Kesi ya Liyumba, Utata na Maendeleo yake

Status
Not open for further replies.
amekuja mwenyewe pasi escort yao hao PCCB wala polisi, ni familia yake tu ndio amekuja nayo.

Nafikiri kumtendea haki huyu bwana kichwa cha habari hii kilipaswa kuwa " Liyumba aibukia/afika mahakamani". Maana hii ya kufikishwa ni kwamba amedakwa mafichoni na kufikishwa mahakamani. Alikuwa bagamoyo huyu na alipewa sharti la kutokuwa na simu, kutosoma gazeti, kutoangalia TV wala kutoaga familia yake mahali alipo ili yale mambo yawekwe sawa.
 

Nakubaliana nawe Jafar kwamba TAKUKURU hawakupaswa kuanza kumtafuta mtuhumiwa. Kazi yao ni kumshika tu na kumfikisha mahakamani na baada ya hapo ni kazi ya polisi kujua wapi alipo mshitakiwa. Iweje TAKUKURU waanze hata kutangaza dau kwamba yo yote atakayetoa taarifa wapi mtuhumiwa alipo atapewa donge nono? Wakati huo huo polisi wanasema hawamtafuti mshitakiwa kwani hakuna warrant ya kumshika. There is a lot that needs clarification.
 
Kuna sheria nyingi tu zinazoweza kutumika kuhakikisha huyu jamaa hawi tena hatari kwa jamii. Rais, Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa wilaya wana nguvu za kutosha ikiwa ni pamoja na zile zinazotolewa na preventive detantion Act, Sina hakika kama ile detantion facility kule mafia infanya kazi au la, lakini huyu jamaa bado ni hatari ka jamii
 
Kumbe Liyumba alipita seminari,no wonder yuko hivyo alivyo! analipia alichokuwa anakosa wakati huo!

There is something which can be called "Seminary phenomenon". Majority of ex-seminary do show such behavior though not to such an extreme of AL.😱
 
Tuambieni jamani vipi huko, mzee wetu aliyekuwa padre mtarajiwa ameshapanda kizimbani?? Ninachotabiri ni kuwa katika kesi zote za EPA mara matumizi mabaya ya ofisi, PCCB na DPP watakuwa loosers. Kwanza wamefungua kesi nyingi mno ambazo ni tricky wakati hawana competent staff wa kuziendesha. Utaona jinsi private advocates watakavyowababaisha katika kusikiliza. Yangu macho.
 
Give us some more updates from kisutu.. nimesikia kumetokea mvutano kati ya mawakili wa serikali na wanaomtetea amatus!!
 
Katika malumbano hayo inadaiwa kwamba hati za mdhamana ziliwasilishwa na watoto wa liyumba wakati yeye akiwa rumande..so katika mvutano huo mawakili waserikali walitaka afunguliwe mashitaka kwa kuleta document zenye utata huo..kesi bado inaendelea ndani ya kisutu
 
hawa wa serikali wamejaa ubabaishaji na kiburi cha mamlaka na ndicho kilichomponza mama Msongo aliposhindwa ku handle arguments za pande mbili huku ikiwa ni dhahiri upande wa watetezi walikuwa na strong argument na wame prove mbele yake lakini mama akachachawa sasa huko ndani sijui kama keshajitoa au la? Na je atakayeipokea kesi ana guts za kuhimili malumbano yao
 
hII NI DRAMA JUU YA DRAMA..KAZI IPO SANA MWAKA HUU HADI KUELEKEA UCHAGUZI 2010......TUTAONA MENGI SANA....
 
du. kumbe AL alipitia seminari! watu waliopitia seminari wanatakiwa wawe mfano wa tabia nzuri na maadili mazuri katika jamii na kwa taifa lao.

ni aibu mtu aliyelelewa katika mazingira ya dini kuingia katika kashfa kubwa kama hiyo. na waliosomea shule za za kawaida zisizo na utaratibu maalum na mzuri wa kulea vijana kiroho /kimaadili waweje?
 

