Kesi ya Wamiliki Ghorofa lililoporomoka na Kuua Kariakoo yaahirishwa hadi Januari 13, 2025

Mtoa Taarifa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2024
Posts
213
Reaction score
671

Mahakama ya Hakimu Kisutu iliyopo Dar es Salaam, imeahirisha kesi inayowakabili wamiliki wa jengo la ghorofa lililoporomoka eneo la Kariakoo hadi Januari 13, 2025 kwa ajili ya kutajwa.

Kesi hiyo imeahirishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo Godfrey Mhina baada ya Wakili wa Serikali Roida Mwakamele kuieleza mahakama kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika hivyo kuomba mahakama ipange tarahe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Wamiliki hao ni Leondela Mdete, Zenabu Islam (wote wakazi wa Kariakoo) na Ashour Awadh Ashour (mkazi wa llala) ambao kwa pamoja wanakabiliwa na shtaka la mauaji pasipo kukusudia.

Wamiliki hao wanatuhumiwa kushindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo na hivyo kusababisha vifo vya watu 31 baada ya ghorofa wanalomiliki eneo Mtaa wa Mchikichi na Congo, Dar es Salaam kuporomoka Novemba 16, 2024.

Baadhi wa washtakiwa hao wapo nje kwa dhamana huku wengine wakikosa vigezo vya kupata dhamana, na kuendelea kusota rumande.
 
Tamaa imewaponza! Wacha wasote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…