Kesi za kubambikiza: Uamuzi mgumu na sahihi ni kutojitetea na kuwaacha waamue watakavyo

Kesi za kubambikiza: Uamuzi mgumu na sahihi ni kutojitetea na kuwaacha waamue watakavyo

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Naamini ipo siku atatokea mtu jasiri ataeamua kutojitetea mahakamani pindi atapobaini mashitaka dhidi yake ni ya kubambikiziwa kwasababu tu ya chuki za kisiasa au vinginevyo.

Huweki Wakili unawaacha waendeshe kesi bila wewe kusema lolote halafu mwisho wa siku watoe hukumu waliokuwa wamepanga roho zao zisuuzike.

Narudiia, mtu wa kuandika historia ya aina hiyo yupo na siku moja atapatikana.

Kama tunavyosikia, mtu anatuhumiwa kutamka maneno haya au yanayofanana na haya: "safari hii tutakupa kesi ambayo hutachomoka" na mtu huyo wala hajitokezi kukanusha au hata kujitetea?

Mtu wa aina hiyo, siku akipatikana, huenda akawa chachu ya kubadili kabisa mifumo ya utoaji wa haki nchi hii na ataenda jela akiwa ameandika historia kubwa na ya kipekee kwa nchi hii.

Ipo siku.
 
Naamini ipo siku atatokea mtu jasiri ataeamua kutojitetea mahakamani pindi atapobaini mashitaka dhidi yake ni ya kubambikiziwa kwasababu tu ya chuki za kisiasa au vinginevyo.

Huweki Wakili unawaacha waendeshe kesi bila wewe kusema lolote halafu mwisho wa siku watoe hukumu waliokuwa wamepanga roho zao zisuuzike.

Narudiia, mtu wa kuandika historia ya aina hiyo yupo na siku moja atapatikana.

Kama tunavyosikia, mtu anatuhumiwa kusema : safari hii tutakupa kesi ambayo hutachomoka" na mtu huyo wala hajitokezi kukanusha au hata kujitetea?

Ipo siku.
Ni swala la muda tu kauli hizi zimekuwa za kutosha mitaani cku izi
 
Back
Top Bottom