Extremities are Everywhere!!! Ndo maana hakuapata daraja la upadre...
 


tk, sababu kubwa ya watu kuandika walivyoandika ni mazingira yenyewe.

1. AL aliambiwa atolewe dhamana ya kiasi fulani halafu kikatolewa kiasi pungufu na kilichotakiwa. tafsir ni nini? kwa wengine wakaona kwa kuwa hela inayotolewa kwenye dhamana hairudi jamaa akitoroka amefanya mpango asipoteze hela nyingi kwasababu alikuwa na mpango wa kutoroka
2. aliambiwa apeleke pasipoti yake lakin yeye akatoa ya zamani wakati wengine hapa wamesema majuz juz tu alienda sijui china, sasa huko china alienda bila pasipot? hapana. hapo watu wakaona changa la macho - jamaa katoa pasipot iliyopitwa na muda kabaki na mpya iliakitaka kuingia mitin iwe rahis
3. majuzjuz aliyekuwa gavana wa bot (mungu amlaze mahali pema peponi)akaenda nje wakat hapa hali ya hewa haikuwa nzuri sana kwake. halafu vuuuuuuuup, taarifa hizo - jamaa kafa na kwahiyo kama kungekuwa na kesi dhidi yake utamfungulia nani? mkewe? nop. mwanae? nop. kwahiyo? imetoka hiyo. na mazishi yakawa kisirsiri. wengine wanasema hajafa. kajificha.

na mambo mengine kama hayo.
kwa hiyo watu wakachukua 1 wakajumlisha na 1 wakapata 2.
 
Amerudishwa rumande mpaka atakapokamilisha masharti yote, mahakama inasema hati yake kusafiria imebainika kuwa ime expire na si ile iliyoletwa kwa hakimu awali, thamani ya mali zilizoletwa bado hazijathibitika kufanana na uhalisia kithamani.

Dhamana iko wazi upon completion of masharti aliyopewa.

Kazi, kwelikweli, mama hadija katoa maamuzi hayo yeye mwenyewe punde
 
TAKUKURU wasitukumbushe machungu ya Richmond wafanye kazi zao bila usanii na sheria ichukue mkondo wake.
 
at least now the gvt is trying to show its responsibility to citizens. but we want more.

government inaonyesha responsibilty gani? kwa kuwakamata akina liumba walioamriwa kuchota pesa kwa ajili ya uchafuzi uliyoiweka the vey vey government?

ni vema tukaacha ushabiki na kuwapa watu sifa wasizostahili, hili drama la lyumba limesukwa tusahau yafuatatyo

1. rostam aziz na wizi wake wa 40bn kupitia kagoda

2. richmond na mitambo ya dowans inayotakika kununuliwa kwa 60bn

3. mkapa na wizi wake wa kiwira nakampuni lake la anben

5 . kikwete na udhaifu wake wa kuvifunga vyuo vyote vya umma baada ya utawala kumshinda

6. mkapa, bernard mchovu na wengine waliochota pesa kupitia EPA

KUNA WANA JF WAMESHAJISAHAU NA KUANZA KUSHABIKIA DRAMA LA LIUMBA, MSISAHAU KUWA WALE WANAOFIKISHWA KIUTU HADI SASA HAKUNA SWAHIBA HATA MMOJA WA KIKWETE, YALE MAJANGILI KAMA ROSTAM, KARAMAGI, CHENGE, MAHITA, NK AMBAO NI CHANDA NA PETE NA JK WAPO MTAANI WAKATI JK AKIENDELEA KUCHEZA MCHEZO MAARUFU WA MDUARA ULE WA UKTI UKTU WA MNAZI, NA WATANZANIA TUKIMSHANGILIA, WA MNAZI WA MNAZI
 
There is something which can be called "Seminary phenomenon". Majority of ex-seminary do show such behavior though not to such an extreme of AL.😱

mmesahau hata chenge ni ex-seminarian!!!
 

