Kesi ya Abdallah Zombe: Mashitaka, hatia, hukumu na yanayojiri

Zombe aelemewa Mahakamani

*Mashahidi 50 kueleza alivyoua

Na Grace Michael

 
Ushahidi kesi ya Zombe watisha

na Asha Bani

 
Kesi ya Zombe: Shahidi: Askari wa kike aling'ang'ania fuko la pesa

 
Zombe atoa kioja kortini

* Anukuu Biblia, adai wakili amefuata posho

Na Grace Michael

 
"Mtukufu Jaji hapa Katiba inatakiwa itumike ili kufikia haki kwani ni marufuku kumkamata mtu kinyume cha sheria, kitendo cha DPP na Polisi kunileta hapa mahakamani sikielewi kabisa, kushitakiwa kwangu ni kwa chuki za watu binafsi !" Alilalamika.

Huku akiendelea kulalamika, Bw. Zombe alinukuu vifungu mbalimbali vya Katiba ya nchi na mstari wa Biblia kutoka Kitabu cha Yohana 7:51 unaosema "Usimhukumu mtu bila kumsikiliza na ibara ya 13 na 15 ya Katiba.

source; http://majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=6833

naam huku kesi ikieendelea bw zaombe anaonekana kutaka watu tuamini kuwa kesi dhidi yake ni chuki tu.

kama ni chuki iwe juu ya nn? na watu gani? au wenyewe huko wamedhulumiana na kumtoa kafara?
 
Hapa mkuu kuna kitu.......yeye alishika bunduki aliwaua hao jamaa??au alitoa amri ya kuuawa kwa hawa jamaa?
 
hii kesi jamani mbona mie nashangaaa huku iko on de low profile??!as natamani sana kujua ukweli wa mambo as sikwepo huko wakati yatokea na basi hata hizo tetesi sina...guys jamani wa huko ufisadini tupeni more mamboz basi on this case
 
senx alot mtoa habari yaan guys kip on up2date us more on this kesi as nasikia itakua yasomwa kila day sina uhakika abt weekends si mwajua tena JF ndo kama gazeti kwa wengine?kila siku yabidi ujipatie nakala yako...actually kila majira as asubuhi mchana na jioni bila kusahau usiku
 
Zombe asitake kudanganya watu. Tunamjua vizuri...Huyu ni mtu ambaye alikuwa anatumia vijana wake kunyanyasa wafanyabiashara mbalimbali na kuwapora hela zao.

Ilikuwa ngumu kuprove case nyingi lakini Mungu si Athumani akajilengesha...
 
Mtu ambaye hakuwahi kufika mikononi mwa zombe na kundi lote lile atasema zombe anaonewa lakini kama uliwahi kufika mikononi mwa zombe na kundi lake hasa yule mwanamama Jane anajua wale marehemu walipitia wakati gani.

Kipindi kile nchi ilikuwa imeoza kwani polisi ndo walikuwa majambazi, mchana mkiona TZR imepita jioni jiandaeni kwani wanasurvey na kurudi usiku, walikuwa wanaiba mtaa kwa kufuata mfulilizo wan nyumba zilivyojipanga leo wakiishia hapa kesho wanaanzia hapo kama hawajapumzika kwa wiki moja.
 
kesi hii imeamsha hisia kali sana za wana jamii hasa waliowahi kupata kipigo na mateso makalitoka kwa bw Zombe....jamani huyu baba alikuwa jasiri na katili hasa....majambazi walikuwa wanamhara sana huyu bw...ila hata...wanyonge alikuwa anawakandamiza maana alizoea sana kudaka...cha juu....hata kwa kuwakandamiza wanyonge.....alizoea sana rushwa kubwa kubwa........na ubabe...time itatuambiaa.....
 
mkuki kwa Nguruwe kwa binadamu mchungu!yeye kucheleweshwa tu anaona soo!na alivyowatoa innocent people uhai wao!hata nafasi ya kujieleza hakuwapa!na hadi leo yale madini waliyokuwa nayo hayajulikani yalipo!Na bado.Cha kushangaza anakoti mistari ya bible si mchezo leo anajua kuwa kuna MUNGU?
 
wewe jaji jamani mbona hivyo si MHKUMU KIFO HUYO JAMANI MNAWAPOTEZEA MUDA WA NINI WANANCHI KUHANGAIKA MAHAKAMANI KILA SIKU JAMANI ADHABU IKO WAZI
CHINJA HUYO JAMANI....NYIE MAJAJI MBONA HIVYOOOOOOOO HUYO MUUWAJI NJE NJE CHINJA HUYO MPELEKENI DODOMA AKFIE UKO AONE UCHHUNGU WAKE NA HII NI KWA TAARIFA YENU TU....WALE WATU WALIPELEKWA SEHEEMU KULE MBEZI YULE ASKARI WA KIKE AKAWATUPIA MADINI KWA MBELE HUKU AMEWAFUNGA MIKONO AKASEMA NENDENI MKAOOKOTE MADINI WAKATI WANAYAFYATA WAKAJUA WAMEACHIWA MASKINI WAKASIKIA BASTOLA NYUMA YAO OOOHHHH MA GOD ....MAHITA HAWA WATU ULIKUWA UKIWALINDA KWASABABU YA TEN PEC ZA MAJAMBAZI UNAONA WANAKUAIBISHA MASIHARA USISHANGAE KUJA HUMO NDANI S
 
kwa jinsi alivyodata inaonyesha kuwa jamaa anaamini kuwa atashinda kesi au kuna uwezekano wa kutoka.Miezi hiyo kidogo aliyokaa korokoroni bado ana picha ya Tanzania aliyoiacha, angejua kuwa Tz na Watz wamebadilika sana ktk kipindi kifupi cha miezi michache aliyokaa ndani asingetoa malalamiko ya kibwege hivyo. Jamaa hajui kuwa hata BWM naye huenda wakakutana huko huko kwa pilato !!!!!!!
 
