Keto weight loss tablets mlio jaribu tupeni matokeo

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Hii ndiyo habari ya mjini, mlioijaribu tuelezeni matokeo.
 
hivi vidonge si vina madhara sana kiafya?
 
Nahisi mnatafuta vidonda vya tumbo.

kuna mdada ninapofanyia kibarua kila siku anabadilisha mimaji ya sijui:-
Hiliki
Mdalasini
Mara matango
Mara diet
Mara malimao ajikondeshe lakini waaapi [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28] anaendelea kuwa chibonge [emoji1][emoji1][emoji1] nidhamu ya kula hana atapunguaje??

Achaneni na hiyo midawa fanyeni mazoezi ya mepesi ya kukimbia kwa dk 20 huku umevaa jaketi siyo kawoshi wala singlendi ili mwili uvuje jasho la kutosha na kunywa maji ya mengi. Kula vyakula vyenye wanga kigodo na matunda mengi.

Menu ya mchana kama unafanya kazi ofisini kula matunda tu na maji mengi, usiku wanga kidogo na mbogamboga au white meat (kidongo) achana na bia, soda na juisi za viwandani ila vinywaji vikali ruksa kama ni lazima saaana

matokeo ni baada ya wiki 3 hadi 4,

Usisahau kikombe kimoja cha maji ya moto yenye limao kila asubuhi.
 
diet gani hiyo, tuelimishe
Niliacha kutumia
-Soda/vinywaji vyote vya kiwandani
-Vitu vyote vinavyotengenezwa na ngano
-Wali
-juice yoyote ya matunda ya kutengeneza
-Vitu vyenye sukari nyingi (hii haikunisumbua maana hata mimi sivipendi)


Asubui nakunywa maziwa tu
Mchana nakula mboga za majani na ugali kidogo/Nyama ya kuku maana ya Ng'ombe pia niliiacha/Samaki
-Katika mboga siweki mafuta mengi

Usiku nakula Tango,Parachichi nalala

Katika kutwa yangu nzima lazima Maji lita2, machungwa mawili


Week1 tumbo lote likaisha .. nikivaa sasa hivi nakua kama nmevaa mkanda wa kubana tumbo
Toka kilo 70 mpk 62 now, najiskia mwepesi ajabu
 
safi sana, nami nitaleta mrejesho
 
Kuna nyingine unakula kuku, samaki au mayai ya kuchemsha pamoja na salad πŸ₯— kwa lunch na dinner.

Breakfast ndizi mbivu moja na mayai mawili ya kuchemsha.

Maji ni muhimu.
 
Hii ndiyo habari ya mjini, mlioijaribu tuelezeni matokeo.
View attachment 1144865


Aisee, kumbe sky ni tipwatipwa?!!😁😁, tetema tu ili upunguze uzito.

Fanya mazoezi tu auntie, hayo madawa wazungu wameyatengeneza na kuyaleta huku as case study kwetu ili wajue efficacy zake kabla ya kwenda kutumia wao wenyewe, kumbuka waafrika tumefanywa Guinea pigs in this case for a long time.

Kuna vyakula vingi vya asili vinavyoweza kufanya kazi hiyo moja wapo ni kula mlenda nk.
 
Stress huwa zibanipa challenge sana. Nikiwa na stress ninakula na kunywa mpaka msala uishe ninajikuta niko kwenye 88-90 kg mbaya zaidi BP inakuwa juu lakini nikishuka kwenye 75-80 BP is normal.
 
Hizo pounds zote umeongeza lini? 😳😳

Stress huwa zibanipa challenge sana. Nikiwa na stress ninakula na kunywa mpaka msala uishe ninajikuta niko kwenye 88-90 kg mbaya zaidi BP inakuwa juu lakini nikishuka kwenye 75-80 BP is normal.
 
Stress huwa zibanipa challenge sana. Nikiwa na stress ninakula na kunywa mpaka msala uishe ninajikuta niko kwenye 88-90 kg mbaya zaidi BP inakuwa juu lakini nikishuka kwenye 75-80 BP is normal.


Pole sana auntie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…