wakimataifa.
JF-Expert Member
- Jun 7, 2015
- 1,625
- 558
Ile songombingo ya mchezaji yatima aitwae Singano anayedhurumiwa haki yake kwa vitisho wa viongozi wa Simba ni leo pale TFF.
Kuna habari Messi alitaka kusaini mkataba miaka miwili Simba walitaka miaka mitatu Simba walipoona watamkosa wakakubali wakaandaa miaka miwili katika mkataba kulikuwa na malipo ya pango kila mwezi Messi akausoma akasaini ile karatasi ya mwisho ndio kuna sahihi ya pande zote mbili simba wakamwambia hizi saini zimekosewa saini hii nyingine akasaini hiyo karatasi ya pili aliosaini wakaiweka kwenye mkataba wa miaka 3.Na malipo ya pango hajalipwa akadai akaambiwa mzawa halipiwagi hela za pango.
Sasa nawambia TFF japo mmesema tusizungumzie suala hili sisi tumesema na msipoamua vizuri tutawaomba FBA.
Maana tumewachoka na mambo yenu
Kuna habari Messi alitaka kusaini mkataba miaka miwili Simba walitaka miaka mitatu Simba walipoona watamkosa wakakubali wakaandaa miaka miwili katika mkataba kulikuwa na malipo ya pango kila mwezi Messi akausoma akasaini ile karatasi ya mwisho ndio kuna sahihi ya pande zote mbili simba wakamwambia hizi saini zimekosewa saini hii nyingine akasaini hiyo karatasi ya pili aliosaini wakaiweka kwenye mkataba wa miaka 3.Na malipo ya pango hajalipwa akadai akaambiwa mzawa halipiwagi hela za pango.
Sasa nawambia TFF japo mmesema tusizungumzie suala hili sisi tumesema na msipoamua vizuri tutawaomba FBA.
Maana tumewachoka na mambo yenu
Uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo umekutana na Uongozi wa klabu ya Simba SC ukiwakilishwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Collin Frisch na mchezaji Ramadhani Yahya Singano akiandamana na Uongozi wa Chama cha Wacheaji wa Mpira wa Miguu (SPUTANZA). Kikao hiki kiliitishwa na TFF kujadili utata wa kimtakabta kati ya mchezaji na klabu ya Simba.
Katika kikao cha leo pande zote zimeeleza kutambua utata ulio ndani ya mikataba iliyokuwepo ambayo kimsingi iliingiwa kabla ya uongozi wa sasa wa Simba SC.
Kwa pamoja pande hizo mbili zimekubaliana kuanza mazungumzo ya makubaliano mapya na hatimaye mkataba mpya utakaoanza katika msimu mpya wa 2015/16.
TFF imevitaka vilabu kushirikiana na SPUTANZA na Bodi ya Ligi katika kuweka mifumo mizuri ya uingiaji mikataba. TFF inao mkataba mama (template) ambao vilabu vyote na wachezaji wanatakiwa waufuate wakati wanaandaa mikataba yao (individual contracts between players and clubs). Aidha TFF imewataka wachezaji kuelewa mikataba kabla ya kutia sahihi.
TFF itazidi kuboresha mfumo wa usajili wa wachezaji na mikataba ili kuweka mazingira sawia kati ya pande zote mbili (Wachezaji na vilabu)
Makubaliano yamefanyika leo tarehe 9 Juni 2015 na kusainiwa na:-
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
- Collin Frisch - Simba SC
- Ramadhan Singano - Mchezaji
- Mussa M. Kissoky - SPUTANZA
- Mwesigwa J. Selestine - Katibu Mkuu - TFF