Kesi ya ugaidi wa Mbowe: Uamuzi wa Jaji wa pingamizi la upande wa utetezi kesho unaweza kuja na haya....

Alimlaani jiwe na akalanika huyo huyo mwizi wa magari.
Mnajionaje ninyi ?!!!

Yaani uhai wa mtu/watu uendelee ama ukome kwa sababu ya MTU FULANI NA MAOMBI YAKE?!!!

Hivi kweli hii ni fikra tunduizi?!!!

Kweli mashuleni kuna kazi....loooh 😪😪😪
 
Hiyo fomu ya police (PF) inayoitwa seizure certificate ndiyo imekuwa ikitumika miaka tangia mwaka 2018 despite hiyo typing/ printing error ya Government Printer ya ku print mwaka 2018 badala ya 2019. Wanasheria bwana, wao kazi yao ni kubishana tu hata kwa mambo madogo madogo kama haya ya typing error. Wewe kama ni shahidi na jina lako ni Wambura lakini limeandikwa Wambula,utakuwa siyo wewe na hutaruhusiwa kutoa ushahidi wako. Yaani kosa dogo la typist/ printer linakufanya usiwe wewe. Busara ya Jaji tunaisubiri kesho.
 
Kama vp kina Kibatala kesho wajitoe tu Kama jaji atazingua... dunia nzima ijue
 

 

 
Mnaukumbuka wito wa Godbless Lema wa kutaka mawakili wa M/Kiti Freeman Mbowe kujitoa ktk kesi ili Jaji ahukumu apendavyo yeye kwa kadiri ya kile kinachodaiwa kuwa "kupokea maelekezo toka juu...?"
Yaani kwa hoja za Mawakili wa Utetezi huyo Judge akichomoa this time around, nitaishushia heshima kabisa kada ya sharia. Nitaidharau sana sana, heri kuwa mganga wa kienyeji kuliko kuitwa Msomi usie msomi!

Elimu ya Tanzania itazidi kudharaulika, wanasheria walianza kudharaulika baada ya Kabudi kuongea ujinga mwingi Mara nyingi na Leo hii Law Society imebakiwa na nafasi hii tu narudia nafasi hii peke yake kulinda heshima ndogo waliyobaki nayo
 
Yaani unataka kuhalalisha na hili pia? Kutumika miaka hata mia moja haimaanishi iendelee kutumika! Ni ujinga saan na kama kweli imekua ikitumika basi kuna watu watakua wamedhulumiwa haki zao kwa makusudi
 
Mahakama haileti busara Bali inatafsiri Sheria kwa namna mlivyokua mnabishania vifungu, hivyo Kesho jaji hatakiwi kuleta busara Bali kutafsiri Sheria ila ajue atakachoamua pia kitakua cited kwenye kesi ingine siku nyingine
 
H
Akili za kichadema hizi ni comedy tosha
Huoni comedy ya jaji kuanzia mwanzo mpaka ya leo? Hilo ni swala la kuomba siku nzima wakati reference zipo kibao.Ajitahidi mahakama iendelee kuheshimika.Otherwise washtakiwa wakiamua kufunga midomo kwa kutumia vitambaa vyeupe ni aibu kwa taifa la Tanzania.
 
Sio kama wanaijua, sema wanaijua. Kwenye kesi hizi ni lazima kuiba taarifa kutoka upande wa pili. Kwamba shahidi anaefuata ni ni nani na anakuja na ushahidi gani?

Upande wa Jamhuri kuna wasamalia wanavujisha taarifa.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Mahakama haileti busara Bali inatafsiri Sheria kwa namna mlivyokua mnabishania vifungu, hivyo Kesho jaji hatakiwi kuleta busara Bali kutafsiri Sheria ila ajue atakachoamua pia kitakua cited kwenye kesi ingine siku nyingine
Kwa hiyo mahakamani hakuna busara bali kuna sheria tu, zilizotungwa na akina Msukuma na Bajaji!

Kwa hiyo mahakamani hakuna haki bali kuna sheria tu? Unaweza ukawa sahihi. Tutaona kesho.
 
Kwa hiyo mahakamani hakuna busara bali kuna sheria tu, zilizotungwa na akina Msukuma na Bajaji!

Kwa hiyo mahakamani hakuna haki bali kuna sheria tu? Unaweza ukawa sahihi. Tutaona kesho.
Kwenye busara ndo hapo akina jaji Siyani walipochafua jina kwa kuanza kuleta ushabiki na maagizo toka juu. Ila tu wajue hukumu Moja hua inatumika kama Sheria kwenye kesi nyingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…