top Bottom