Kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi yaahirishwa. Kuendelea Jumatatu ya tarehe 27/09/2021

Wameona wameshikwa pumbu,pimbi hawa. Wanaogopa sasa kwa shahidi kama hizi watu wanaendelea kuwa na chuki na polisi
 
Kuuliza sio ujinga...hivi komandoo amestaafu ? Mbona bado kijana
Si ulisikia wanasema wenyewe kwamba walistaafishwa kwa manufaa ya afya zao baada ya kutoka huko Congo walipo pelekwa na serikali ya kikwete kwenda kumfurumusha maimai wa Congo au ? Jamaa walikaa huko sana hadi wakapata PTSD au battle fatigue ...yaana milio ya mizinga na risasi ilizafanya akili zao ziyumbe... sasa baada ya kustaafishwa kwa manufaa ya afya zao, ndio wakatafuta njia mbadala za kutunza familia zao kwa kujiajiri... na ajila waliyoipata ni hiyo ya Mbowe (ulinzi wa VIP)... sasa jiulize, inakuwaje serikali ina gharamia mafunzo yao ya ukomandoo kwa hao vijana miaka mingu tu huko ngerengere , halafu inawatuma huko kwa maimai vitani Congo, wanaugua hiyo PTSD, halafu wanastaafishwa na kubambikiwa kesi ya ugaidi, si ni bora tu wangekuwa Hamza, labda ndio serikali ingewachukulia serious makomandoo.. au labda ingewafanyia utaratibu waendelee kuvunja matofali pale uwanja wa uhuru kila sherehe ya kitaifa... ingewasaidia sana kudumisha afya zao bila kutelekezwa kwa mtindo huu wa kubambikiwa kesi ya ugaini, kuninginizwa kama popo, kunyanganywa tsh 260, 000 , kuchomwa bisibisi halafu eti mawakili wa serikali wanasema hayo ni mambo ya kawaida... labda siku Sirro akitimba, naye wamchome bisibisi kama atasema ni kawaida ...
 
Mkuu usihofu, Kingai na MAGENGE YAKE hakika watalipia hili. Uzuri aliyekuwa anawapa jeuri hatuko naye tena.
 
Hao makomando wapo poa sana ingekuwa nimimi hao wakina mahita na kingai ningewanyonga hadharani hapohapo mahakamani
 
Ila jamani,hii dunia ina mambo sana,yaani watu wamepata mafunzo hadi ya ukomando,wakapelekwa na serikali kupambana na maimai,akili zao zikapata shida kwasabau ya kazi walizotumwa kuzifanya,halafu serikali ikawafukuza,duuuh! kwanini wasingewafanyia namna jamani?
Wanahangaikabadala wangewekwa wafanye kazi mbalimbali kambini,duuh no fairness at all.
 
Hii kesi inathibitisha kuwa ili uwe polisi wa Tanzania lazima uwe mjinga na kuwa CCM ni chama kinachotegemea polisi ili kiweze kuwepo.
 
Hivi wakoloni walipokuwa wanatutawala hawakuwa na jeshi la polisi? Mbona miaka yote kesi ilikuwa moja tu! Kwani mungu wa wazungu na mungu wetu ni tofauti? Kama ningeweza kuriwaindi miaka ningefanya hivyo turudi kwenye utu.
 
Mbona Lisu alisema alikimbilia ubalozini baada ya kupokea simu za vitisho?

..Ni kweli alikimbilia ubalozini.

..lakini alipofika huko, kabla hajaingia akakamatwa na watu wasiojulikana.

..Lissu anadai watu hao walikuwa na magari yenye namba za Kenya.

..sasa huyu Maza Naibu Balozi wa Ujerumani alishuhudia ukamatwaji wa Lissu ndipo alipowafuata wahusika mpaka kituo cha Polisi walipompeleka.

..Kilichofuatia ni Lissu kutoka ktk " kinywa cha mamba " na kupewa hifadhi ubalozi wa Ujerumani mpaka siku aliyokwea pipa kwenda Ubelgiji.

..Ndio maana najiuliza ilikuwa ni bahati tu kwamba wasiojulikana walikuwa wameamka vizuri siku hiyo, wakaamua kutokumdhuru Lissu, au kuna mkwara huyu Maza aliutoa na kusababisha wasiojulikana waufyate mkia?

Cc Fundi Mchundo, Erythrocyte
 
Mkuu hivi komandoo anaweza kushikwa kijinga namna hii kweli

..what is your point?

..unataka kusema hakushikwa, au unataka kusema sio komandoo?

..polisi wanadai walipowashika makomandoo MAGAIDI waliwanunulia mishikaki na vinywaji.

..hivi umesikia wapi kwingine gaidi anakamatwa halafu anapelekwa kwenye MGAHAWA na kulishwa mapochopocho na vinywaji?
 
Mfano kesi inaisha komando anaachiwa huru. Anatoka gerezani akiwa na kinyongo, mara anapata access ya vitendea kazi kama vya Bwana Hamza, Naye anaamua liwalo na liwe lazima niondoke na roho kadhaa…! Kama Hamza alitamba kwa takribani nusu saa nzima bila kudhibitiwa , Huyu mwamba watamzuia vipi akiwa na AK na njugu za kutosha?
 
Kisasi ni cha Mungu
 
Uhusianano kati ya ccm na polisi kidogo unafanana na ule wa konda na mpiga debe kwenye vituo vya daladala.....kulindana na kunufaishana .
 
Hivi kwa akili za kawaida tu mwizi wa kuku tu ameiba na amekamatwa na kidhibiti anakataa sembuse komandoo!!!

Hao wasingeweza kukiri bila kibano cha msingi kinachotafutwa hapo walikuwa na nia ofu au laah mengine hapo ni blah blah tu
Askari anakamata "mhalifu" anamkuta na bastola na heroin alafu anamfungulia kesi ya ugaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…