Kesi ndogo ya Freeman Mbowe: Shahidi akamilisha ushahidi wake, Shahidi mwingine kuendelea tarehe 12/11/2021

hii kitu hachomoki walahi!!! Kama timu kibatala imeanza kuishiwa pumzi Basi jamaa hachomoki kwa hii kitu!!
 
Huyu afande Jumanne Malangahe kweli ni MWONGO sana...

Yaani mji wa Moshi ambao hauna foleni za magari kutoka KCMC kwenda Rau Madukani walitumia dakika 45...!!!!!?????

Duuh, ama kweli njia ya mwongo ni fupi sana...

Kwa wasioifahamu Moshi Manispaa, umbali wa kutoka KCMC hadi Rau Madukani, kwa DSM tunaweza kulinganisha na umbali wa kama kutoka Buguruni kwenda Shule ya Uhuru....!!

Sasa hapo kwa gari na tena ni sehemu isiyo na msongamano unaweza kutumia dkk 45 kweli?? Labda uwe unasukuma gari kwa mikono...!!!

Yaani huu ni uthibitisho tosha kuwa hii kesi in UONGO uliotengenezwa na watu tu waliokuwa wamekaa ofisini kwa kusukumwa na NIA OVU nyuma yake...
 
Mh,kazi kwelikweli,kesi hii itaingia kwenye rekodi za Karne hii Kama kesi ya kubambika aliyoandaliwa kizembe na watu wasio kuwa na ueledi wa kutosha kubambikia watu kesi😆😆😆 tuanzishe kozi maalumu watu wasome 😜😜
 
Police wanaajiriwa kwa mbio na urefu ndiyo kipimo cha interviews
 
Alijitahidi sana kukwepa kutaja muda sababu alijua atajichanganya na wale wenzake walishakwisha kutoa ushahidi.
Ushahidi wa kuchonga ni lazima wotw muwe makini saana msiende nje ya script..
 
Yaani wafuasi wa Mbowe wao wanacho taka kuona mara zote kuwa Jaji anaamua jinsi wao wanavyo taka, kinyume cha hapo, wataanzisha matusi na kejeli.

Hiii inathibitisha wazi jinsi walivyo funzwa na kiongozi wao tabia za kihalifu na wamekomaa.
Kichwa maji
 
hii kitu hachomoki walahi!!! Kama timu kibatala imeanza kuishiwa pumzi Basi jamaa hachomoki kwa hii kitu!!
Wamesha create reasonable doubt, mshitakiwa hakupekekwa kwa mlinzi wa amani na hakuthibitisha kukiri kwa maandishi,,
Hivyo kukiri kwake ni irrelevant im material,
Huwezi kutumia bastora yenye risasi tatu kulipua visima vya mafuta across country,, at least unahitaji baruti[emoji23].
Hamna kesi hapo
 
hii kitu hachomoki walahi!!! Kama timu kibatala imeanza kuishiwa pumzi Basi jamaa hachomoki kwa hii kitu!!
Mungu ni wetu sote.Huwezi Amini Kabla ya MBOWE kufungwa Kuna kitu kinaweza kukutokea.Magufuli alitamani sana TUNDU LISSU afe haraka.Magufuli alikuwa zaidi yako alitamani kuona MBOWE anafungwa Maisha.Ukweli huu Magufuli alifariki kabla hayo hayajatokea.Mungu Ni waajabu Sana.Nilimwambia hayo ndugu yako jingalao akapuuza sasa hivi mateso anayo yapitia Ni zaidi ya MBOWE..!MBOWE atafungwa na hii ndiyo furaha na ushindi wa CCM ,familia yako Utapata kinga ya magonjwa MBOWE akifungwa,Familia atachana na umasikini MBOWE akifungwa.Ndugu zako wote hatakufa tena MBOWE akifungwa.Furahi na Kushangilia Kwani MBOWE atafungwa soon
 
ubambikiaji wakati mzee mboe alikuwa anapanga mikakati ya kuvuruga amani ya nchi, kisa uchu wa madaraka, sasa ngoja akawe mnyampara.
Umekazana kuita mboe ndio nani huyo? Au unashindwa kuandika vizuri kutokana na kukosa elimu na kuwa na matamanio yako yaliyopitiliza?
Angalia utakalia mpini bwege we!
 

Tatizo mnajiona wote ni wanasheria kweli zuzu ni zuzu tu
 
Hii kesi nashauri Rais Samia aongee na mwana sheria wake aiondoe tu ili Serikali yake iendelee kuheshimiwa.
Sababu moja kuu
Rais Samia hii kesi kaikuta mezani.
Waliopanda asilimia kubwa hawapo ofisini au duniani.
Samia aitumie kesi kujijengea heshima mbele ya jamuia ya kimataifa.
 
