Kesi ya Mbowe isizuiwe watu kutaarifiwa

Kesi ya Mbowe isizuiwe watu kutaarifiwa

Kisanduku

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2009
Posts
284
Reaction score
483
Jana dunia nzima ilifaidi kesi ya Mbowe na hata Jaji alisema ana taarifa kwamba proceedings za kesi hiyo zinataarifiwa mitandaoni.

Tulifaidi RPC wa Kinondoni alivyhojiwa na Advocate Kibatala hadi akaomba kwenda kukojoa.

Jioni watu wakanusa mkakati wa kukatazwa kuingia na simu, siyo Mahakama, wala si sheria, bali askari.

Dakika hizi tunavyoongea ni kweli wanautekeleza, kesi imekaribia kuanza lakini wamezuia wenye simu wasiingie nazo hivyo taarifa zidhibitiwe.

IGP alisema wana ushahidi mzito sasa kwanini wasiuelezee watu live kwenye kesi hii ambayo ni open court.

Sasa watu wa upande wa Mbowe wamekubaliana kwamba ikibidi wawatoe Mawakili wao kesi isiendelee hadi Mahakama iseme utaratibu wa Kisheria wa huu mkakati uliopangwa na polisi.

Katika hili nawakumbusha jambo moja. Mwaka 1983 akina Zacharria Hans Pope walitaka kuipindua serikali, wakakamatwa kwa kosa la uhaini.

Kesi ile ilianza kusikilizwa mwaka 1985 na gazeti la UHURU lilikuwa linaandika kila mahojiano.

Watu walifaidi uhondo kila siku. Kuna wakili wa aliyewatetea wahaini aliitwa Murtaza Lakha alipata umaarufu kuwapelekesha Serikali kama Kibatala alivyompelekesha RPC jana.

Imagine Lakha alimuuliza wakili wa serikali kuhusu tetesi kwamba mama yake Rais Julius Nyerere alikuwa mchawi hivyo alisababisha mwanaye asipinduliwe.

Kama mkuu wa nchi alitajwa hivyo kwenye kesi na ikaendelea kuandikwa magazetini iweje mtu mdogo sana kama RPC au IGP tusione anavyokomosha au kukomeshwa Mahakamani.

Hivyo tusubiri tuone nini kitaendelea, macho yote mahakamani.

Mbowe ni gaidi au siyo gaidi


UPDATE:


 
Kibatala peleka motooooooo

Haahaahahaa raha sana ukiwa wakili msomi na hujashikiwa akili pale Lumumba!

Nadanganya wadau?
 
Labda Pascal Mayalla atusaidie

Huyu Peter Kibatala ananikumbusha wakili msomi Murtaza Lakha!
Bwashee si ulikuwepo enzi hizo ukifaudu uhondo wa maswali ya Adv Lakha? Kwa nini unamuuliza Paskali ambaye wakati huo alikuwa hajazaliwa; au kama alikuwa amezaliwa alikuwa bado ananyonya? Waeleze wenzio tu kwamba kesi hii ni ya kubuni na serikali inajikuta pabaya siku ya kwanza na mwisho wa kesi hii umeshafahamika!
 
Bwashee si ulikuwepo enzi hizo ukifaudu uhondo wa maswali ya Adv Lakha? Kwa nini unamuuliza Paskali ambaye wakati huo alikuwa hajazaliwa; au kama alikuwa amezaliwa alikuwa bado ananyonya? Waeleze wenzio tu kwamba kesi hii ni ya kubuni na serikali inajikuta pabaya siku ya kwanza na mwisho wa kesi hii umeshafahamika!
Adv Lakha alikuwa wakili wa mzee Mayalla ( baba yake Pascal) na wakati ule Pascal alikuwa anajitambua tayari!
 
Wakenya wao wamefikia kwenye kesi hadi TV zinakua live sasa Tanzania kuna wajinga ambao hawajui dunia iko wapi, hiyo ni kesi wa wazi lazima tuifuatilie sote kama taifa
Kenya wana uwazi sana hasa kwenye maswala ya kisheria!
 
Jana dunia nzima ilifaidi kesi ya Mbowe na hata Jaji alisema ana taarifa kwamba proceedings za kesi hiyo zinataarifiwa mitandaoni.

Tulifaidi RPC wa Kinondoni alivyhojiwa na Advocate Kibatala hadi akaomba kwenda kukojoa.

Jioni watu wakanusa mkakati wa kukatazwa kuingia na simu, siyo Mahakama, wala si sheria, bali askari.

