Kesi nyingi za wanandoa ni kupangiana au kunyima unyumba

Kesi nyingi za wanandoa ni kupangiana au kunyima unyumba

chizcom

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2016
Posts
8,680
Reaction score
18,035
Ni aibu sana au kukuta mtu jasiri akitamka kuwa mizozo na kushindwa kuelewa ni unyumba.

Shida hii inaweza kuwa kwa mwanaume au mwanake kila mtu kuwa na sababu zake mfano utafutaji,kukosekana kwa ubunifu,kupungua kwa mapenzi,kuzoeana na kujuana sana kabla mjaingia kwenye ndoa.

Sababu zengine zinapelekea mpaka wengine kuchepuka nayo ni moja ya kupima mwenza wake kifedha,uwezo,ubunifu,kupungua kwa mapenzi na n.k

Ili tukiweka ukweli tuwe tuna washauri ambao wanaingia kwenye ndoa kupeana tu kama uzamini wa GSM na vilabu vyote kupangiwa matokeo.
 
Hilo ni tokeo la migogoro mingine ndani ya ndoa na hatimaye linazaa hili la kunyimana unyumba. Mfano kama kuna ugomvi unaotokana na mmoja kati ya wanandoa wa ku- cheat, ni dhahiri itasababisha wanandoa kutoshiriki tendo.
 
Nakuchokana pia kunachangia..mtu unaamua kupiga kamoja Tena kwakujilazimisha
 
Familia ya mume kuleta migogoro ndani ya ndoa, inapelekea mke kujawa na stress kushuka kwa peformance ndani.
Ulevi kupindukia inapelekea kutojali familia.
Mume kusikiliza ndugu zake badala ya mke.
Usiri wa kufanya mambo peke yako kunapunguza imani ndani.
Aaaah yanachangia kunyimana unyumba.
 
Nyuma ya kupangiana unyumba kuna kukosa hisia
Palipokosekana hisia kuna kukosekana kwa mapenzi and it keep going.. So hiyo ni immediate course.
 
Eehehehe wacha ncheke kwanza.....

Patq picha wanandoa wote ni waumini wa dini moja na wanashiriki vizuri ibadani.
Ghafla mmoja wa wanandoa anapitia changamoto kazini na anafukuzwa kazi. Anajaribu kutafuta kazi nyingine hapati, kila akijiajiri hola anaambulia hasara.
Anakutana na rafiki anamwambia ampeleke kwa fundi(mganga) sio bure amechezewa...
Wanapanga mipqngo yote ana anaweka imani atafanikiwa akitoka huko.

Wanandoa hawa hawajawahi kushiriki wala kiwa na imani na waganga wala ushirikina. Anarudi anamwambia mwenza wake kuhusu kwendq kwa mganga, mwenza wake hakubaliani na hilo wanakosana na anamwambia nenda ila mimi sijaafiki na usinihusishe na hiyo ibada sitaki kushiriki.

Jamaa anaenda kwa mganga anarudi na marundo ya dawa za kienyeji, sijui ya kunywa, ya kuoga, ya kupaka, yakutafuna basi tafrani. Mwenzake anamwambia tenga vyombo utavyotumia na madawa yako sitaki watoto washiriki kwa namna yeyote ile.
Jamaa anakuwa kiburi anataka mke amchemshie dawa zake eehehehe mke anamwambia sishiriki ibada za sanamu nilishakwambia ukitaka mwambie dada akutengenezee... mzozo ila mwanaume anakaza kichwa anaendelea na dawa zake.

Eehehehee usiku mwanaume anataka unyumba, mwanamke anamwambia umetoka kufanyiwa madawa na mengine unaendelea kunywa na kujipaka tafadhali maliza madawa yako ndo tuendelee sitaki kujihusisha na hizo ibada, nikishiriki tendo na wewe nakuwa nimeunga nafis yako na yangu kwenye hizo ibada tafadhali naomba umalize matibabu yako utanikuta nakusubiri.

Mwanaume anasema siwezi kusubiri wiki mbili, maana dawa anatumia kwa wiki mbili. Hapo unafikiri kunyima unyumba ni kosa ama ndo migogoro ya ndoa....


Bado hujakutana na mwanaume ametoka kunywa wanzuki yuko tip amelewa na amejikojolea anafanikiwa kurudi nyumbani anadai unyumba, tena kwa kelele... weee mama sikununu, panda juu uchezee koki hiyoo..... huku anapiga kwikwi.... mwanamke anatoa msonyoo wa kinaijeria halafu anajifunika tenge lake analala...
Je hii nayo ni migogoro ya ndoa?
Au ndo ile inasemwa kwa shida na raha?

#kataa ndoa mpoo...!!??

All in all, hakuna mwanadamu aliyekamilika ikiwemo mimi na wewe. Wote tunachukuluana na wengine wanashida ya akili ila sababu wanapata nyege huwezi kiwazuia kupata wenza, itakuwa ni ukatili wa hisia.

Alnuru,

Kasinde Mahaba 😉.
 
Back
Top Bottom