Kesi ya Kumjeruhi na kutishia kwa bastola Klabu 1245 yasimama, baada ya mlalamikaji kuchelewa

Kesi ya Kumjeruhi na kutishia kwa bastola Klabu 1245 yasimama, baada ya mlalamikaji kuchelewa

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kivukoni, iliyoko Kinondoni, imeshindwa kuanza usikilizwaji wa kesi ya kumjeruhi na kutishia kwa silaha ya moto (bastola), katika klabu ya usiku (Night Club) 1245, Masaki, Dar es Salaam, kutokana na mlalamikaji kuchelewa kufika mahakamani kwa muda uliopangwa.

Katika kesi hiyo, mshtakiwa Derick Derick Junior (36), mkazi wa Salasala, jijini Dar es Salaam, anakabiliwa na mashtaka mawili: kujeruhi na kutembea na silaha hadharani kwa namna ya kuleta utisho.

Anadaiwa kutenda makosa hayo Oktoba 27, saa 12:30 asubuhi, katika Kklsbu hiyo, eneo la Masaki wilayani Kinondoni.

Soma Pia: Kesi ya Mtumishi wa TRA aliyetishia Bastola na kujeruhi mtu Club 1245 yapigwa Kalenda hadi Januari 21, 2024

Kesi hiyo inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Is-haq Kuppa, ilitarajiwa kuanza kuunguruma leo rasmi, kwa Mahakama kuanza kupokea ushahidi wa upande wa mashtaka.

Hata hivyo, usikilizwaji hakufanyika kutokana na mlalamikaji, Bujuru, ambaye ni shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka, aliyetarajiwa kuanza kutoa ushahidi wake, kuchelewa kufika mahakamani kwa muda uliopangwa.
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kivukoni, iliyoko Kinondoni, imeshindwa kuanza usikilizwaji wa kesi ya kumjeruhi na kutishia kwa silaha ya moto (bastola), katika klabu ya usiku (Night Club) 1245, Masaki, Dar es Salaam, kutokana na mlalamikaji kuchelewa kufika mahakamani kwa muda uliopangwa.

Katika kesi hiyo, mshtakiwa Derick Derick Junior (36), mkazi wa Salasala, jijini Dar es Salaam, anakabiliwa na mashtaka mawili: kujeruhi na kutembea na silaha hadharani kwa namna ya kuleta utisho.

Anadaiwa kutenda makosa hayo Oktoba 27, saa 12:30 asubuhi, katika Kklsbu hiyo, eneo la Masaki wilayani Kinondoni.

Kesi hiyo inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Is-haq Kuppa, ilitarajiwa kuanza kuunguruma leo rasmi, kwa Mahakama kuanza kupokea ushahidi wa upande wa mashtaka.

Hata hivyo, usikilizwaji hakufanyika kutokana na mlalamikaji, Bujuru, ambaye ni shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka, aliyetarajiwa kuanza kutoa ushahidi wake, kuchelewa kufika mahakamani kwa muda uliopangwa.


Mlalamikaji.png
 
Ni mimi wako UWESUTANZANIA ✍️

Kwanza, club asubuhi unaenda fata nini?
Pili, kesi ya kumiliki silaha inamuhitaji yule shahidi?
Tatu kamdomo nilale mie🛏️🚪
 
Back
Top Bottom