Kwanza unasema 99% ya wana JF sijui ni formula gani hio uliyotumia...Ila karibu JF na utaendelea kujifunza tu.

Pili naomba nikukumbushe kitu kimoja;Kwenye data processing kuna Input Proceesing Output (IPO mode)Mwakatojofu amegusia baadhi ya points hapo juu na mimi nita add just a couple...

1)Masharti ya mdhamana yalikiukwa kwa vielelezo visivyokidhi mahitaji ya mdhamana na hivyo wachambuzi wa mambo lazima watahoji...This is regardless of the fact kuwa bail money ilikuwa reduced kwa kwa namna ambayo inazua maswali.

2)Mahakama iliwashikilia kwa muda wadhamini kwani mtuhumiwa hakufika mahakamani hapo ambapo aliitwa kabla ya tarehe hiyo feb 24 ambayo kila mtu alijuwa ndio siku kesi itakapotajwa tena except sababu ya kuitwa mahakamani kabla ya siku ya kesi ndiyo hakuna anayejuwa ila tulidhani kuwa ni kwasababu ya fununu kuwa litoroka na mazingira ya document zake un qualified.(rejea kauli ya hakimu Khadija kwamba faili liko mahakama kuu)

3)TAKUKURU wakatangaza "donge nono" kwa mwenye taarifa za kuwezesha kupatikana kwa mtuhumiwa.....Hapo tukajuwa ni kweli mtuhumiwa hapatikani...Sasa TAKUKURU wenyewe wako hapo bongo na wakakiri katoroka..Sisi je? Mazingira yote ya kesi yalipelekea mjadala huu kuenda ulivyoenda...Kwa maana kwamba ni input ya data hapa JF na tukaprocess na information ndio kama ilivyo kama unavyosikia huko mahakamani mvutano kuhusu mdhamana na documents....Hatukuanzisha hizi habari ila sisi tulikuwa tuna process ama tuna analyze,all in all hata kama walikuwa wanapima zali wamegunduwa mboga moto na ugali moto kama nilivyosema huko nyuma.

Kwa kifupi ni kwamba huwezi kukaa pembeni halafu unakuja mwishoni na kudai eti ilikuwa mseme hivi na si vile kwasababu tulikuwa wrong, na mambo ya 1% ya JF na 99% ambayo hata namna uliyofikia hiyo conclusion haujulikani,kwamba eti busara,haa hii ndio busara...If that was the case JF isingekuwa hapa JF mkuu....Na kwamba eti habari ikija sijui hatufahamu kama ni kweli...Mambo haya na mawazo haya sishangazwi kwani hata Pengo na yeye ana mawazo kama yako tu...Sasa na habari za Ufisadi zilianzia wapi? Si ziliitwa porojo za vyombo vya habari na mtandao?
Ndugu tk quit be an opportunist na uchangie mjadala si kwa madhumuni ya kushindana bali kuelimishana.
Na pia unaposema tuliwatukana watu wa serikalini bila subira, kwani TAKUKURU ni ya wapi? Mahakama ni ya wapi? Kwenda mahakamani kwa Liyumba haina maana kuwa serikali haikufanya makosa, na ndio maana kama ulifuatilia mjadala huu nilisema kuwa tusijadili sana kuhusu kutoroka bali tujadili kuhusu mazingira ya mdhamana wake kwasababu bottomline lazima kuwe na accountability, kutokuja bila escort ni kujaribu kuwasifisha waliokuwa responsible,kwamba hakukuwa na nia yoyote ya kumtorosha,kama kulikuwa na mawasiliano mabovu kiasi cha TAKUKURU kutangaza pesa kwa mtuhumiwa aliyetoroka basi JF tulikuwa na haki ya kusema lolote.
 
Last edited:
Kosa la kutoripoti mahakamani kila siku kama alivyokubaliana na mahakama au dhamana lipo au halipo ? Mengine yote kwanza wekeni kando ,maana kama kuendeshwa kiubabe ndio huku.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…