Kero za kuajiriwa ...

Kero za kuajiriwa ...

ngoshwe

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2009
Posts
4,131
Reaction score
937
Nafanya kazi, laki tisa KITU NI mshahara wangu wa mwezi unasoma kwenye "salary slip" lakini kiasi nachoingiziwa benki ni laki nne na USHEE tu. Hii inatokana na makato kibao, nakatwa bima ya afya (27, 565.20) , malipo ya bodi ya mikopo ya vyuo vikuu (18,377.08), mfuko pensheni, (45,942) , mkopo mdogo niliokopa benki (ZAIDI YA 200,000). Kodi ya mapato (163,882).

Inaonekana kodi kwa kuajiriwa ni klubwa sana. Miaka fulani serikali ilifuta kodi ya kichwa na baadae ushuru kwa mazao ya kilimo ili kuwaondolea kero wakulima (wananchi). Lakini cha kusikitisha nchi hii kufanya kazi imekuwa kero, tupu, ukiwa unafanya kazi na wakati huo huo ni mkulima na mfanyabiashara nadahani utayaona maumivu ya hizi kodi.

Sisi tulioajiriwa hatulalamiki sana tunapokatwa " pay as you earn (paye)" ambayo wajanja wachache wanaitumia kuishi japo ilitarajiwa kuwasaidia wengi lakini bado hao wengi ndio imekuwa mzigo kwetu, tuna ishi nao majumbani tukitumia nao hicho hicho kidogo tunachopokea baada ya kukatwa !.

Kule ulaya na marekani, wale wanaoishi kwa kutegemea posho na uwezeshaji wa umma ( "ma-benefit" ) wengi wameamua ni heri wasifanye kazi kabisa ili waendeelee kuhudumiwa na serikali kuliko kufanya kazi halafu ukaishia kupokea mshahara kichele baada ya makatio kibao.

SINA HAKIKA KAMA HIVI VYAMA VYETU VYA WAFANYAKAZI VINAJUA MAJUKUMU YAKE VIZURI..SISI WANYONGE TUNAUMIA. NI HERI SERIKALI INGEAMUA KUANDIKISHA KILA FAMILIA NA KUJUA MAHITAJI YAO NA IKIWEZEKANA IKAANZISHA UTARATIBU WA KUZIHUDUMIA ZILE AMBAZO HAZINA UWEZO..UNAKUTA KATIKA FAMILIA NYINGI ZA KITANZANIA PENGINE MTU MMOJA TU NDIE ANAEFANYA KAZI LAKINI ANAWAJIBIKA KULISHA NA KUTOA HUDUMA ZA JAMIII KWA KAYA ZAIDI YA TATU ZENYE WATU WASIOPUNGUA KUMI KATIKA KILA KAYA (MTU MMOJA ANAHUDUMIA FAMILIA YAKE YA MKE/MUME NA WATOTO, ANAHUDUMIA PIA FAMILIYA YA WAZAZI WAKE, WAKWE ZAKE NA ANAWAJIBIKA PIA KUTOA MICHANGO YA MAENDELEO YA JAMII IKIWEMO HARUSI, NK...) HALI HII INAWAFANYA WATANZANIA WENGI WAISHI MAISHA MAFUPI KUTOKANA NA MARADHI YANAYOWAPATA WAKIWA BADO VIJANA....NA HATA WAKIENDA KUTAFUTA HUDUMA ZA AFYA, KILE WANACHOKATWA HAKIONEKANI KUPELEKWA HUKO ILI KIWASAIDIE KUWATIBU..
 
Kodi inaliwa na Kikwete katika safari zake, mnafikiri nani anafadhili Safari zake kama sio wewe kufanyakazi
 
Mtazamo wa maisha yetu watanzania unamatatizo makubwa, kwa umaskini wetu tutaendelea kuwa maskini mpaka tutakapobadilika.
Haiwezekekani mtu uwe na watoto 5 wakati huo unategemee ndugu wakusaidie, wakati unalipuwa unakula raha ukiwatafuta, hukuomba kusaidiwa matokeo yake ndio haya.
Watu wengi wamebebeshwa majukumu yasiyo yao, na hicho ndio chanzo cha matatizo yote.
Working class are paying so much in this country, na hao ambao unawasaidia wengi ndio wanaohongwa t-shirt na kofia na wafuja kodi zetu wa magamba.
in general working class are the most exploited people in this country kuliko hata wananchi wanaolala njaa, na wengi ndio wanataka mabadiliko, ila kinachoumiza ni unaowasaidia hawaelewi wapowapo tu na kuchukuliwa na malori kusikiliza uongo wa kina 6 na nape.
 
paye ni muhimu kwa kila nchi!ila hapa kwetu rate yake ipo juu sana!tupiganie jamaa wapunguze tax rate!
 
dawa ni kujiajiri

kuajiriwa nchi hii ni upumbavu saana

Mkuu, bado hata ukijiari kwa mfiumo wa maisha yetu ya kitanzania, huna guarantee ya kuendesha maisha. Hata wafanyabiashara ambao wameajiri wana machungu makubwa pengine unatakiwa ukiuke sheria na taratibu ili uweze kufanikisha ajira binafsi kwa mfano kukwepa kodi, kuwalipa mishahara midogo wale wanaokusaidia nk. Lakini kwa kuwa tunaishi katika mfumo wa kutegemeana kama kupe (mutually defendants), inakuwa vigumu pia kufanikiwa, inakupasa utokwe jasho la kutosha kulisha familia zetu za utegemezi wa mabehewa ya "TRENI"
 
Kuna haja ya kutazama upya mfumo wetu wa ajira; kweli wapo wanoumia sana na wapo pia walio peponi
 
Hizi kaya zisizo na ajira rasmi zinashindwa kujiongeza! Sisi wa vijijini huwa tuna was janga watu wa mjini. Wewe huna kazi wala pesa unaamua saa nne.

Mjini ukichemsha mihogo tu asubuhi hutakosa wateja.
 
Back
Top Bottom