Kesi ya Abdallah Zombe: Mashitaka, hatia, hukumu na yanayojiri

hivi huu ulokole mpaka uwe kizimbani ya Rama mla vichwa haya
 
Huyu jamaa katolewa kafara kama funzo kwa wengine. Hakuna aliye juu ya sheria. Jana nilifanikiwa kutembelea kituo kimoja cha polisi, na nikashuhudia jinsi gani hii kesi ya Zombe imewapa polisi utu na adabu. Polisi hawapigi tena watuhumiwa. Wanaogopa kufanywa kama Zombe.
 
Huyu mpuuzi kabisa ulokole haupate wapi, imefika zamu yake kulipa anaangaika tulia unyolewe kamaulivyowanyoa wengine na kuwafunga kwa kesi za kumbikiwa wakati hawana hatia, utakutana nao jela ndo ujue kuwa ulimwengu una sura mbili kama shilingi.

M/mungu siku hizi mkali sana naona kaamua kuacha kusubiri siku ya kiama kaamua kuwadhibu wakosaji hapahapa ulimwenguni.
 
Nilikuwa Post Office Moshi siku hiyo sitakaa nisahau.
Kuna mtu nilikuwa nimempa ride na mimi nilikuwa nimebaki kwenye gari nikimsubiri jamaa yangu huku nikila mziki laini ndani ya gari lenye namba za kigeni za SA.



Muziki ulipotoka Moshi ulihamia Tanga, Mavuno yakawa madogo bosi naye hakuridhika na uchaguzi ulikuwa karibu na umri wa kustaafu pia ulikuwa karibu, hivyo Bosi akaamua amsogeze kipenzi ili watengeneze fastafasta na kweli mambo ikawa kila siku majambazi yameuwawa na polisi. Bosi akastaafu lakini jamaa akasahau kuwa aliyekuwa anamkingia kifua hayuko tena madarakani, hayo ndio mazoea ya mafisadi wengi hujisahau kuangalia na kusoma alama za nyakati (Pole sana bwana Mushi, lakini pale Dar es salaam streat hukunywa bia zake wakati akimlambia alhaji wa visiwani?)
 

Pole sana kwa yaliyokupata. Wengi tunaamini kwamba malipo ya dhambi huwa ni hapa hapa duniani, na wala sio mpaka ufe ufike huko jehanamu. Natamani kusikia wamemgeuza bibi huko jela.
 

Pole sana Mushi. This was the kind of law enforcers we used to have by that time na wengi sana wameumia katika mikono yao. nadhani idadi ya watu waliouawa na majambazi, inakaribia kulingana na waliouawa mikononi mwa polisi. lakini kama alivyosema mmoja hapo juu, Mungu si Zombe na siku zote mtu hupata malipo ya matendo yake, kama si hapahapa duniani, basi mbele ya Allah.
Aliyoyafanya Zombe yanafahamika lakini yeye mwenyewe anayafahamu vizuri sana kuliko mtu mwingine. Ingekuwa vema kwake iwapo angeamua kutubu sasa na kumgeukia Mungu, kuendelea kuonyesha kiburi ni kujiongezea mzigo ambao hatoweza kuubeba mbele ya haki.
Pole Mushi, lakini ninaamini kuwa maisha yanaendelea kwako kama kawaida, hata kama hautasahau ya Zombe, msamehe na wewe utapata baraka zako
 
Mungu ana hekima za ajabu ambazo hatuwezi kuzicgunguza....

Fisi kung'oka jino kwa kutafuna nyama si jambo la kawaida....

Haya zombe ngoma iko ngumu sasa na roho ulizoamrisha zitolewe zimekushtaki kwa Mungu zinakulilia.... Mi simo
 
Yaani ukinitajia jina la Zombe najisikia kichefua - chefua! tena ingekuwa kunauwezakano hukumu ya kesi yake ingesomwa hata leo hii, ale miaka yake

Na hilo lililokuwa likubwa lao (Mahita) hili jamaa lilikuwa na vijana wa kazi waliokuwa wakiendesha shughuli za uporaji wa madini na pesa, wahindi wawatu wafanya biashara ya tanzannite mkoani Arusha walikiona cha moto.

Kosa walililofanya ni kumpeleka Bwana Kombe kuwa RPC Arusha, Mzee Wakimarangu alikwenda akaufyeka mtandao mzima, Ujambazi ukaisha. Walivyogundua kumbe wamempa machapakazi anawaramba mpaka vijana wao akaondolewa na kupelekwa makao makuu - Dar kwenda kuwa kamanda wa Kikosi cha usalama Barabarani.

