Kesi ya akina Slaa kusikilizwa Januari

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
Kesi ya akina Slaa kusikilizwa Januari

Imeandikwa na John Mhala, Arusha; Tarehe: 21st December 2011 @ 12:00 Imesomwa na watu: 54; Jumla ya maoni: 0


[TABLE="align: right"]
[TR]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][TABLE="align: right"]
[TR]

[/TR]
[TR]

[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]
[TABLE="align: right"]
[TR]
[/TR]
[TR]
[TD="class: Marquee"]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
USHAHIDI wa kesi inayomkabili Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willbroad Slaa na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu pamoja na wafuasi 26 wa chama hicho walioshitakiwa kwa ajili ya mkusanyiko usio halali na kutoa lugha ya uchochezi, umekamilika na kesi hiyo itaanza kusikilizwa Januari 23, mwakani.

Wanadaiwa kutenda kosa hilo katika Jiji la Arusha katika Viwanja vya NMC Novemba 7 na 8, mwaka huu.

Akizungumza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, mbele ya Hakimu Devotha Kamuzora, Wakili wa Serikali, Ellen Rwijage alidai upande wa mashitaka uchunguzi umekamilika na kuomba kupangwa kwa usikilizwaji wa awali.

Pia wakili huyo aliomba Mahakama hiyo itoe amri ya kumtaka Lissu, kuja na vielelezo vya kuonesha kama alikuwa mgonjwa na kiasi cha kushindwa kuhudhuria mahakamani jana.

“Mheshimiwa pamoja mdhamini wake Calistus Lazaro, amekuja hapa kusema amepigiwa simu, lakini bado tunaomba Mahakama yako imwagize huyu mshitakiwa aje na kithibitisho siku ya kesi itakapopangwa ya kuonesha alikuwa mgonjwa Desemba 21 mwaka huu,” alisema Rwijage.

Akijibu ombi hilo, Hakimu Kamuzora, alisema mshitakiwa siku ya kesi afike na kielelezo cha kuonesha ni mgonjwa na pia itaanza usikilizwaji wa awali Januari 23, mwakani.
 
badala ya kulijenga taifa tunahangaika na migogoro uchwara.......
 
serikali iliyopoteza muelekeo ndo dalili zake hizo.huwa siku zote wana deal kwa nguvu zote na mambo yasiyo na tija kama haya
 

Lissu hakufika, Slaa alifika?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…