Kesi ya Mbowe: Kesho shahidi J4 Kizimbani na Kielelezo Chake Tata

Kesi ya Mbowe: Kesho shahidi J4 Kizimbani na Kielelezo Chake Tata

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kesho tutakuwapo kukipokea kile kielelezo kisichojulikana kilivyomfikia Jumanne mahakamani tokea alipomwachia Inspector Swilla.

Pamoja na kuwa kina kurasa 2 na ni ukurasa wa kwanza pekee ulio na sahihi, mchumi wa maneno aliyedhamiria anaweza kutatizika vipi hata kwenye hali tata kama hizo?

Kwamba kunasomeka Halifan, kuwa kuna majina na saini zisizokuwapo, karatasi batili ya usajili imetumika, sheria fyongo imenukuriwa kukihusisha, nk, yote yakiwa yalivyo.

Kwani akisema hakuna athari kwa mshitakiwa na kwamba kwa maoni yake nyie mtajiju, si ndiyo basi?

Akikomelea kabisa na "ninatoa AMRI" si ndiyo itakuwa kwishney?

Tatizo la kisiasa halionekani kuwa na suluhu kwenye mahakama hii.

Yote tisa, kila kona ya nchi bila kupasahau chamwino na magogoni, mdundo ni ule ule. Watu hawaridhiki na kesi hii pamoja vikorombwezo vyake ukiwamo mwenendo wake.

Sasa iko na jina jipya. Wanaiita "jumba bovu."

Kunyoa au kusuka, hiyo sasa ni shauri yake.
 
Nimejifunza kitu, serikali ikiamua kukuacha upotee inaacha haki ifuate mkondo wake, naona hayo kwenye kesi ya Sabaya inayoendelea sasa ambapo hadi maafisa wa Takukuru wanaotoa ushahidi wao wanamkaanga Sabaya.

Lakini kwa kesi ya Mbowe wameamua kuiweka haki ya mtuhumiwa mfukoni kwa kuwatuma maafisa wa polisi kusema uongo mahakamani.
 
Nilijua baada ya ombi la juzi hakuna tena kupandishana vizimbani, Ooh Boy!
Ndugu yangu, wazee wa zamani walisema afadhali mwanaume awe mchawi kuliko mwanamke. Mwanamke akiamua kuwa shetani, anakuwa shetani hasa. Ndiyo maana waovu wengi wakiona ni ngumu sana kumnasa mtu fulani, humtumia mwanamke.

Mwanamke akiwa mwema anakuwa mwema hasa, akiamua kuwa shetani, anakuwa shetani kamili. Katika historia, sijasikia kuna wanaume waliwahi kuandamana uchi wa mnyama, ila wanawake wamefanya maeneo mengi. Sijawahi kusikia kuna club za usiku ambazo wanaume wanacheza uchi wa mnyama, ila za wanawake zimejaa kibao.

Tunapitia kwenye uovu wa mwanamke. Mwanamke mnafiki, mwenye sauti ya huruma lakini roho ya shetani.
 
Nimejifunza kitu, serikali ikiamua kukuacha upotee inaacha haki ifuate mkondo wake, naona hayo kwenye kesi ya Sabaya inayoendelea sasa ambapo hadi maafisa wa Takukuru wanaotoa ushahidi wao wanamkaanga Sabaya.

Lakini kwa kesi ya Mbowe wameamua kuiweka haki ya mtuhumiwa mfukoni kwa kuwatuma maafisa wa polisi kusema uongo mahakamani.

Mchumi wa kutupilia mbali mapingamizi katika ubora wake. Karibu anatoa AMRI.
 
Nimejifunza kitu, serikali ikiamua kukuacha upotee inaacha haki ifuate mkondo wake, naona hayo kwenye kesi ya Sabaya inayoendelea sasa ambapo hadi maafisa wa Takukuru wanaotoa ushahidi wao wanamkaanga Sabaya.

Lakini kwa kesi ya Mbowe wameamua kuiweka haki ya mtuhumiwa mfukoni kwa kuwatuma maafisa wa polisi kusema uongo mahakamani.
UNAHAKI NA MAONI YAKO
 
Kesi imekosa uhalali wa kisheria.

Kazi kweli kweli

IMG_20211217_122156_944.jpg
 
Back
Top Bottom