Uchaguzi 2020 Keshokutwa tunapiga kura, tutangulize maslahi ya taifa

Uchaguzi 2020 Keshokutwa tunapiga kura, tutangulize maslahi ya taifa

dndagula

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2016
Posts
1,602
Reaction score
1,650
Wakati zimebaki siku mbili kupiga kura ninachukua fursa hii kuomba Watanzania wenzangu kujitokeza kwa wingi kwenda kutimiza wajibu wetu wa kitaifa. Tumesikia ajenda na ahadi za wagombea mbalimbali ni jukumu letu kupima na kufanya uamuzi ulio sahihi kwa kuangalia mahitaji ya nchi.

Maneno matamu yamesemwa lakini ni bora kuyatafakari kwa kina. Haya nayasema kama mzalendo kwa leo bila kumshawishi mtu aegemee upande fulani lakini watanzania ni watu wenye hekima na busara watachagua kulingana na mizania hususani ikizingatiwa kuwa sote tunapiga kura tukiwa na miaka si chini ya 18 umri wa mtu mzima mwenye maamuzi.

Aidha, tujiepushe na fujo na kuvunja Sheria za nchi wakati na baada ya uchaguzi. Na wataoshindwa wakubali matokeo na iwapo hawataridhika wafuate sheria za rufaa.

Kwa haya machache ninawatakia Uchaguzi mwema.

Mtumishi wa umma Mwandamizi Mstaafu.
 
Watanzania tujitokeze kwa wingi tukamuadabishe msaliti wa nchi kutoka Ubeligiji
 
NEC isimamie uchaguzi huru na haki kwa kutoa fomu za matokeo palepale kwenye kituo kujiepusha na kesi ya wizi wa kura kwa kukusudia na kusabisha kuvunja amani.
 
Kwa yale yanayoendelea Zanzibar, CCM fungeni virago muondoke ama mtaondoka kwa aibu.
 
Watanzania tujitokeze kwa wingi tukamuadabishe msaliti wa Nchi kutoka ubeligiji
Tutajitokeza kwa wingi kumuondoa muovu, muuaji na ambae anajihisi baada ya mungu anafuata yeye, ameiaibisha sana taasisi ya uraisi hafai kamwe apigwe vita kwa nguvu zote,. Man from tocha.
 
Tumefunga Kampeni Zanzibar kwa kaswida Muruwaa

 
Back
Top Bottom