Ibrahimu Zuberi Mkondo
Member
- Sep 19, 2019
- 43
- 383
Bismillahir Rahmanir Rahiim
SHURA YA MAIMAMU TANZANIA
MASHEIKH WAPATA USHINDI MKUBWA MAHAKAMA YA RUFAA LEO
Hukumu ya rufaa ya Jamhuri dhidi ya Masheikh imesomwa leo katika Mahakama ya Rufaa Tanzania.
Majaji watatu wa Mahakama hiyo wametupilia mbali rufaa ya upande wa Jamhuri ya kutaka mashtaka 14, dhidi ya Masheikh yaliyofutwa na Mahakama Kuu ya Tanzania yarudishwe.
Katika Mahakama hiyo leo Mawakili 9, wanaowatetea Masheikh na wanasheria 11, wa upande wa serikali walionekana wakisikiliza kwa umakini mkubwa wakati hukumu hiyo ikisomwa.
Mahakama ya rufaa imeitupa rufaa ya Jamhuri kwa hoja iliyotokana na pingamizi lililowekwa na mawakili wa masheikh kuwa Jamhuri haikuwa na haki ya kukata rufaa hukumu iliyofuta mashitaka 14 kwasababu hukumu ile haikumaliza kesi (yaani haikuwatia hatiani wala kuwaachia masheikh).
Haki ya kukata rufaa kwa Jamhuri ipo tu ikiwa hukumu imewatia hatiani au kuwaachia washitakiwa kitu ambacho hakipo katika hukumu ya mahakama kuu.
Mahakama ya rufani imesema haki ya kukata rufaa kwenye maamuzi madogo iliondolewa na mahakama ya Kikatiba na sasa Jamhuri hawana haki hiyo.
Duru za wanasheria zinasema hukumu ya leo ya mahakama ya rufaa imeleta mapinduzi makubwa katika tasnia ya sheria kwani sasa Jamhuri wameondolewa uwezo wa kukata rufaa hovyohovyo kitendo ambacho kilikuwa kinawaonea washitakiwa katika kesi za jinai na ucheleweshaji wa kesi.
Kufuatia hukumu hiyo shauri hilo sasa linarudishwa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam kuendelea kusikilizwa mashauri 11, yaliyobaki.
Aidha Shura ya Maimamu Tanzania inawapongeza Mawakili wasomi 9, wanao watetea Masheikh hao kwa kazi kubwa wanayoifanya.
Shura pia inawapongeza Watanzania wote walioitikia wito wa kuwaombea dua Masheikh hao wapate ushindi katika hukumu ya leo.
Ust. Ibrahim Z. Mkondo
Msemaji wa Shura.
0713118812
SHURA YA MAIMAMU TANZANIA
MASHEIKH WAPATA USHINDI MKUBWA MAHAKAMA YA RUFAA LEO
Hukumu ya rufaa ya Jamhuri dhidi ya Masheikh imesomwa leo katika Mahakama ya Rufaa Tanzania.
Majaji watatu wa Mahakama hiyo wametupilia mbali rufaa ya upande wa Jamhuri ya kutaka mashtaka 14, dhidi ya Masheikh yaliyofutwa na Mahakama Kuu ya Tanzania yarudishwe.
Katika Mahakama hiyo leo Mawakili 9, wanaowatetea Masheikh na wanasheria 11, wa upande wa serikali walionekana wakisikiliza kwa umakini mkubwa wakati hukumu hiyo ikisomwa.
Mahakama ya rufaa imeitupa rufaa ya Jamhuri kwa hoja iliyotokana na pingamizi lililowekwa na mawakili wa masheikh kuwa Jamhuri haikuwa na haki ya kukata rufaa hukumu iliyofuta mashitaka 14 kwasababu hukumu ile haikumaliza kesi (yaani haikuwatia hatiani wala kuwaachia masheikh).
Haki ya kukata rufaa kwa Jamhuri ipo tu ikiwa hukumu imewatia hatiani au kuwaachia washitakiwa kitu ambacho hakipo katika hukumu ya mahakama kuu.
Mahakama ya rufani imesema haki ya kukata rufaa kwenye maamuzi madogo iliondolewa na mahakama ya Kikatiba na sasa Jamhuri hawana haki hiyo.
Duru za wanasheria zinasema hukumu ya leo ya mahakama ya rufaa imeleta mapinduzi makubwa katika tasnia ya sheria kwani sasa Jamhuri wameondolewa uwezo wa kukata rufaa hovyohovyo kitendo ambacho kilikuwa kinawaonea washitakiwa katika kesi za jinai na ucheleweshaji wa kesi.
Kufuatia hukumu hiyo shauri hilo sasa linarudishwa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam kuendelea kusikilizwa mashauri 11, yaliyobaki.
Aidha Shura ya Maimamu Tanzania inawapongeza Mawakili wasomi 9, wanao watetea Masheikh hao kwa kazi kubwa wanayoifanya.
Shura pia inawapongeza Watanzania wote walioitikia wito wa kuwaombea dua Masheikh hao wapate ushindi katika hukumu ya leo.
Ust. Ibrahim Z. Mkondo
Msemaji wa Shura.
0713118812