Pre GE2025 Kesi ya Dkt. Slaa imeahirishwa mpaka Februari 18, 2025

Pre GE2025 Kesi ya Dkt. Slaa imeahirishwa mpaka Februari 18, 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Kesi ya kusambaza taarifa za uongo kwenye Mtandao wa X inayomkabili wanasiasa mkongwe nchini, Dkt. Willibrod Slaa (76) itatajwa leo Februari 6, 2025 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.

1738822421320.png
Dk Slaa anadaiwa kutenda kosa hilo chini ya kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao namba 14 ya mwaka 2015.

Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Beda Nyaki na imeitwa leo Alhamisi, Februari 6, 2025 kwa ajili ya kutajwa na kuangalia iwapo upelelezi wake umekamilika.


Updates...
Kesi Namba 993/2025 inayomkabili Mwanasiasa mkongwe, Dkt. Willbroad Slaa (76), inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Beda Nyaki, imeahirishwa mpaka Februari 18, 2025 ambapo iliitwa kwa ajili ya kutajwa na kuangalia iwapo upelelezi umekamilika.

Dkt. Slaa anakabiliwa na tuhuma za kusambaza taarifa za uongo kwenye Mtandao wa X ambapo inadaiwa ametenda kosa hilo chini ya kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao namba 14 ya Mwaka 2015.

Ikumbukwe, Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) amekata rufaa katika Mahakama ya Rufani, kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu ulioelekeza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kushughulikia suala la dhamana ya Dkt. Slaa na kuangalia uhalali wa kesi ya jinai inayomkabili kwa haraka.

Soma, Pia: Dkt. Slaa ashindwa kufikishwa Mahakamani kutokana na changamoto za usafiri
 
Mkiambiwa CCM imeoza na ni waoga kuliko kunguru muwe mnaelewa sasa dr slaa mmoja tu inamuogopa mpaka kutumia polisi na mahakama viwasaidie wakati wangempa kazi ya kujibu hoja zake babu wasira tu
 
Nakumbuka Lema alivyo soteshwa mahabusu bila dhamana kwa miezi kadhaa
 
Mkiambiwa CCM imeoza na ni waoga kuliko kunguru muwe mnaelewa sasa dr slaa mmoja tu inamuogopa mpaka kutumia polisi na mahakama viwasaidie wakati wangempa kazi ya kujibu hoja zake babu wasira tu
Slaa anastahili anachokipitia sasa tena ikibidi aongezewe dose
 
Kesi ya kusambaza taarifa za uongo kwenye Mtandao wa X inayomkabili wanasiasa mkongwe nchini, Dk Willibrod Slaa (76) itatajwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.

Dk Slaa anadaiwa kutenda kosa hilo chini ya kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao namba 14 ya mwaka 2015.

Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Beda Nyaki na imeitwa leo Alhamisi, Februari 6, 2025 kwa ajili ya kutajwa na kuangalia iwapo upelelezi wake umekamilika.

Soma, Pia: Dkt. Slaa ashindwa kufikishwa Mahakamani kutokana na changamoto za usafiri
Hamna kesi hapo bali wanamkoa ili akae kimya.
 
Kesi ya kusambaza taarifa za uongo kwenye Mtandao wa X inayomkabili wanasiasa mkongwe nchini, Dk Willibrod Slaa (76) itatajwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.

Dk Slaa anadaiwa kutenda kosa hilo chini ya kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao namba 14 ya mwaka 2015.

Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Beda Nyaki na imeitwa leo Alhamisi, Februari 6, 2025 kwa ajili ya kutajwa na kuangalia iwapo upelelezi wake umekamilika.

Soma, Pia: Dkt. Slaa ashindwa kufikishwa Mahakamani kutokana na changamoto za usafiri
Huyu Mzee apatiwe haki yake ya kupewa dhamana
 
Mkiambiwa CCM imeoza na ni waoga kuliko kunguru muwe mnaelewa sasa dr slaa mmoja tu inamuogopa mpaka kutumia polisi na mahakama viwasaidie wakati wangempa kazi ya kujibu hoja zake babu wasira tu

Tayizo ni Maza. Yuko tayari kufanya lolote abakie madarakani. Uliiona sura yake kwenye mkutano Mkuu wa CCM. Hata JK alionekana kuingiwa na woga.😁😁😁😁
 
Watt hawajifunzi sijui kwa Nini. Hakika Machi, 21 inaondoka na huyu wa sasa tena labda hapo wanaokuja watajifunza
 
Back
Top Bottom