Kesi ya Ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake watatu yaendelea kuvutia Mabalozi na Wawakilishi wa Jumuiya za Kimataifa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426


Kesi hiyo inayoendelea leo kwenye Mahakama ya Uhujumu Uchumi chini ya Jaji Mpya Mustapha Siyani , kama kawaida imehudhuriwa na Mabalozi na wawakilishi wa Jumuiya za Kimataifa .



Tayari Mheshimiwa Mbowe amefika ndani ya Mahakama hiyo kwa usikilizaji wa kesi dhidi yake na wenzake watatu .



Endelea kutufuatilia ili kufahamu yanayojiri Mahakamani
 
Huyo mdhungu kaja kudanga tu kortini. Haohao wanahudhuria kortini jioni utasikia haohao wametoa bilioni kadhaa kusapoti kazi nzuri ya serikali. Nyumbu huwa hamuwezi kujinasua na misimamo ya kijinga kama wataleban. Subirieni mvua zinamhusu DJ
 
Mungu ibariki CHADEMA Mungu zidi kumtia nguvu mwamba
 
Mkuu, tunatumai kuwa mambo yatakuwa mazuri huko mahakamani. Halafu, huyo dada aliyechuchumaa mbele ya Mbowe amependeza na pete zake mkononi na mguuni. Msalimie sana!
 
Ninafuatilia kwa makini sana ili nijue kinacho jiri hapo mahakamani
Msalimie wakili msomi pita kibatalaa na jopo zima la mawakili wasomi wa mh mwamba
Nina hamu kubwa kujua hiyo hati mpya ya mashitaka wame edit namna gani?
 
Ni vyema wakihudhuria, ili ikitokea sheria imemkuta na hatia na kapewa miaka kadhaa msipate mwanya wa kwenda kuwadanganya kama ilivyo kawaida yenu.
 
Mvua nyingi zinamuhusu alifikiri kubadili jaji ndiyo suluhisho?
Ndugu yangu, yawezekana shetani ndie anakuendesha kushabikia sana dhulma kwa wengine bila hata chembe ya soni.
Ninakuombea uhai ili uje na uwepo kushuhudia Mbowe akitoka akiwa HURU, nikitumaini kwamba itakusaidia kuachana na shetani pamoja na mambo yake yote.
Mungu mwenye upendo atakusamehe, kukupokea na kukufanya uwe kiumbe kipya.
AMEN
 
SAWA NDUGU MBOWE ATATOKA JE SABAYA VIPI ALE MVUA?
 
Ni vyema wakihudhuria, ili ikitokea sheria imemkuta na hatia na kapewa miaka kadhaa msipate mwanya wa kwenda kuwadanganya kama ilivyo kawaida yenu.
hao wanaenda kuhakikisha jamaa anakula mvua ngapi maana walimpa hela nyingi waingie madarakani ili waje kula rasilimali zetu
 
Imeandikwa "Nayaweza mambo yote katika yeye anitiae nguvu"

Pia imeandikwa " Mungu akiwa upande wetu, Ni nani aliye juu yetu"

Mungu aliyefunga kinywa Cha Simba wakat Daniel ametupwa katika Shimo la Simba huyu ndiye atakaye mtetea Mbowe dhidi ya watesi wake!

Mungu mbariki mbowe, mtetee, muokoe na kumtoa katika mikono ya watesi wake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…