 


mkuu anaonesha jinsi alivyokuwa akitekeleza kazi zake.


ukimuangalia tu utajua hili ni jambazi
 
Zombe hizi sheria na maonevu ameanza kutajua lini ? Je wale waliokuwa anawakamata na kuwatesa wakati ule hakuwa anajua Katiba ama ndiyo madaraka tena ?
 
Niliposoma maelezo ya yule shahidi wa kwanza kwenye kesi ya Zombe basi nikajua kweli hawa jamaa nao walikuwa ni victims wa uhuni roho mbaya aliyokuwa nayo Zombe.

Kila kitu alichoelezea kilichowapata marehemu hao ni kama ambao yalishawahi kunipata mimi kwa amri za aina hiyo hiyo za Zombe.

Nilikuwa Post Office Moshi siku hiyo sitakaa nisahau.
Kuna mtu nilikuwa nimempa ride na mimi nilikuwa nimebaki kwenye gari nikimsubiri jamaa yangu huku nikila mziki laini ndani ya gari lenye namba za kigeni za SA.

Wakati bado nikiwa ndani ya gari mawazo yangu yakiwa mbali ghafla nikaona gari (through side mirror) Ghafla lime block nyuma yangu.

Gari aina ya defender ikiwa na maaskari wengine kanzu na wenye mavazi yao ya kipolisi huku waiwa na misilaa kama vile ni raid flani hivi ya majambazi.

Maajabu ni kwamba nilikuwa nikiwafahamu zaidi ya wawili ama watatu wa hao maaskari kanzu.

Ghafla mmoja wao akaingiza mkono na kuchomoa funguo za gari...Na kufungua mlango huku wakiniamrisha kushuka kutoka kwenye gari.

Nikamwambia mmoja wa wale niliokuwa nikiwafahamu..Ni nini tena ndugu yangu kuvamiana kama majambazi?

Yeye mwenyewe alikuwa akinieleza kwa masikitiko kuwa ni amri kutoka kwa Zombe.

Baada ya jamaa yangu naye kurudi kutoka Posta...Tukajumuishwa wote ndani ya gari na mmoja wa wale waliovalia kiraia akawa ndiye mwendeshajiwa gari lile nilolokuwa nalo...Baada ya kufikishwa kituoni ndio nikakutana na Zombe mwenyewe kwa mara ya kwanza!
Na ndugu zangu story ya shahidi yule ni kama yale yaliyonipata hivyo hivyo..Amri ilitoka kwa Zombe aliyekuwa upastairs ofisini kwake na kufoka walete wa*** huku juu.

Vitisho kama alivyosema yule bwana ni the same..Tofauti ni kwamba hakuwa na bunduki kama yule shahidi mwingine alivyokuwa akisema..Bali alikuwa na kamera...Na bastola moja ikiwa mezani nahuku akivuta midroo yake kwa vurugu nyingi..Na kuikamata bastola yake mara kwa mara..Huku tukiwa tumekalishwa chini ofisini kwake kama vile tayari sisi ni majambazi ama vibaka!

Huku akiongea kwa vitisho na mara nyingine kejeli..Huku akitupiga mipicha ya kila namna na kudai kuwa sisi ni majambazi na huku akitisha kutukanyaga usoni!

Jamaa yangu alikuwa akifikiri ni kama masikhara vile akatabasam...Jamaa akamtukana matusi ya nguoni na huku akisema jambazi mkubwa we na maneno kede kede.
Baada ya vitisho na unyanyasaji mwingi ndio tukapelekwa chini lock up kusubiri wadhamini.
Huyu bwana kusema kweli alikuwa anajuwa kabisa kuwa wale watu walikuwa innocent!

Na mimi huwezi kujuwa labda ni Mungu alisaidia kukawa na maafisa wengine waliokuwa wakijuwa kabisa kuwa amri ya bosi wao ilikuwa na walakini kwani mimi si jambazi na wao walikuwa wakifahamu kuhusu gari hilo.
Huu unyanyasaji wake naona umefikia kikomo na ni malipo ya Mungu kwa unyama wote aliwahi kuufanya dhidi ya raia wema huku akiwalinda majambazi!

Yeye ndiye mmojawapo aliyekuwa akitoa amri za kuwanyanyasa raia huku ujambazi ukishamiri akiwa in charge wa upelelezi.
Mabilioni waliyojivunia wakiwa na kina Mahita ni mtandao wa kigaidi uliokuwa ukiwalenga raia wema specifically na kuwa wasindikizaji wa majambazi kwenye matukio yao ya uamabazi!
Wewe unaweza kuona polisi wametokea ukadhani kuwa ni msaada ukaja ukashangaa wanakumalizia wao wenyewe!
Na hayo ndiyo yaliyotokea kwenye kesi hii ya Zombe!
Na asijidahi kuongea maneno ya dini sasa hivi!
Labda atakuwa amegeuka na kuwa mlokole akiwa huko jela...Kitu ambacho mke wake ambaye ni mlokole alikuwa akimlimlilia sana afanye hivyo !

Ama kweli Mungu si Zombe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…