Magu alipiga push ups kwa kumkejeli Lowassa. Alijiona ni mzima na mwenye kinga. Alimuona Lowassa ni mgonjwa na kifo kinamnyemelea. Aah wapi Mungu ni Mkubwa kuliko awae yote ktk dunia hii.
 
Yaani Askari Mzima Kwa Anakiri Kuwa Kesi Ya Ugaidi ni Kesi Kubwa, Lakini Anasema Hakuona Umuhimu wa kutumia Audio recording au video kumuhoji Mtuhumiwa [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28] Angeuwawa Huko Ndani? Hivi hawa Askari wetu Hata Movie Tuu hawaangalii?

Askari amefanya kazi Dar es Salaam lakini kuna vituo Vya Polisi Havijui?

Askari amehamisha Mahabusu kuepuka mchanganyiko na Taarifa kuvuja, lakini hajui kama watuhumiwa walikuwa Isolated au laaa, sasa ulihamisha Wa Nini?
 
leo mmefurahi eeeh...
sasa ikitokea siku nyingine mmekataliwa muwe na heshima na adbu.
acheni matusi, ukorofi na kejeli, hivyo hivito msaidia mzee wenu mboe.

Ndezi, hujajua madhara ya nyaraka kukataliwa mahakamani! Usichojua ni kuwa kazi ya utetezi sio kuonesha Mbowe na wenzie hawakufanya makosa wanayoshtakiwa nayo bali kuweka shaka katika mashitaka. Kama jaji ataamua kwa msingi wa “ushahidi usiokuwa na mashaka” basi washitakiwa wataachiwa huru!!

Mashaka yaliyowekwa sasa hivi ni namna nyaraka hii ilivopatikana wakati ilikuwa mahakamani! Je mahakama inawasiliana na waleta mashitaka against washitakiwa?? Usione jaji ni mjinga, wala usione ni ushindi kwa Chadema. Jaji kaamua kuikataa document ambayo mbeleni angeulizwa waleta mashtaka wameipataje bila maombi!!

Ndezi kama wewe mnaagaliaga mtu alipoangukia, badala ya kwanini ameanguka!
 
Kwani mmesahau kuwa Mh SSH alikuwepo kwenye Serikali ya mwendazake, na kwamba haya mambo yalisukwa miezi ya July/August cho2020?
Lakini mama aliingia kwa ahadi kuwa hataki kuona kesi kubambikia watu.
Kilichokuja kuvuruga haya masuala/kesi hii ni pale mkuu wa jeshi la polis IGP alipoongea na chombo kimoja cha habari cha Dakika 45 aliposema Mbowe ni mhalifu hata kabla mahakama haijamhukumu.
Mbaya zaidi tena pale Rais wetu alipoitangazia dunia kupitia chombo kimoja cha habari cha kimataifa kwamba Mbowe ana kesi ya kujibu (inawezekana Mh Rais wetu hakupewa taarifa sahihi kutoka kwa wasaidizi wake juu ya dual/kesi hii). Matamko ya viongozi hawa, kwa maoni yangu yanaathiri sana mwenendo wa kesi hii.
Kwa maoni yangu, DPP ndiye mtu sahihi anayeweza kuokoa jahazi kwa kuifuta/kuiondoa kesi hii mahakamani kwa MASLAHI mapana ya Taifa.
 

Umeona udhaifu wa shahidi vizuri kabisa. Anaulizwa kwanini baada ya kukiri makosa yake hawakumpeleka kwa mlinzi wa amani. Anajibu: hatukutaka kupoteza muda tulikuwa tunataka kuhakikisha ugaidi hautokei. Anasahau hata shahidi mwenzake aliulizwa kama kuna taarifa zozote kwa wakuu wa polisi wa maeneo lengwa, jibu hakuna. Kama walengwa (Sabaya) walifahamishwa kuhusu kutafutwa kwao kutendwa ubaya, hapana. Kama walitoa taarifa kwa kamati za usalama za wilaya au mkoa, hapana. Sasa sijui ni hawa watu wanne tu walikuwa na jukumu la kuzuia ugaidi nchi nzima???

Tuna polisi wa ajabu sana. Na bahati mbaya huyu shahidi nae amesimamishwa kazi kwa kubambikizia mtu kesi!!
 
hii kitu hachomoki walahi!!! Kama timu kibatala imeanza kuishiwa pumzi Basi jamaa hachomoki kwa hii kitu!!
Mnakichafua chama na serikali kwa michango kama hii. Kitu hakifurahishi wewe unashangilia. Wenzako wanafuatilia kwa umakini, wapo kimya, wewe unafanya unafiki. Mbaya sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…