Dakika hizi tunavyoongea ni kweli wanautekeleza, kesi imekaribia kuanza lakini wamezuia wenye simu wasiingie nazo hivyo taarifa zidhibitiwe.

IGP alisema wana ushahidi mzito sasa kwanini wasiuelezee watu live kwenye kesi hii ambayo ni open court.

Sasa watu wa upande wa Mbowe wamekubaliana kwamba ikibidi wawatoe Mawakili wao kesi isiendelee hadi Mahakama iseme utaratibu wa Kisheria wa huu mkakati uliopangwa na polisi.

Katika hili nawakumbusha jambo moja. Mwaka 1983 akina Zacharria Hans Pope walitaka kuipindua serikali, wakakamatwa kwa kosa la uhaini.

Kesi ile ilianza kusikilizwa mwaka 1985 na gazeti la UHURU lilikuwa linaandika kila mahojiano.

Watu walifaidi uhondo kila siku. Kuna wakili wa aliyewatetea wahaini aliitwa Murtaza Lakha alipata umaarufu kuwapelekesha Serikali kama Kibatala alivyompelekesha RPC jana.

Imagine Lakha alimuuliza wakili wa serikali kuhusu tetesi kwamba mama yake Rais Julius Nyerere alikuwa mchawi hivyo alisababisha mwanaye asipinduliwe.

Kama mkuu wa nchi alitajwa hivyo kwenye kesi na ikaendelea kuandikwa magazetini iweje mtu mdogo sana kama RPC au IGP tusione anavyokomosha au kukomeshwa Mahakamani.

Hivyo tusubiri tuone nini kitaendelea, macho yote mahakamani.

Mbowe ni gaidi au siyo gaidi
Naomba kuuliza, hivi Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), halioni jinsi watawala wanavyotumia vyombo vya Dola kunyanyasa raia wake? Je Jeshi ni kulinda maadui wa Raia walio nje tu ya mipaka na wala si Maadui walio ndani ya Mipaka? Je Jeshi halijui hao wanaonyanyaswa ni Ndugu zao? Au jeshi nalo halina watu weredi wa kurekebisha hayo?

Naomba mwenye majibu tafadhari anieleweshe.
 
Bwashee si ulikuwepo enzi hizo ukifaudu uhondo wa maswali ya Adv Lakha? Kwa nini unamuuliza Paskali ambaye wakati huo alikuwa hajazaliwa; au kama alikuwa amezaliwa alikuwa bado ananyonya? Waeleze wenzio tu kwamba kesi hii ni ya kubuni na serikali inajikuta pabaya siku ya kwanza na mwisho wa kesi hii umeshafahamika!

Yaani Paskali awe hajapevuka (achilia mbali kuzaliwa) mwaka 1985! Mtake radhi kama haumaanishi FUTUHI hapa.
 
Mliopo mahakamani fanyeni juu chini tupate Cross examination ya Kitabala na huyo shaidi Kingai,najua ndicho wanachoogopa[emoji3]

Kumbe hadi aliomba kwenda kukojoa?
 
Naomba kuuliza, hivi Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), halioni jinsi watawala wanavyotumia vyombo vya Dola kunyanyasa raia wake? Je Jeshi ni kulinda maadui wa Raia walio nje tu ya mipaka na wala si Maadui walio ndani ya Mipaka? Je Jeshi halijui hao wanaonyanyaswa ni Ndugu zao? Au jeshi nalo halina watu weredi wa kurekebisha hayo?

Naomba mwenye majibu tafadhari anieleweshe.
Fuatilia mishahara ya JWTZ hapo ndipo utapata majibu sahihi na wala utojusumbuwa tena akili yako kuwaza kwamba ipo siku wanaweza kuingilia kati dhuluma zinazoendelea.

V8 si kwa wanasiasa tu hata vigogo wa jeshini wanazo na marupurupu kedekede.

Wakati wa kula mezani si muda wa kuongea, unaweza kuchukuwa sample ya yule Chakubanga Polepole, ukimchukuwa Polepole wa Tume ya katiba ya Warioba na ukimchukuwa Polepole wa serikali ya Magufuli na ukimchukuwa Polepole huyu mtoto yatima kutoka sukuma gang ni lazima wapigane ngumi za kufa mtu.

Hiyo ndio taswira halisi ya Watanzania walivyo, ni wanafki hata shetani anawaogopa.
 
Back
Top Bottom