Kombe alipoingia Arusha akatangaza, jamani sasa kazi kila mtu atakuwa salama pamoja na mali zake, hatutamwangalia mtu,Hawa vijana wa kazi kwenye vikao vyao wakajibu mapigo kwa kusema, hatuongei na mbwa tunaongea na mwenye mbwa.(hawaongei na RPC wanaongea na IGP)

Kombe akasema, anaapa kama hatawamaliza basi yeye anarudi zake moshi kulima mgomba na kazi ya upolisi haimfai.

Mahita..Zombe.. yote mijambazi
 
loh pole sana jmushi kwa mkasa wako...sasa wajimini naomba kuuliza hivi huko bongo sasa siku hizi nani wa kuaminika??maana viongozi full of ufisadi,polisi nao ndo ka hivi,sheria ni pwesa yako tuu,hospitalini nasikia nako ni mijihelaa tuu yatakiwa mwee balaah!
 
Halafu anali lia pale ushahidi unapotolewa na details zote za ugaidi wake zinapowekwa hadharani.

Hii ni kwasabab ushahidi unamwumiza roho kwasababu ni ukweli!
Halafu anajisahahu kama Saddam na kuanza kubwatuka kama vile alivyokuwa akifanya wakati akitoa amri zake za kijambazi na kigaidi dhidi ya innocent citizens.

Naomba waendesha mashtaka wasikubali intimidation zake na wa take tieir time wakati wa kesi hii na kumkaanga vizuri mpaka aive na kuelewa nini maana ya kunyanyaswa kwani malipo huanzia kwenye kusutwa,ukweli kuwekwa wazi,ujambazi wake kuainishwa pamoja na yeye kuwa embarassed na uchungu wa maelezo ya kesi na mashahidi halafu then huendelea pale anapokuwa sentenced hadi pale anapomalizia adhabu yake.
 
kuna forums fulani wanasema kuwa ZOMBE kafa
je kuna yeyote kwenye ukweli wa hili?
 

by the way,Chico yuko wapi naye siku hizi?
 
Jamani Wakulu Taratibuni, Forum Gani Umesikia Nnaamini Si Jf
 
kuna forums fulani wanasema kuwa ZOMBE kafa
je kuna yeyote kwenye ukweli wa hili?

Ukweli Zombe hajafa, labda kama ni Breaking News!
Zombe anaendelea na kesi yake....
"Katika kesi hiyo itakayosikilizwa na Jaji Kiongozi Salum Massati kwa siku 13 mfululizo, upande wa mashitaka unategemea kuita mashahidi zaidi ya 50 na kuwasilisha vielelezo kadhaa vya kuthibitisha makosa dhidi ya washitakiwa"

kwa hiyo hata leo Zombe yuko Mahakamani...sasa hili la kufa limetokea lini?
 
Kesi ya mauaji ya wafanyabiashara, polisi adai aliamriwa abadilishe taarifa
* Ni kuhusu silaha zilizotumika kwa wafanyabiashara wa Mahenge
* Adai alishinikizwa kutoa bunduki na risasi zikapigwe porini

James Magai na Nora Damian

 
hii nayo siasa ? muone kwanza !

Kada
Hii si siasa ila ni habari mkuu .Unaweza kusoma na kupita si lazima uonyeshe upumbavu wako .Hii inaweza kuwa siasa in a way yes .Kwa nini JK hawakamati mafisadi kakazana huyu pekee ? Kweli aliua lakini wako mafisadi wanao tuua taratibu na tutakufa .Inaweza kuwa siasa kwa kuwa imepewa uzito mkubwa hadi mawakili wa kujitegemea kuendesha kesi , je wangapi DPP kawapa kibali cha kuwatumia mawakili wa kujitegemea? All in all nilikuwa natoa tu habari kama vile juzi ilitolewa hapa akisema anaonewa huyu Zombe huja question why leo ukurupukie hapa ?
 

inaelekea una stress kichizi lunyungu..............

umetoa mada inayohusu wafungwa, then ukasema

(a)kada mpumbavu
(b)jk hakamati mafisadi

issues a and b hazihusiani kabisa na mada yako, second...nakushauri ukasome ile mada ya mwanakijiji ya tumewaudhi maana naona na wewe pia inakuhusu. Yaani umeudhika kupita kiasi, sababu ? sijui.. pole mzee na stress !

zaidi ya yote, umekiri kwamba hiyo sio siasa, na unafahamu fika kwamba hii ni seksheni ya siasa, lakini still umekuwa ignorant kupita kiasi na kupenyeza "habari" yako kwenye siasa....huu sasa nao pia ni UFISADI !! inafaa ukamatwe !!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…